Katika baadhi ya nyakati, wakazi wa maeneo ya kanda ya Ziwa, hususan wilaya ya Ukerewe, wameripoti kushuhudia maji ya Ziwa Victoria yakibadilika rangi na kuonekana ya buluu kijani kibichi chenye mchanganyiko wa bluu Hali hii huwavutia na kuwashangaza wengi kutokana na kutokuwa ya kawaida.
Kwa mujibu wa maelezo ya wakazi wa maeneo hayo, tukio hili hujitokeza zaidi katika mwezi wa sita (Juni), hasa kuanzia majira ya asubuhi (karibu saa moja) hadi mchana, na kisha huonekana tena kwa kiwango kikubwa zaidi nyakati za jioni.
Uchunguzi uliofanywa kwa kutumia nyenzo mbalimbali umebaini kuwa mabadiliko hayo ya rangi husababishwa na kuongezeka kwa maua hatari ya mwani (Harmful Algal Blooms – HABs), hasa jamii ya cyanobacteria. Ukuaji huu...