JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

LISSU KWENYE UKURASA WAKE WA X (TWITTER) AMENENA MAZITO ASEMA HATA AKIBAKI MWENYEWE CHADEMA ITASONGA. Hayo yamekuja mara baada ya viongozi mbalimbali wa Kanda wa CHADEMA kujiuzulu kwa madai ya Chama chao (CHADEMA) kukosa Muelekeo na Kwenda kujiunga na ACT wazalendo ili kuongeza nguvu kwenye chama chenye nia ya mabadiriko ya kweli sio kwa Sasa CHADEMA imejifia kifo cha asili sema viongozi taifa hawataki kusema ukweli.
Wakuu hii taarifa nimekutana nayo Facebook je, ni ya kweli? 𝐁𝐎𝐍𝐈 𝐘𝐀𝐈 𝐊𝐔𝐉𝐈𝐔𝐙𝐔𝐋𝐔 𝐍𝐀𝐅𝐀𝐒𝐈 𝐘𝐀 𝐔𝐄𝐍𝐘𝐄𝐊𝐈𝐓𝐈 𝐂𝐇𝐀𝐃𝐄𝐌𝐀 𝐊𝐀𝐍𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐏𝐖𝐀𝐍𝐈 Habari za ndani kabisa ya CHADEMA zinasema bundi ameendelea kulia; safari hii Boni Yai akitajwa kuwa mbioni kujiuzulu kutoka nafasi ya Uenyekiti wa chama hicho Kanda ya Pwani, na kwamba barua yake ya kujiuzulu tayari ameshaiwasilisha kwa Katibu Mkuu John Mnyika. Hatua hii inatokana na kutokukubaliana na uongozi mbovu wa Tundu Lissu na migogoro inayoendelea ndani ya chama hicho. Kujiuzulu kwa Boni Yai kunadhihirisha mpasuko mkali ndani ya CHADEMA, huku migawanyiko ya kimtazamo ikizidi kuleta mvutano mkubwa kati ya wanachama na viongozi wa juu wa chama.
Ndugu zangu Watanzania, Unaweza kusema ya kuwa Mheshimiwa Boniface Jacob ameamua kujiweka pembeni ya ulingo na masuala mazima ya siasa za CHADEMA na kuamua kujikita kwenye shughuli zake binafsi za kijasiriamali. Ambapo Mheshimiwa Jacob ambaye ni Mayor wa zamani wa Ubungo ameonekana akiwa katika chumba au ukumbi wenye Trei za mayai Mengi sana. ambayo ni biashara amekuwa akiifanya kwa muda mrefu sana na ambayo imeonekana kumpatia matokeo chanya na faida kubwa sana. Amepongezwa sana mitandaoni na watu mbalimbali na wa vyama tofauti tofauti kwa juhudi zake kubwa na kuwa mfano wa Kuigwa katika mapambano ya kukabiliana na umaskini na kujikwamua kiuchumi. Wengi wamemsifu na kusema kwa hakika anapaswa kupewa sapoti na kuungwa mkono sana...
𝗞𝘂𝗻𝗮 𝗷𝗶𝘄𝗲 𝗸𝘂𝗯𝘄𝗮 𝗹𝗶𝘁𝗮𝘀𝗵𝘂𝗸𝗮 𝗻𝗰𝗵𝗶𝗻𝗶 𝗧𝗮𝗻𝘇𝗮𝗻𝗶𝗮 𝗺𝘄𝗮𝗸𝗮 𝟮𝟬𝟯𝟮 Watafiti kutoka Nasa wameshaanza kutoa ripoti kuhusu jiwe kubwa litakalo weza shuka duniani ambalo linaitwa asteroid 2024 YR4, na kuibua wasiwasi juu ya maafa yanayoweza kuhalibu baadhi ya miji kwenye nchi kadhaa. Imelipa jina la ukanda wa hatari "risk corridor" litakaloweza kuathiri baadhi ya nchi kwa mawe hayo makubwa kushuka Kuanzia ukanda wa kaskazini Ya Amerika ya kusini kuvuka bahari ya pasifiki, ukanda wa kusini mwa bara la Asia, pamoja Afrika upande wa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.
