JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Inadaiwa huyu jamaa bhana enzi za utumwa, alitumika na masta wake kama mbegu ya kuzalisha watumwa wenye nguvu. Inadaiwa kutokana na kuwa na nguvu, umbo maridadi na urefu wa futi 7 hivyo masta wake alimpa upendeleo wa kipekee wa kumpunguzia majukumu mengi huku kazi yake kubwa ilikiwa ni kulala na kuwapa mimba wanawake mbalimbali ili waweze kumzalia masta wao watoto wenye nguvu ambao wangetumika katika shughuli za kitumwa. Roque Jose Florêncio aliacha idadi kubwa sana ya watoto.
Je, ni kweli kuna Samaki mtu? Maana huku mtaani kuna watu huwa wanatuhadithia namna walikutana na Samaki watu au kuhadithiwa na wengine stori kama waliona mwanamke Mrembo mweupe kama Mwarabu ila amekaa juu ya jiwe au ufukweni au anaogelea kwenye bahara au ziwa. Mwanamke huyo wanaeleza anakuwa na nywele ndefu na chini umbile la samaki wa kawaida ila kuanzia kiunoni ndio binadamu, na wasimuliaji husimulia kuwa ukitaka kumkamata unaona analia na anaomba usimkamate wengine wakidai wana watoto wadogo wananyonyesha, au wana familia hivyo kuomba waachwe huru waondoke. Stori ni nyingi sana huku wakidai samaki watu hao hukamatwa na kuliwa kama samaki wengine huku viwiliwili vyao vikizikwa au kutupwa tena majini. Je, ukweli ni upi JamiiCheck...
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limeeleza masikitiko yake na kulaani vitendo vya upendeleo vinavyodaiwa kufanywa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). TEF limezitaka taasisi zote zinazojihusisha na haki za binadamu, kama LHRC, kulaani vitendo vya ukiukwaji wa haki bila kuegemea upande wowote. TEF imetoa wito kwa LHRC kutoa kauli ya wazi dhidi ya mauaji, utekaji, na vitendo vya ukiukwaji wa haki kwa watu wasio na hatia. Pia, TEF imeshauri LHRC kufanya maboresho ya kimkakati ili kuepuka upendeleo wa aina yoyote unaoweza kudhoofisha lengo lake la kutetea haki kwa uwazi na usawa. TEF inaamini kuwa hatua hii ni muhimu katika kujenga jamii yenye misingi bora ya haki na usawa kwa wote.
Baada ya jana Klabu ya Simba kutoa taarifa kuwa mlinda mlango wao, Aishi Manula alishindwa kusafiri kuelekea Algeria baada ya kupata hitilafu ya kiafya dakika chache kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Haya ndio majibu ya Tanzania One "Siumwi chochote, ila wao ndio wanajua nini kinaendelea. Siwezi kuzungumza chochote, naacha wasimamizi wangu wazungumze." — Aishi Manula
Wanawake wajawazito hupewa tahadhari au hata hukatazwa kabisa kufanya baadhi ya mambo kwa lengo la kuwaepushia madhara yanayoweza kuhatarisha afya zao, pamoja na mtoto aliyeko tumboni. Miongoni mwa mambo yaliyodumu kwa muda mrefu kwenye jamii zetu ni kuzuia wanawake wajawazito kutumia mayai ili kuwalinda watoto wasizaliwe wakiwa na vichwa vikubwa, au wakiwa hawana nywele. Kisayansi, jambo hili lina ukweli kiasi gani?
Back
Top Bottom