CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimeibua mkanganyiko mkubwa kwa wanachama na wananchi baada ya kubadili msimamo wake kuhusu kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.Awali, chama kilieleza nia ya kushiriki uchaguzi lakini Freeman Mbowe alinukuliwa akisema hawatashiriki.
Baadaye, chama kilikanusha kauli hiyo kikisisitiza hakijajitoa. Kwa mshangao mkubwa, Oktoba 27, Chadema kimetoa taarifa rasmi ya kutoshiriki uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Novemba 27.Akitoa tamko hilo, Suzan Limo Spika wa kinachoitwa Bunge la Chadema alisema: "Leo tumewaita kwa hoja mahususi kuhusu mchakato wa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa... Chadema imejiondoa rasmi kutoka uchaguzi wa vitongoji, vijiji na mitaa."
Hatua hii imeshtua wengi hasa...