TANESCO kuanza uunganishaji Mitambo kutoka Bwawa la Nyerere (JNHPP)

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetoa taarifa ya kuanza kwa kazi ya kuunganisha kituo cha kupoza umeme cha Chalinze kitakachopokea umeme kutoka Bwawa la Nyerere na Gridi ya Taifa kwenye njia ya msongo wa kilovoti 220 inayoanzia Kinyerezi hadi Morogoro.

TANESCO imesema Kazi hii itakapokamilika itawezesha kupeleka umeme wa Gridi kwenye Mitambo ya Umeme ya Bwawa la Nyerere (JNHPP) kwa ajili ya kuanza majaribio ya mitambo hiyo “Kuanza kwa zoezi hili ni mafanikio makubwa kwa Shirika, na Taifa kwa ujumla kwani tumeweza kuanza mwezi mmoja kabla ya muda uliokuwa umepangwa awali”

“Zoezi hili lililoanza leo tarehe 01 Disemba 2023 litafanyika kwa siku 10 na kukamilika tarehe 10 Disemba 2023, awali zoezi hili lilipangwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Disemba 2023 lakini kuongezeka kwa kasi ya utekelezaji wa mradi wa Julius Nyerere kumewezesha majaribio kuanza mapema zaidi”

“Aidha, kipindi zoezi hili linapoendelea kutakuwa na athari za kutokupatikana umeme katika baadhi ya maeneo yaliyounganishwa na Gridi ya Taifa, kwani njia hiyo ya umeme italazimika kuzimwa kwa siku hizo”

“Kuanza kwa kazi hii ni katika hatua za ukamilishwaji wa Bwawa la Nyerere ambalo litasaidia sana kupunguza na hatimaye kuondoa kabisa makali ya mgao wa umeme, hatua nyingine zitakazofuata baada ya kukamilisha zoezi hili, zitakuwa za kuunganisha kituo hicho na njia ya kusafirisha umeme kutoka Luguruni, Dar es Salaam hadi Morogoro, kuunganisha kituo na njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Ubungo Dar es Salaam, na hatimaye njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze kwenda Tanga, kukamilika kwa hatua hizi zote itapelekea kituo kuwa tayari kupokea na kuingiza umeme wa Bwawa la Julius Nyerere kwenye Gridi ya Taifa, tunaomba radhi kwa
usumbufu utakaojitokeza”
 
Kuna aliyeielewa taarifa hii?
Wanamaanisha makali ya mgao wa umeme yataongezeka kwa sababu watakuwa wanafanya majaribio ya kuunganisha wire za kupeleka bwawa la Mwalimu Nyerere.

Huwa hawakosi sababu.

Mwanzoni walisema kutakuwa na mgao wa umeme kwa sababu wanafanyia service mitambo ambayo kipindi chote cha Magufuli, haikuwahi kufanyiwa. Baadaye wakasema kuna mgao wa umeme kwa sababu wanabadilisha nguzo. Baadaye wakasema kuna mgao wa umeme kwa sababu watumiaji wameongezeka sana kutokana na sera nzuri za uwekezaji za mama. Sahizi ndiyo wamekuja na hii sababu.
 
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetoa taarifa ya kuanza kwa kazi ya kuunganisha kituo cha kupoza umeme cha Chalinze kitakachopokea umeme kutoka Bwawa la Nyerere na Gridi ya Taifa kwenye njia ya msongo wa kilovoti 220 inayoanzia Kinyerezi hadi Morogoro.
naomba radhi kwa
usumbufu utakaojitokeza”
Waache blah blah, watanzania wanataka umeme wa uhakika na wenye gharama nafuu, hizo technical operative schedules hazituhusu sisi watumiaji wa umeme.
 
JNHPP halijaanza uzalishaji umeme wowote kwa kuwa ujenzi wake unaendelea chini ya changamoto kubwa

Maelezo ya mhandisi katika mradi wa bwawa la umeme la JNHPP Rufiji kwa mh. Naibu Waziri Mkuu, jinsi ya kuimarisha mwamba ambao ndiyo msingi wa ukuta na tuta la bwawa la JNHPP Rufiji kitaalamu zoezi linaitwa grout curtain.

Hivyo kwa sasa maji yanafunguliwa kwa wingi yasijaze bwawa maana linaweza kubomoka kutokana na michoro ya ramani ilivyotaka haikufuatwa.

