Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Zungu, amekanusha madai ya vyombo vya habari yanayodai kuwa baadhi ya wabunge wameitwa kuhojiwa na TAKUKURU kutokana na michango yao wakati wa mjadala wa hotuba ya Rais. Akizungumza bungeni Dodoma Februari 5, 2026, amesema ofisi yake haijapokea wito wowote wala kutoa kibali kwa mbunge yeyote kuhojiwa.
Amesisitiza kuwa kwa mujibu wa kanuni za Bunge, wabunge wana uhuru wa kutoa maoni na kushiriki mijadala bila hofu, shinikizo, kushtakiwa au kuhojiwa. Uhuru huo unalindwa na Ibara ya 100 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na kifungu cha 3C cha Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge.
Soma: TAKUKURU yawaita Shabiby na Kangi Lugola
Hata hivyo, Spika Zungu amesema endapo mbunge atakiuka kanuni za Bunge kwa kuchangia hoja zisizoruhusiwa, Spika ana mamlaka ya kuagiza mchango huo ufutwe au mbunge husika kufuta kauli yake. Akikaidi, hatua za kinidhamu zinaweza kuchukuliwa ikiwemo kupelekwa kwenye Kamati ya Bunge kwa mahojiano.
Amesisitiza kuwa kwa mujibu wa kanuni za Bunge, wabunge wana uhuru wa kutoa maoni na kushiriki mijadala bila hofu, shinikizo, kushtakiwa au kuhojiwa. Uhuru huo unalindwa na Ibara ya 100 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na kifungu cha 3C cha Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge.
Soma: TAKUKURU yawaita Shabiby na Kangi Lugola
Hata hivyo, Spika Zungu amesema endapo mbunge atakiuka kanuni za Bunge kwa kuchangia hoja zisizoruhusiwa, Spika ana mamlaka ya kuagiza mchango huo ufutwe au mbunge husika kufuta kauli yake. Akikaidi, hatua za kinidhamu zinaweza kuchukuliwa ikiwemo kupelekwa kwenye Kamati ya Bunge kwa mahojiano.
