Alikuwa na matumaini makubwa ya kuwa waziri toka enzi za Mkapa lakini hakupata na ninafikiri sasa anajuta kuacha kazi yenye mafao ya uhakika kwa tamaa ya cheo cha kisiasa. Yeye na Serukamba huwakosi kwa mshua, utadhani ni house boys.
Hivi ukishinda baada ya kuhonga sana unajisifu kwamba una sifa wakati ni ushawishi wa fedha ndiyo umekufikisha hapo? Ni kama kununua mtihani ukachana pepa halafu ukajisifu. Aibu ya hali ya juu.
Leo katika pita pita yangu maeneo ya Dodoma Hotel, St. Gaspar na maeneo ya Club 84 hali ya unyonge imetawala katika kambi ya mafisadi. Nilimsikia mjumbe mmoja wa Nec toka mkoa mpya wa Simiyu akisema kwamba walikosea kumuacha Mwenyekiti akiacha wagombea kujieleza maana hilo ndilo lililomjenga...
Ni mapema sana kumsifia maana kukitokea suala la M4C Karagwe anaweza kukimbilia huko akawaacha mkishangaa. Nimecheka kusoma stori hiyo, naye akijigamba kutoa laki 2.
Hakuna ubaya, lakini kwa nini huyu bwana atoe sababu zizsizo za ukweli katika mazingira ambayo hata yeye anakiri hajui sababu? Lowassa kila siku anashusha heshima yake.
Sasa nani ana IQ ndogo hapa kama siyo wewe ambaye umehamisha mada na ujinga aliouonyesha huyo mungu wako? Mimi nafikiri haya ndiyo mambo yanayochangia kuzorota kwa afya ya Lowassa. Obsession yake katika kumshambulia Membe bila mafanikio imemuweka katika hamaniko linalomuumiza sana hata kuathiri...
Huku Bonyokwa tuna hasira naye sana. Hata daladala zimeamua kuongeza nauli zikidai barabara ni mbovu na ukweli ni kwamba huku kuna makorongo na toka achaguliwe hajawahi kuonekana wala kufanya lolote. Hata diwani wake hajulikani alipo.
Kwa hakika Tanzania inahitaji muujiza wa Mwenyeezi Mungu maana hapa tulipofika ni pabaya na sijui kama Mungu atakuja kutunusuru kupata viongozi wenye mapenzi ya dhati na watu na nchi hii na kuwaokoa. Sijui nani alimuumba Lowassa na hawa wenzake. Ooh maskini nchi yangu.
Sasa hivi mchakato wa ubunge wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) unaendelea na wiki hii itakuwa ya patashika. Nikitambua kwamba wagombea kibao wamejitokeza kuwania na nafasi za uwakilishi ni chache, kuna habari kwamba kinara mmoja wa ufisadi na mtakasaji wa fedha anaalika wale wote wanaotaka...
Kwanza niliposikia mapacha hawa wanaanzisha gazeti mimi nikajua ni kupanua wigo wa magazeti mamluki baada ya kuona kwamba Habari Corporation imeshashtukiwa na haina tena mvuto wala ushawishi kwenye jamii. Hata mimi nimelipitia na tayari kwenye toleo la kwanza Sitta ameanza kuwambwa msalabani...
Sasa mwisho wake ataishiwa na mistari ya kunukuu maana ile ya Lazaro alishaimaliza kwenye harambee ya Yombo. Mimi nashauri aunde sekretarieti itakayokuwa inaratibu maombi yote ya harambee hizi za nyumba za ibada na kupitia risala na mapambio ya kumsifu kama yanakidhi haja maridhawa za kiutakaso.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.