JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Nimekutana na taarifa zinadai kuwa Baltasar Ebang Engonga ameachiwa huru na kurudi mtaani baada ya kukutwa hana hatia kwani Wanawake wale aliokuwa akifanya nao ngono kwenye zile video zaidi ya 400 ni watu wazima na walionekana kuwa wameridhia kufanya na kurekodiwa. Aidha vipimo vilionesha hana ugonjwa wowote wa zinaa na hivyo kuwa huru kwani hajasababisha madhara yoyote kwa jamii. Je, ni kweli au watu wanatupiga huku mtaani wakuu?
Wakuu nimekutana na barua mtandaoni inasambaa inaonekana kuwa ya LHRC ina kichwa cha habari, uimarishwaji wa demokrasia uchaguzi wa serikali za mitaa 2024, barua hiyo inaeleza kuwa Tanzania imeonesha hatua kubwa katika kuimarisha demokrasia kutokana na uchaguzi wa serikali za mitaa. wakuu hapa uhalisia ni upi imetolewa na LHRC kweli?
JamiiCheck imefuatilia hotuba iliyotolewa na Stephen Wasira akiwa kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa mkoani Mwanza tarehe 26-11-2024 ambapo mbali na mambo mengine alisema kuwa Serikali katika awamu hii sita ilinunua magari ya wagonjwa 528, lakini pia CHADEMA ilijipanga kusimamisha wagombea kwa 85% mijini na 60% vijijini.
Back
Top Bottom