JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Huku kwetu kila kukicha deni linazidi kupaa na maisha kuzidi kuwa magumu. Na hapo tunajinasibu kuwa na amani na utulivu. Burkina Faso mbali ya kuwa katika machafuko kwa muda mrefu, kwa miaka 2 tu Traore kaweza kulipa deni la taifa la Dola Bil. 4. Halafu Tanzania Wasira anajisifu kuwa deni ni la enzi na enzi huku Bi. Mkubwa akijisifia kupokea 'vijisenti' vya mkopo ambavyo hata la maana hatulioni zaidi ya anasa za Mama hiki na Mama kile. Millard Ayo hawezi kuripoti habari kama hii. Media za bongo kazi ni kusifia upumbavu tu.
Magonjwa mbalimbali yametufanya binadamu kubuni tiba aina mbalimbali ambazo zitatusaidia kuondokana na magonjwa hayo. Moja ya tiba iliyobuniwa na binadamu ni pamoja na mkoja wa binadamu kama tiba ya magonjwa mbalimbali. Tena unaambiwa ukipata mkojo wa asubuhi ndio kiboko ya magonjwa kama anavyosema mdau hapa wa mtandao wa JF kuwa Mkojo wa asubuhi ni dawa murua Shuhuda ni nyingi sana, moja ikiwa ni ya mdau huyu wa JF kutibu maumivu ya meno kwa kunywa mkojo wa asubuhi Miaka ya 2013-2016 nchini Tanzania kulitokea kundi la wanunuaji wa mkojo wa binadamu kwa madai kuwa unaenda kutumika kama dawa. Katika ukuaji wangu, mimi ni mmoja wa walioshawishika kutumia mkojo kwa kunywa au kupaka. Kwa kutokuzingatia suala la afya, nimewahi pia kunywa...
Wakuu nimeona hii taarifa kuwa Mbunge wa Chadema wa Nkasi Kaskazini, Aida Khenan, ametangaza kuwa atashiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu, akipinga kaulimbiu ya chama chake ya "No Reform, No Election," inayosisitizwa na Mwenyekiti Tundu Lissu. Taarifa imeongeza kuwa akizungumza na wananchi wa jimbo lake, Khenan alisema kaulimbiu hiyo haina mashiko kwani ni msimamo wa mwenyekiti pekee na si wa wanachama wote. Alibainisha kuwa baadhi ya viongozi waandamizi wa Chadema hawaungi mkono kususia uchaguzi, wakiona kuwa hatua hiyo inakiuka sheria na kuwanyima wananchi haki yao ya kupiga kura. Kama kweli, basi atakuwa amekisaliti chama kilichompa dhamana.
Leo nimeona video ambao imewekewa sauti ya mtu akisema wametumiwa video hiyo kwenye group la shule ya Themihill, video hiyo inaonesha mtu akifungua kitu kinachoonekana kama pen (kalamu) ambacho ndani yake kina risasi na baadaye kufyatuliwa. Anayeelezea video hiyo anadai pen hizo zinagawiwa mashuleni na kuuzwa huku akionesha hofu ya watoto kuuana au wao wenyewe kujidhuru kwa peni hizo. Ningependa kufahamu ukweli kuhusu video hiyo.
TAARIFA KWA WANACHAMA, WANANCHI NA WAPENZI WA CHADEMA TANZANIA Ndugu wanachama, Wananchi na wapenzi wa CHADEMA, Tunapenda kuwajulisha kuwa tarehe ya uzinduzi wa Operation #NoReforms, NoElection – Kanda ya Nyasa (Mbeya) imebadilishwa kutoka 23 Machi 2025 hadi 1 Aprili 2025. Marekebisho haya yamefanywa kutokana na sababu za kifedha na maandalizi yanayohitaji muda wa ziada ili kuhakikisha uzinduzi unafanyika kwa mafanikio makubwa na kwa ufanisi wa hali ya juu. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza na tunawashukuru kwa uvumilivu wenu. Tunaendelea kuwasihi muendelee kuwa na hamasa, mshikamano, na utayari kwa siku hiyo muhimu. Kamati ya Maandalizi: Operation No Reforms, NoElection Kanda ya Nyasa - Mbeya.
Back
Top Bottom