JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Kwenye hii video Manara anadai kuna Fact ambayo haisemwi kuwa Simba ilianza kuuza jezi na tiketi wiki 5 nyuma. Yanga wametumia wiki 1 tu kuuza tiketi na jezi na zimeisha, huku akisema kuna propaganda ambazo yeye alikuwa anatumia huenda ndio Simba wametumia kuonesha wamemaliza tiketi zao( Sold out) Anesena wana Yanga wajipongeze kwa kumaliza tiketi hizo kihalali. Je, Ni kweli Simba walianza kuuza Tiketi wiki 5 nyuma? Jamiicheck naomba msaada hapa tupate ukweli.
Picha hii inadaiwa kuchukuliwa maeneo ya Ubungo, Dar es Salaam. Inadaiwa kuwa twiga hawa wanasafirishwa kinyume cha utaratibu hivyo mamlaka za Serikali ikiwemo Polisi zifuatilie kwa undani suala hili. Kadhalika picha hiyo imetumika Oktoba 10, 2025 katika mtandao wa Instagram na kuelezwa kuwa "Muongoza watalii huko Zambia amekimbia na Twiga wawili na nyoka mmoja baada ya kuchelewesha kulipwa pesa zake"
Mei 29, 2023 kwenye Mtandao wa Twitter, Mtumiaji mmoja alichapisha andiko linalosomeka kuwa Mwaka 2016 Serikali Ilikataa kumpokea Balozi Mpya wa Zambia Nchini Tanzania Bwana Musenge Mukuma kwa kuwa Jina lake linatoa tafsiri Mbaya Katika Lugha ya Kiswahili. Andiko la aina hii liliwahi pia kuchapishwa Januari 1, 2023 kwenye Mtandao huohuo. Ukweli upoje?
Hello JamiiCheck, Nimeona mtandaoni ukurasa wa Mtandao wa X wa Watetezi TV ukikanusha madai ya kuwahi huchapisha taarifa ya Rais Samia akisema kuna madini kwenye baadhi ya hifadhi zetu na yanapaswa kuanza kuchimbwa kwakuwa Simba na Tembo hawali Madini. Wao wanasema akaunti iliyoposti ni bandia, siyo yao lakini nakumbuka kama niliwahi kuiona mtandaoni siku za nyuma. JamiiCheck fanyieni uhakiki hili suala.
Ninahitaji kufahamu ukweli kuhusu hawa watu wa UNICEF kutoa fedha kwa watu kupitia humanitarian Foundation kutoka kenya ni kweli au matapeli, maana wanakupa maelekezo kisha kukwambia ili upate fedha za UNICEF unatakiwa ulipie kiasi fulani kinachoendana na kiasi utakachopatiwa mfano ulipie elfu 20 kwa account fulani wanazijua wao kisha uwaambie kwamba ushalipia ili wakuingizie Tsh. Milioni 1M.
Klabu ya Simba ambayo ipo nchini Misri katika maandalizi ya msimu mpya 2024/25, leo Julai 14, 2024 imecheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Tersana FC inayoshiriki ligi daraja la pili Misri na kuambulia kichapo cha goli 6-2. Mchezo huo ambao ulikuwa na lengo la kujaribu kikosi chao, Wanalunyasi walijikuta wakipokea kichapo hicho cha goli 6-2 baada ya kiungo wao Debora kupata kadi nyekundu dakika ya 36 huku matokeo yakiwa 2-1. Magoli mawili ya Simba katika mchezo huo yalifungwa na mshambuliaji raia wa Zambia Fred Koblain dakika ya 32 na Kiungo wao mpya Yusufu Kagoma dakika ya 61. Magoli 6 ya Tersana yalifungwa dakika za 12, 26, 41, 54,67 na 76. Mara baada ya mchezo huo makocha wa Simba waligoma kuongelea matokeo hayo kwani ni...
Back
Top Bottom