Zuia Utapeli Special Thread

Zuia Utapeli Special Thread

Airmanula

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
3,524
Reaction score
5,785
Habari wanajukwaa na wote kwa ujumla. Tafadhali sana mods naomba msiondoe huu uzi sababu nimefikiria itakua very helpful kwa ajili ya kuripoti utapeli unaofanyika haswa kwenye eneo la kutafuta kazi, biashara na mengineyo.

Hii itasaidia sana kuwa expose hapa matapeli kama sio wa humu basi sehemu nyingine ili jamii husika ijue ama iwajue na wachukue tahadhari. Kwaio hapa tunaweza kuweka emails tunazotumiwa za utapeli ama namba zao za simu ama chochote kinachohusiana na utapeli. Pia itakua vema anayetoa taarifa za utapeli anakua na details za kutosha ili jamii ifahamu mana tunajua JAMII FORUM iko kwa ajili ya watanzania wote na marika yote na hata nchi zingine pia.

Fraud.jpg
 
Kutapeli kazi yangu ila si kwa udanganyifu nakutapeli karibia na ukweliukweli
😀😀😀 😡
 
Naomba nilete utapeli unaofanywa ama uliokwishafanywa na hawa wanajiita GOLDEN BISTRO HOTEL ya arusha ...kazi za nafas kibao zilitangazwa zoomtanzania na watu waka apply, lakini katika majibu ya kuitwa usaili wakasema kwamba ili uconfirm ushiriki wako utume shilingi elfu 10 ...
Mimi mmoja wao nliyeomba kazi lakin sikutuma hio elfu 10, lakin cha ajabu email iliyotumika kwamba ndo tutume maombi kule ndio ikatuandikia katika email zetu na zaidi ya watu 500 kwamba eti ni utapeli ...badae mmoja wa walituma hela akaja kusema kwamba eti mhusika kaapiga simu kasema asamehewe kwamba kweli hakuna hio hoteli arusha na hizo kazi hamna kwamba alikua anatafuta ada ya chuo.
Watu wengi wametoa hio elfu 10 ...
 
Back
Top Bottom