Mkuu wa Idara ya habari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Bw. Gervas Lyenda ni amesema Chama chake kipo tayari kushiriki kwenye mchakato wa maridhiano ili kuhakikisha Tanzania inakuwa na amani na utulivu wa kisiasa wa kudumu.
Lyenda amebainisha hayo wakati akifanya mahojiano na chombo kimoja cha habari Jijini Dar Es Salaam, suala ambalo limepokelewa kwa maoni mseto na baadhi ya Wananchi wakiwemo wanachama wa Chadema na baadhi ya wachambuzi wa siasa, wengi wakiunga mkono kauli hiyo kwa maslahi ya Umma na umoja wa Kitaifa.
"Hiki alichokisema Bwana Lyenda kando ya kwenda kinyume na baadhi ya Viongozi wake wakuu ni suala linalotakiwa kuungwa mkono, ni kitendo cha kikomavu katika siasa na demokrasia kinachopaswa kuungwa mkono na...