JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

kumekuwepo na chapisho ambalo linasamambazwa na moja ya ukurasa wa facebook likidai kuwa Inawezekana unatafuta dhahabu machimboni au madukani, lakini ukweli ni kwamba tayari unatembea ukiwa na dhahabu mwilini mwako! Katika chapisho hilo wamedai kuwa Wanasayansi wamethibitisha kuwa ndani ya mwili wa binadamu kuna wastani wa miligramu 0.2 za dhahabu safi. Madini haya ya thamani yanapatikana ndani ya damu yetu yakifanya kazi zake za kibaolojia. Sambamaba na hilo kumekuwepo na madai kuwa Hii ni dhihirisho tosha kuwa kila mmoja wetu ameumbwa akiwa na thamani kubwa tangu awali. Hivyo basi, thamani yako haitokani na kile unachomiliki kwa nje, bali kile kilichopo ndani yako!
There have been widely circulated social media posts following the outbreak of violence in South Africa. One of the posts claims that the President of Botswana took drastic measures against South Africa, including cutting off electricity supplies and closing the border due to rising xenophobic tensions. The post further alleges that: "President Duma Boko declared a state of emergency, criticizing South Africans for the mistreatment of Batswana and fellow Africans. He also stated that South Africans have failed to recognize that many African nations, including Botswana, supported them during the apartheid era. The conflict allegedly started by South Africans has also worsened the energy crisis in some parts of South Africa.” Claims...
Siku za hivi karibuni, taifa la Afrika Kusini limeendelea kukumbwa na changamoto ya kuongezeka kwa mashambulizi na vurugu za chuki dhidi ya wageni (xenophobia). Maandamano hayo yanadaiwa kulenga kuwaondoa raia wa kigeni nchini humo. Pamoja na kuendelea kwa matukio hayo, kumekuwa pia na ongezeko la matumizi ya picha za zamani na picha zilizohaririwa kwa teknolojia ya akili unde (AI) katika kuelezea matukio ya sasa yanayoendelea nchini humo. Moja ya chapisho lililosambaa kupitia chombo cha habari cha Mwananchi lilikuwa na kichwa kisemacho, “Ukaburu unarejea Afrika Kusini”, kikitumia picha ambayo kwa uhalisia ilipigwa mwaka 2015 wakati wa machafuko yaliyolenga raia wa kigeni katika eneo la Johannesburg Central Business District (CBD)...
Jamani kichwa kinajieleza. Kwanza ni kweli mende anazalisha maziwa? Mende hawa hawa tunaowaona chooni? Sasa maziwa yenye yanakaa wapi na wanakamuaje? Halafu eti inasemekana maziwa ya mende yanavirutubisho kuliko ya ng'ombe, si makubwa haya! Mende walivyo wachafu na wanavyoogopesha leo mtu ukanywe sijui ule maziwa yake, yaani sitaki hata kupata picha kwakweli. Wakuu hili ni kweli?
Kumekuwepo na chapisho linalosambaa kwenye mtandao wa Facebook likimuonesha Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Paul Kagame, akipiga magoti mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, wakati wa ziara yake ya siku moja nchini Tanzania. Je ?ni upi uhalisia wa chapisho hilo la picha ambalo lina sambaa kwa kasi kwenye mitando ya kigiditali..
Katika baadhi ya nyakati, wakazi wa maeneo ya kanda ya Ziwa, hususan wilaya ya Ukerewe, wameripoti kushuhudia maji ya Ziwa Victoria yakibadilika rangi na kuonekana ya buluu kijani kibichi chenye mchanganyiko wa bluu Hali hii huwavutia na kuwashangaza wengi kutokana na kutokuwa ya kawaida. Kwa mujibu wa maelezo ya wakazi wa maeneo hayo, tukio hili hujitokeza zaidi katika mwezi wa sita (Juni), hasa kuanzia majira ya asubuhi (karibu saa moja) hadi mchana, na kisha huonekana tena kwa kiwango kikubwa zaidi nyakati za jioni. Uchunguzi uliofanywa kwa kutumia nyenzo mbalimbali umebaini kuwa mabadiliko hayo ya rangi husababishwa na kuongezeka kwa maua hatari ya mwani (Harmful Algal Blooms – HABs), hasa jamii ya cyanobacteria. Ukuaji huu...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…