Zuio la kujenga makaburi ya kujenga ni muhimu sana

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Sep 30, 2015
1,526
3,802
Salama wakuu,

Sio leo wala kesho lakini baada ya miaka mingi mbele kutakuja kuwa na changamoto ya maeneo ya kuzikia.

Najua wengi tutasema nchi bado ina maeneo mengi sana lakini ukweli ni kwamba watu wanaongezeka kwa kiwango kikubwa, mwaka 2050 tunategemea kuwa na watu zaidi ya milioni 137 nchini Tanzania. Wakati huo huo, kati ya watu 1000 basi watu sita wanakufa Tanzania.

Binadamu unatakiwa kuishi kwa kutatua matatizo yanayoweza kujitokeza huko mbeleni kabla hayajakukuta, nchi za wenzetu kwa kuona hilo sasahivi wanazika kwenye maghorofa.

Huu utaratibu wa kujengea makaburi, hasa huu utaratibu wa kisasa ni changamoto itakayo kuja kujitokeza miaka mingi ijayo. Pengine wakati hiyo changamoto inakuja kujitokeza mimi sitakuwepo na hata wewe unayesoma hutakuwepo ila andiko hili litakuwepo na litawahukumu.

Sent from my SM-A235F using JamiiForums mobile app
 
wachaga sasa na kuzika majumbani, inakera mno

sijui tutafikaje huko watu wanafuata dini, wanataka kurudi mavumbini
 
Kweli mwanangu.

Tuweke eneo elekezi kuwa ni ukubwa wa kama wa mwili tu. Sio hii ya sasa ivi nafasi ya ka jiko au kastoo kadogo kabis

TEknolojia ikikua basi iwe tu saizi ya kama tofali tu. Kama ni kuyeyusha au kuchoma ni sawa ila mwisho mabaki yawe kidooooogo sana
 
Kuna Nchi huwa Kaburi moja linatumika mara nyingi huko South America na Uarabuni.
 
Salama wakuu,

Sio leo wala kesho lakini baada ya miaka mingi mbele kutakuja kuwa na changamoto ya maeneo ya kuzikia.

Najua wengi tutasema nchi bado ina maeneo mengi sana lakini ukweli ni kwamba watu wanaongezeka kwa kiwango kikubwa, mwaka 2050 tunategemea kuwa na watu zaidi ya milioni 137 nchini Tanzania. Wakati huo huo, kati ya watu 1000 basi watu sita wanakufa Tanzania.

Binadamu unatakiwa kuishi kwa kutatua matatizo yanayoweza kujitokeza huko mbeleni kabla hayajakukuta, nchi za wenzetu kwa kuona hilo sasahivi wanazika kwenye maghorofa.

Huu utaratibu wa kujengea makaburi, hasa huu utaratibu wa kisasa ni changamoto itakayo kuja kujitokeza miaka mingi ijayo. Pengine wakati hiyo changamoto inakuja kujitokeza mimi sitakuwepo na hata wewe unayesoma hutakuwepo ila andiko hili litakuwepo na litawahukumu.

Sent from my SM-A235F using JamiiForums mobile app
Kuna wakati nilipiga hesabu nikaona kuwa, katika miaka 100 ijayo, watu wakiendelea kuzikana kwa makaburi mapya, watatumia ardhi kubwa kama nchi ya Gambia.

Matumizi haya ya ardhi, hususan sehemu za mijini au karibu na mijini, yatapunja vizazi vijavyo ardhi.

Miaka ya zamani, hapo Dar, Upanga, kulikuwa na mpango wa kuunganisha barabara kutoka Upanga chini kwenda Upanga juu, barabara ya Maliki kuanzia Muhimbili Primary School hapo United Nations Road.

Kulikuwa na umuhimu kuunganisha barabara ili watu waweze kuwahishwa hospitali ya Muhimbili kwenye dharura.

Tatizo likawa, hapo katikati kuna makaburi ya miaka mingi sana ya Jumbe Tambaza.

Ikabidi serikali iyahamishe yale makaburi, yafukuliwe, watu wazikwe sehemu tofauti pale, barabara ikatishe katikati ya makaburi.

Ndiyo ile barabara ilivyopata kuunganisha Maliki ya Upanga chini na Maliki ya Upanga juu.

Ukiangalia mfano huu, huko baadaye kutakuwa na matatizo sana ya land use na tukiendelea kuzikana tutawapunja watu wa vizazi vijavyo nafasi.

Moja ya suluhisho ni kuacha juzika, kufanya cremation au mazishi ya aina nyingine ambayo hayatumii ardhi.