WanaJF Nimekutana na taarifa hii huko mtandaoni. Je, ina ukweli wowote? Hali ya kiafya ya Mheshimiwa Tundu Lissu, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), imeendelea kuzorota, hali iliyolazimu apelekwe nchini Ubelgiji kwa matibabu ya dharura. Kutokana na changamoto za afya zinazomkabili, madaktari wameshauri apokee matibabu maalum ili kurejesha afya yake haraka. Wananchi, wanachama wa CHADEMA, na wapenda demokrasia kwa ujumla wanaombwa kuendelea kumuombea, pamoja na kuchangia kwa hali na mali ili kufanikisha matibabu yake. Ushirikiano wa Watanzania utasaidia kuhakikisha Mheshimiwa Lissu anapata huduma stahiki na kurejea katika hali yake ya kawaida haraka iwezekanavyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema kuwa juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zimeifanya Tanzania kuwa kinara barani Afrika katika uzalishaji na usambazaji wa umeme. Akizungumza na wanahabari katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) mkoani Pwani siku ya Jumapili Februari 16, 2025, Msigwa amesema kuwa mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika kuhusu nishati uliofanyika Januari 27-28, 2025 jijini Dar es Salaam, ni uthibitisho wa mafanikio ya Tanzania katika sekta hiyo. Kwa mujibu wa Msigwa, hali ya upatikanaji wa umeme nchini imeimarika na kufikia 78.4%, huku serikali ikipanga kuhakikisha asilimia 100 ya Watanzania wanapata huduma hiyo...
Wakuu nimekutana na hii taarifa mtandaoni kwenye magroup ya facebook. Je, ni ya kweli? === 𝗠𝗔𝗥𝗜𝗔 𝗦𝗔𝗥𝗨𝗡𝗚𝗜 𝗔𝗧𝗢𝗔 𝗧𝗔𝗠𝗞𝗢 𝗞𝗔𝗟𝗜 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 Mwanaharakati Maria Sarungi ameweka wazi msimamo wake kuhusu CHADEMA, akieleza kuwa kwa hivi sasa hayupo tayari kukichangia chama hicho. Ameeleza kuwa sababu kuu ya uamuzi wake ni ukosefu wa mipango madhubuti ndani ya chama pamoja na mgawanyiko unaoendelea. Kauli yake imezua mjadala mkali miongoni mwa wafuasi wa chama hicho na wanaharakati wa siasa, huku baadhi wakikubaliana naye na wengine wakipinga mtazamo wake. Hili linakuja wakati ambao CHADEMA inaendelea kujipanga kwa ajili ya chaguzi zijazo na harakati zake za kisiasa.
Baada ya Trump kutangaza kusitisha misaada nchini humo kisa madai ya ukiukwaji wa haki za Binadamu na Wazungu kunyanyaswa na kupokonywa ardhi wanazomiliki ambapo Ramaphosa amemtaka Trump aache kuingilia mambo ya Afrika Kusini kwakuwa hayamuhusu na kusema ardhi ya Afrika Kusini sio ya Trump. “Hii ishu ambayo Donald Trump anaiogopa sana, hii ardhi ni ya kwetu, sijui Donald Trump anahusika vipi na atafanya nini kuhusu ardhi ya Afrika Kusini kwasababu hajawahi kuwa hapa, aitunze America yake na tutaitunza Afrika Kusini yetu, Afrika Kusini ni ardhi yetu na inamilikiwa na Watu wote wanaoishi Afrika Kusini, Afrika Kusini haimilikiwi na Donald Trump” “Nikikutana na Trump nitamwambia, nitamwambia wewe Trump ni Mtu mbaya kwasababu...
Back
Top Bottom