membe ni mnafiki,muongo,hana uwezo wa kuongoza,kigeugeu,mtupu kichwani,hatutaki kiongozi anayetishia watu kuwa 2016 watakimbilia kenya,,wenzie mwakyembe na sitta kimya,lowasa go,edo nenda,lwaiganan jembe mwanaume wa kuchukua maamuzi magumu,nenda lowasa kiboko ya wanafiki wakubwa kama membe
Hakika Lowassa ni mwanaume wa kuchukua maamuzi magumu na mifano iko wazi. Michache kati ya hiyo ni hii:
1. Aliingiza nchi gizani kwa tamaa ya utajiri binafsi na familia yake. Mkataba ule wa Richmond mpaka leo umeiweka nchi kitanzini.
2. Bila aibu wala kupepesa jicho alidai rushwa ya dola milioni 2 kwa muwekezaji aliyetaka kununua NIC.
3. Alichukua maamuzi ya kukatiza makataba wa Dawasa na Bywater na baadae kuliingiza taifa katika hasara ya dola 11 milioni za legal fees walizogawana na Mkono.
3. Alipora viwanja na kuzua migogoro ya double allocation wakati ule akiwa waziri wa Ardhi.
4. Aliiba fedha za maafa kwa waathirka wa mafuriko ya Lindi na Mtwara mwaka 1990 wakati ule akiwa waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu akihusika na majanga.
5. Kwa kukosa upeo na kwa maslahi madogo ya kiimani aliingiza nchi katika makubaliano na dhehebu moja la dini huku akijua kwamba kufanya hivyo kulikuwa kunatishia umoja na mshikamano wa nchi yetu na kukiuka ukweli kwamba serikali yetu haina muegemeo wa kidini.
6. Alipita nchi nzima na husuasani mikoa ya kusini akimwaga ahadi ya kugawa ng'ombe kwa vikundi vya akina mama na kuwahimiza kujenga mabanda ambayo yamegeuka kuwa sehemu za kulaza mbwa.
7. Amechukua maamuzi magumu ya kuwashuhudia wamasai wenzie na hasa wale wa jimbo aliloliongoza kwa miaka 20 wakigeuka kuwa walinzi wa nyumba za watu na sehemu za maegesho ya magari, na wengine wakiwa wasusi wa nywele za wanawake badala ya kuwaendeleza kielimu na kuwawezesha ili kuwaondolea umaskini na kuondoa jinamizi la ukosefu wa ajira analolipigia kelele.
8. Amechukua maamuzi magumu ya kuhakikisha kwamba wilaya ya Monduli anayoyiongoza kama mbunge kwa miongo zaidi ya miwili inageuka kuwa inayotegemea msaada wa chakula kila mwaka na huku bila aibu akipuuza kauli mbiu ya kilimo kwanza.
9. Maamuzi magumu ya kutumia fedha za walipa kodi kwa kuzua safari za Kamati yake ya ulinzi na mambo ya jje kwa ziara zisizo na tija, huku akisafiri kwa daraja la kwanza na mkewe.
10. Maamuzi magumu ya kuwamaliza wabaya wake kwa kuwashambulia kwa sumu na tindikali ili asiwe na ukosoaji au asiwe na ushindani katika medani ya ksiasa, huku akiwa hajui kwamba Mungu naye atampa udhoofu wa afya ambao unatishia ndoto zake za kuelekea magogoni.
Maskini jasiri Lowassa. Mzee kipenzi cha watu kwa maamuzi magumu.