Changamoto kubwa ni suala la utamaduni, itakuwa si rahisi watu kuwa practical katika suala hili, na kuacha utamaduni wao wa kuzika walioufuata kwa miaka mingi.
 
Salama wakuu,

Sio leo wala kesho lakini baada ya miaka mingi mbele kutakuja kuwa na changamoto ya maeneo ya kuzikia.

Najua wengi tutasema nchi bado ina maeneo mengi sana lakini ukweli ni kwamba watu wanaongezeka kwa kiwango kikubwa, mwaka 2050 tunategemea kuwa na watu zaidi ya milioni 137 nchini Tanzania. Wakati huo huo, kati ya watu 1000 basi watu sita wanakufa Tanzania.

Binadamu unatakiwa kuishi kwa kutatua matatizo yanayoweza kujitokeza huko mbeleni kabla hayajakukuta, nchi za wenzetu kwa kuona hilo sasahivi wanazika kwenye maghorofa.

Huu utaratibu wa kujengea makaburi, hasa huu utaratibu wa kisasa ni changamoto itakayo kuja kujitokeza miaka mingi ijayo. Pengine wakati hiyo changamoto inakuja kujitokeza mimi sitakuwepo na hata wewe unayesoma hutakuwepo ila andiko hili litakuwepo na litawahukumu.

Sent from my SM-A235F using JamiiForums mobile app
Upo tayari mwili wako uchomwe moto majivu yatupwe baharini au mashambani?
 
Kuna wakati nilipiga hesabu nikaona kuwa, katika miaka 100 ijayo, watu wakiendelea kuzikana kwa makaburi mapya, watatumia ardhi kubwa kama nchi ya Gambia.

Matumizi haya ya ardhi, hususan sehemu za mijini au karibu na mijini, yatapunja vizazi vijavyo ardhi.

Miaka ya zamani, hapo Dar, Upanga, kulikuwa na mpango wa kuunganisha barabara kutoka Upanga chini kwenda Upanga juu, barabara ya Maliki kuanzia Muhimbiki Primary School hapo United Nations Road.

Kulikuwa na umuhimu kuunganisha barabara iki watu waweze kuwahishwa hospitali ya Muhimbili kwenye dharura.

Tatizo likawa, hapo katikati kuna makaburi ya miaka mingi sana ya Jumbe Tambaza.

Ikabidi serikali iyahamishe yale makaburi, yafukukiwe, watu wazikwe sehemu tofauti pale, barabara ikatishe katikati ya makaburi.

Ndiyo ile barabara ilivyopata kuunganisha Maliki ya Upanga chini na Maliki ya Upanga juu.

Ukiangalia mfano huu, huko baadaye kutakuwa na matatizo sana ya land use na tukiendelea kuzikana tutawapunja watu wa vizazi vijavyo nafasi.

Moja ya suluhisho ni kuacha juzika, kufanya cremation au mazishi ya aina nyingine ambayo hayatumii ardhi.

Changamoto kubwa ni suala la utamaduni, itakuwa si rahisi watu kuwa practical katika suala hili, na kuacha utamaduni wao wa kuzika walioufuata kwa miaka mingi.
Iringa TANESCO walitaka kupitisha Nyaya za Umeme juu ya kaburi la mzee mmoja,Umeme Ulikuwa haupiti,Yaani ng'ambo hii Umeme upo lkn ng'ambo ya pili bilabila ikabidi walizunguke kaburi.Nyie Mambo haya kuna nguvu kubwa sana ya kiroho,si suala la kuhamisha hamisha tu makaburi wala kuchoma choma maiti.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Iringa TANESCO walitaka kupitisha Nyaya za Umeme juu ya kaburi la mzee mmoja,Umeme Ulikuwa haupiti,Yaani ng'ambo hii Umeme upo lkn ng'ambo ya pili bilabila ikabidi walizunguke kaburi.Nyie Mambo haya kuna nguvu kubwa sana ya kiroho,si suala la kuhamisha hamisha tu makaburi wala kuchoma choma maiti.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Wabongo wengi hata wakikosea kuunganisha nyaya juu ya makaburi tu, umeme usipite, watakimbilia kusema kuna mambo ya kiroho hapa.

Bila hata kufanya uchunguzi zaidi.

Ni tabia fulani ya uvivu kutaka kukimbilia majibu rahisi.

Kama kweli kuna mambo ya ajabu hapo hiyo ikikuwa ni bonge la deal kualika dunia nzima ije kuangalia maajabu. Mbona hatukuona hili?
 
Makaburi ya Kisutu huwa hayajai?
Tangu nakuwa mpaka leo nusu karne bado nasikia watu wanazikwa hapo
Au
 
Back
Top Bottom