Sasa hivi mchakato wa ubunge wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) unaendelea na wiki hii itakuwa ya patashika. Nikitambua kwamba wagombea kibao wamejitokeza kuwania na nafasi za uwakilishi ni chache, kuna habari kwamba kinara mmoja wa ufisadi na mtakasaji wa fedha anaalika wale wote wanaotaka kushinda katika kinyang'anyiro hicho, kwa sharti kwamba wale wanaoutaka ubunge huo wamuahidi kumuunga mkono kwenye harakati zao za kutwaa hatamu za uongozi wa nchi hii.
Pamoja na anguko tulilolishuhudia kwa chaguo lake kule Arumeru, nawashauri wale wote wenye kuhitaji kufanikiwa basi wamuine mkubwa huyu lakini wawe waaminifu katika ahadi zao kwake. Kila la heri.
Pamoja na anguko tulilolishuhudia kwa chaguo lake kule Arumeru, nawashauri wale wote wenye kuhitaji kufanikiwa basi wamuine mkubwa huyu lakini wawe waaminifu katika ahadi zao kwake. Kila la heri.