JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Dkt. Wilbrod Slaa Aachiwa kwa Dhamana Yenye Masharti Makali Leo Februari 7, 2025 Mahakama Kuu ya Tanzania leo imemuachia kwa dhamana Dkt. Wilbrod Slaa, baada ya kukaa mahabusu kwa zaidi ya mwezi mmoja. Dkt. Slaa anakabiliwa na shtaka la kusambaza taarifa za uongo kupitia mtandao wa X (zamani Twitter), kinyume na Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015. Masharti ya Dhamana Masharti aliyowekewa ni pamoja na: Kuwa na wadhamini wawili wenye mali isiyohamishika. Kukabidhi hati za kusafiria mahakamani. Kutosafiri nje ya Dar es Salaam bila kibali cha mahakama. Kesi hii imeibua mjadala mkubwa. Serikali inasisitiza umuhimu wa kudhibiti taarifa potofu, huku wanaharakati wakionya kuwa sheria za mtandao zinatumiwa kuzima uhuru wa...
Nimeipata WhatsApp hii, Je ni kweli? Inadai kuwa ipo dawa mpya inayojulikana kama 'strawberry quick' ambayo imekuwa ikitolewa kwa kificho kwa wanafunzi kwa malengo ambayo hayajafahamika hadi sasa. Taarifa inadai zaidi kuwa Watoto wanakula wakifikiri kwamba ni peremende na wanakimbizwa hospitali wakiwa katika hali mbaya. Pia inakuja katika chokoleti, siagi ya karanga, cola, cherry, zabibu na machungwa. JamiiCheck tusaidieni kufuatilia!
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikiwa na historia ya miaka 48 ya uimara, umoja, na mafanikio makubwa, kimeendelea kuwa mwamba wa siasa za Tanzania huku kikijipambanua kama kiongozi wa maendeleo na mshikamano wa kitaifa. Kwa upande mwingine, vyama vya upinzani, kama CHADEMA, vimeonekana mara kwa mara kushindwa kuonyesha uimara wa kisiasa na kusimamia masuala ya msingi yanayogusa maisha ya Watanzania. CCM, kupitia misingi yake imara ya kihistoria, kimefanikiwa kuimarisha uchumi, kuleta amani na utulivu, na kuendelea kushika usukani wa maendeleo ya kitaifa. Kwa mfano, katika awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, CCM imeonyesha jinsi ya kuendesha diplomasia madhubuti, kuimarisha miundombinu, na kutoa fursa kwa Watanzania kushiriki...
Zipo imani na madai ya mbalimbali ya kijamii yanayobainisha namna ambavyo mama anaweza kumdhoofisha (kumbemenda) mtoto wake baadhi ya madai hayo ni: 1. Baba na Mama hawapaswi kujamiiana wakati kipindi cha unyonyeshaji kwa sababu kufanya hivyo hupelekea mtoto wao kudhoofika (kumbemendwa). 2. Lazima mama aoge ajioshe na sabuni kwanza baada ya kujamiiana ndipo amnyonyeshe mtoto wake ili asimbemende. 3. Mama akipata ujauzito wakati bado ananyonyesha anaweza kumbemenda mtoto wake. 4. Mzazi akijamiiana nje ya ndoa akishiriki tena tendo na mwanamke wake anayenyonyesha anambemenda mtoto.
Nimekutana na hii taarifa mtandaoni ikisema mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa kushirikiana na chombo cha utoaji wa huduma za Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa pamoja wametoa mkataba KANJU ENTERPRISES LDT wa kutoa huduma kwa wananchi ya kufanya marekebisho ya majina/taarifa zilizo tofautiana kwenye; Cheti cha Kuzaliwa na NIDA/Kitambulisho cha Taifa. Je ni upi uhalisia wa taarifa hii?
Back
Top Bottom