ZIARA YA NAIBU WAZIRI MKUU BWAWA LA JNHPP TAREHE 18 September 2023

Mhandisi wa mradi anafafanua kwa naibu waziri mkuu aliye pia waziri wa nishati Mh. Dotto Biteko juu umuhimu wa kufanya grout curtain kuimarisha msingi wa bwawa kuzuia maji kupenya ktk msingi / foundation kuzuia hatari kubwa ya dhahiri :


View: https://m.youtube.com/watch?v=Y8CkZ4Za7Gw

1701466462177.png


A vertical section through a concrete dam is shown here. The stored water is on the left and the grout curtain is shown in black, with the drainage curtain downstream of it also in black.

seepage under concrete gravity dam


An exaggerated example is shown at a concrete gravity dam where wide cracks in a foundation permit seepage to pass under the dam and emerge downstream.

downwards, counteracts against the water pressure to stop the dam overturning about the downstream toe.

1701466401399.png

3. If there is no grouting under the dam seepage can potentially pass along open cracks at its base and exert pressure upwards. This acts to reduce the effect of the dam's weight and therefore reduces its safety.
The illustration shows a dam tilting about its downstream toe because the dam has insufficient weight to withstand the combined effect of storage pressure and uplift pressure.



4. However, if a grout curtain intercepts the seepage and thereby cuts off most of the uplift pressure, the dam's stability is improved.

 st francis dam failed.

This dam failed because of foundation problems.

Blocks of it tilted around the downstream toe and were then washed downstream by the suddenly released water. One of them remained and can be seen lying on its back beyond the two blocks which did not fail.
 
msingi wa bwawa kuzuia maji kupenya ktk msingi / foundation kuzuia hatari kubwa :

Injinia bwawa la Aswan nchini Misri anafafanua njia ya kukabiliana na uwezekano wa bwawa kuvunjika kwa kutumia utaalamu wa kiuhandisi kuimarisha msingi na tuta kwa kufanya grout curtain kuziba nyufa zinazoweza kupenyeze / kuvuja maji chini ya msingi / foundation.

Grout curtain :

1701467028483.png


THE CONSTRUCTION CHALLENGES ASWAN HIGH DAM, EGYPT

View: https://m.youtube.com/watch?v=0VaCxQnrAFY
The designing of the Aswan High Dam faced many difficulties, for it has to be constructed on a pervious foundation in the lake of the existing Aswan Dam.

The whole extent of the main dam foundation will be covered with a layer of compacted dune sand about 82 feet deep.

The rockfill above this layer will have a clay core made of Nile silt. The dam will be protected against seepage by two lines of defence, a horizontal impervious blanket in the upstream part and a vertical grout curtain descending in the pervious bed of the river to a depth of 690 feet until it strikes natural bed rock.

This grout curtain will plug the voids in the layers of sedimentary materials underneath the dam.
 
Changamoto zilizoelezwa na mhandisi tarehe 18 September 2023 wakati naibu waziri mkuu eneo la mradi wa bwawa la JNHPP, ndiyo zimechelewesha kazi kumalizika kama ilivyoahidiwa huko nyuma :

TANESCO on Twitter: ""Bwawa la JNHPP litaanza kujazwa maji ya ...

21 Feb 2021 — "Bwawa la JNHPP litaanza kujazwa maji ya kuzalisha umeme ... ujazaji wa maji Unatarajiwa kukamilika #15Aprili2022" Dkt. Medard ...

22 Februari 2021
Dr. Medard Kalemani : Ujenzi wa mradi huo umepangwa kukamilika Juni 14, 2022
.

WAZIRI wa Nishati , Dk Medard Kalemani, amesema bwawa la kufua umeme wa maji la Julius Nyerere (JNHPP) litaanza kujazwa maji Novemba 15 2021 mwaka huu na hadi Aprili 15, 2022 litakuwa limejaa.


Dk Kalemani jana alimuagiza mkandarasi na msimamizi wa mradi huo ahakikishe shughuli zote za maandalizi ziwe zimekamilika kabla ya Oktoba mwaka huu ili ujazaji wa maji kwenye bwawa uanze Novemba 15 mwaka (2021) huu.

Alitoa agizo hilo alipombelea kukagua mradi huo unaotarajiwa kuzalisha megawati 2,115. Ujenzi wa mradi huo umepangwa kukamilika Juni 14, 2022.


