Bondpost
JF-Expert Member
- Oct 16, 2011
- 6,603
- 9,380
May be upo sahihi ila najua unajua kwamba serikali ipo kila sehemu ya ardhi yake kwenye nchi hii. Na hapo ndipo kwetu sisi wanasheria huwa tunashangaa sana kwamba inakuwaje watu wanajenga mpaka sehemu inakuwa mji tena mkubwa tu halafu serikali iseme wamevamia????? Hii yote ni kukosekana kwa uwajibikaji serikalini. Watu wanahitaji makazi halafu hawatengewi maeneo na yakitengwa basi serikali inauza viwanja kwa bei ya juu sana ambayomtanzania wa kawaida hawezi kumudu. Unakuta sehemu iliyopimwa wanauza square meter moja kwa elfu 15 sasa ukitaka kiwanja cha square meter 600 unahitaji milioni tisa wakati ukienda unsurveyed area unapewa kwa milioni tatu au nne sasa huoni serikali ndio inachangia haya mambo yote!!!!!! Whether kuna plan au hakuna serikali I walipe fidia hao ni wananchi wake na ni watu wenye familia imagine ingekuwa ni wewe kwa kweli iwaangalie kuwasaidia ndio maana ya kuwa na serikali ni kama mzazi vileRamani za mipango miji zinaonyesha upana wa barara ni mita 243 na ni zazamani tu kama mtu amejenga bila kufuatilia ramani imepanga matumizi gani ya ardhi katika eneo husika hapo asiilaumu serikali