Kazi ya kuongoza nchi ni kazi ngumu sana, hususani TZ, nchi yenye watu zaidi ya milioni 40 wenye mahitaji tofauti, nchi ambayo viongozi waliopewa dhamana ya kuwaongoza wa TZ wamekuwa wakulia lia tu na kulalamikia ufisadi na rushwa iliyokithiri pasi na kuchukua hatua thabiti, nchi iliyojaa...
PhD ama piechi di za makachanjanja, mbona wako wengi wa hizo peichi di huko Mbeya, hata dada mmoja wa chama tawala mbunge wa viti nya upendeleo anayo peichi di ya kupewa, eti nae ni Daktari siku hizi, hata degree ya kwanza hana. Nchi hii sijui tunakoelekea.
Ewe muumba utuepushe na dhahama hii, ndiyo kwanza tupo kati kati ya 2013, mpaka ifike 2015 basi tutashuhudia maovu makubwa ndani ya nchi hii, ile dhana ya "kisiwa cha amani" haipo tena, damu za watu wasio na hatia zinazidi kumwagika, ubinafsi, uroho wa madaraka na ufisadi ndiyo inapelekea yote...
Serikali ijiwajibishe yenyewe, usitegemee upande bangi uote mpunga, haya matokeo ya litarajiwa na bado tusubiri kiama cha matokeo mabovu kwa mtindo huu tuendao. Mungu ibariki Tanzania na kizazi hiki cha utawala usio na muelekeo thabiti.
Kwa maoni yangu, sidhani kama kulikuwa na jambo kubwa sana kwa Mnyika kutimuliwa mjengoni, nafikiri naibu spika halipaswa kuwa na kauvumilivu ili Mh. Mnyika alieleze bunge udhaifu wa Mh. raisi kwa tafsiri aliyokusudia na kama itaonekana aliyoyasema ni uongo then zipo taratibu na kanuni za bunge...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.