"Hizi ni habari njema kama tunafikia kuona tunaanza kujaza maji kwa ajili ya kuanza kufua umeme ni faraja kwetu , lakini kwa leo ninaagiza kwa mkandarasi na hili ni agizo mahususi mkandarasi asimamiwe akamilishe kazi hii haraka ndani ya mpango kazi wake " aliagiza Dk Kalemani.


Alisema bwawa hilo litakuwa na kimo cha mita 131, urefu wa mita 1,125 na ujazo wa mita bilioni 35.5 za maji.

Dk Kalemani alitoa maagizo matatu kwa mkandarasi wa Arab Contractors na Elsewedy Electric kutoka Misri aongeze idadi ya wafanyakazi, apeleke vifaa vya kutosha na afanye kazi usiku na mchana.

"Hapa panapojengwa bwawa hili alete wafanyakazi wa kutosha, sijaridhika na idadi ya wafanyakazi waliopo, ninataka kuona kazi hizi zinafanyika usiku na mchana " alisema.

Dk Kalemani alimtaka msimamizi wa mradi huo ahakikishe anamsimamia mkandarasi ili kuona bwawa hilo linajazwa maji ndani ya mkataba na si anavyotaka yeye ya kulijaza hadi Desemba mwakani (2022) na akaagiza kazi hiyo iishe Aprili 2022.

Alihoji kuhusu maelekezo aliyoyatoa kuhusu mapitio ya mpango kazi wa mkandarasi ili aweze kufidia muda unaopotea wa siku 10 hadi 15.

“Mmemweleza nyie lakini mmeniambia hawezi kuuleta na kama hawezi kuuleta anafanya nini hapa, na wewe mhandisi mkazi wa mradi huu nimekuambia una mamlaka kwenye mkataba "alisema Dk Kalemani.

Alisema mhandisi mkazi wa mradi huo, ana uwezo wa kumkataa kiongozi wa wakandarasi (Mohammed Hassan)kwa kuwa yeye (Waziri) hajaridhishwa na ufanyakazi na utendaji wa kiongozi wa wakandarasi.

"Ndiyo maana nimeelekeza mpitieni mkataba mkatae, kwa dalili hii hatuwezi kufika nataka kuona nikataporudi hapa Aprili mwaka huu nisimkute ,nikute msimamizi mwingine, bosi wao mwingine anayeweza kuwasimamia kwenda mbele, hawezi kwenda tofauti na makubaliano ya mkataba na sitaki kuona mkandarasi anapingana na maelekezo ya mwajiri wake " aliagiza Dk Kalemani.

Alisema tayari serikali imemlipa mkandarasi trilioni 1.902 hadi Februari mwaka huu ambazo ni asilimia 100 ya malipo ya mpango kazi wake.

Habari Leo
 
Tanesco taarifa zenu huwa hazieleweki, kwahiyo sasa kuunganisha umeme kupeleka huko bwawani nako kutasababisha mgao wa umeme, hivi ni kusababisha mgao wa umeme au kuongeza mgao wa umeme?

Mimi naona ni kuongeza, kwasababu kama ni mgao tayari tumeshaishi nao kwa zaidi ya miezi mitatu sasa, na mbaya zaidi mlishatumbia, hata kama hilo bwawa likianza kufanya kazi, halitamaliza mgao wa umeme, nashanga kwenye hii taarifa yenu mnajipinga wenyewe kwa kutuambia bwawa litapunguza na hatimaye kumliza kabisa mgao wa umeme!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
“Kuanza kwa kazi hii ni katika hatua za ukamilishwaji wa Bwawa la Nyerere ambalo litasaidia sana kupunguza na hatimaye kuondoa kabisa makali ya mgao wa umeme, hatua nyingine zitakazofuata baada ya kukamilisha zoezi hili, zitakuwa za kuunganisha kituo hicho na njia ya kusafirisha umeme kutoka Luguruni, Dar es Salaam hadi Morogoro, kuunganisha kituo na njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Ubungo Dar es Salaam, na hatimaye njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze kwenda Tanga, kukamilika kwa hatua hizi zote itapelekea kituo kuwa tayari kupokea na kuingiza umeme wa Bwawa la Julius Nyerere kwenye Gridi ya Taifa, tunaomba radhi kwa
usumbufu utakaojitokeza”
Wao wafanye tu maana maelezo ni mengi mpaka yanachanganya, mbinu hii hii itatumika kutuchanganya umeme ukianza kukatika wakati bwawa linafanya kazi
 
Back
Top Bottom