Zitto tena kachafua hali ya hewa bungeni

Au kama kwa hekima yake ambayo inashangaza bado aliona ni lazima kutoa taarifa hiyo ya makabidhiano ambayo Wabunge wengine hawahusiki na wala haiongezi chochote cha maana kwenye hansaRd, kwa nini asingesema tu kuwa ‘nilipewa mchango na Mbunge mwenzetu lakini kwa bahati mbaya nimeshindwa kuusoma' .
Hon.MP Mkuu, hata kama angesema hivyo, kuna uwezekano wewe ukawa wa mwanzo kuichambua hiyo sentensi:
- Mwenzao gani huyo aliyempa mchango?
- Kwa nini akashindwa kuusoma - una matusi ndani yake, una shutuma zisizothibitishwa n.k.

Moja ninakubaliana nawe, kuwa bora angenyamaza. Laiti watu wangekuwa wanaandika kwanza yale wanayotaka kuyasema, baadae wakatumia japo dakika mbili kutafakari athari zinazoweza kutokana na kauli zao!
 
Last edited by a moderator:
Dah haya kajizihirishia kuwa hajui kusoma kwani Lisu aliandika kichina au Kiswahili? Utani kwenye Bunge jamani ifike mahali tuache uvivu wa kufikiri zito Kabwe ni Kansa kwenye siasa za chadema Hilo litaridhihika soon enough. Ntawachukia viongozi wa juu wa cdm kwa kuwa mabubu kwa vimeo Kama hawa.wanatukatisha tamaa sisi tunao volunteer kujenga chama kwani hatuna cha kupoteza Kama vile wao waheshimiwa
 
zito something not good with u'jichunguze na rekebisha mwenendo wako'kila mtu anafanya makosa lakini this is too much'mimi natamani nijue mwisho wako utakuwaje
 
Mi nadhani ni utoto na kulewa sifa za kijinga ndiko kunako mwathili Mh zitto, Tusubiri akikua ataacha, na atakuwa na chekeche la kuchuja mambo ya kuzungumza, maana Mdomo umemponza kwenye kamati yake yeye ndie anayetajwa 2 wengine kama hawapo vile
 
Sidhani kama alikuwa serious kihivyo! Wakati mwingine huwa ni utani, so usiunganishwe na matukio mengine. Wazungu kibao wana miandiko mibaya sana, ingawa wanaweza kuwa wanauelewa wa mambo hayo wanayoyaandika kuliko wenye miandiko mizuri!
 
Watu kila mara wanajiuliza kwa nini kila siku, kila mara, kila mahala ni Zitto, Zitto, Zitto hadi inatia kichefuchefu
Ukweli ni kwamba ni yeye anapenda iwe hivyo kwa kuwa hajakamilisha kazi aliyotumwa. Mpaka pale itakapokamilika, tutaendelea kusikia vitimbwi na show mbalimbali za huyu kijana.


Akihitimisha mchango wako Bungeni, Zitto kasema, “ nilipewa mchango na Tundu Rissu lakini mwandiko wake ni mbaya sana kwa hiyo nimeshindwa kuusoma”. Tujiulize:


1. Je, kweli kulikuwa na ulazima wa yeye kutamka au kutoa taarifa hiyo Bungeni? Faida yake ni nini maana haiongezi chochote (katika mchango wake) wala hawezi kuwahi nafasi kwamba pengine Rissu akirudi basi akute nafasi aliyo ‘bukiwa’ na mwenzake.


2. Hata kama ilikuwa lazima aseme, Je, ilikuwa lazima atamke sababu na kuchagua maneno ‘mwandiko mbaya sana?' angalia kuna kivumishi ‘sana’ kama vile ‘mbaya’ haingetosha!


Si kwamba Zitto ni mzito wa kuelewa, la hasha, anafanya makusudi akijua kuwa mambo kama haya ya kuwadhalilisha wenzake yanaweza kuleta vurugu ndani ya chama na hivyo kukisambaratisha.


Amenihudhi sana, kama si kweli yanayosemwa juu yake, kwa nini asingekaa tu na kutulia kisha aje amweleze Rissu sababu iliyofanya asiwasilishe ujumbe wake. Au kama kwa hekima yake ambayo inashangaza bado aliona ni lazima kutoa taarifa hiyo ya makabidhiano ambayo Wabunge wengine hawahusiki na wala haiongezi chochote cha maana kwenye hansad ,kwa nini asingesema tu kuwa ‘nilipewa mchango na Mbunge mwenzetu lakini kwa bahati mbaya nimeshindwa kuusoma’ .



Kweli sasa tunaaamini, kazi ya double agency ni ya kipuuzi sana maana ni ya kutekeleza kile usichoamini na kuamini kile usichotekeleza! Zitto hawezi kuaminika tena katika jamii ya wasema kweli.

Alikuwa anamtania tu. halafu kwanini wewe umeumia sana na wakati aliyeambiwa wala hajaona kama ni tatizo.
 
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]It is unwise to be too sure of one's own wisdom. It is healthy to be reminded that the strongest might weaken and the wisest might err.

Mahatma Gandhi

[/FONT]
 
Jadilini mambo ya msingi sio mwandiko, kwani mwandiko mbaya haimaanishi mtu hana uwezo, ni kawaida tu sidhani kama zitto alimaanisha vibaya
 
Zitto bonge la kichwa ndani ya chadema vyovyote itakavyokuwa yeye ndo mtu wa kumdiscuss baaaaaasi
 
Wewe ni mmoja wa watu wenye kumuogopa ZITO sana tu and that is ZITOPHOBIA....Huwezi jua zipi ni jokes na zipi sio! Wabunge ni watu km wewe wanaishi kwa kutaniana na sivyo unavyofikiria...ZITO kumpoke LISSU kua muandiko wake ni mbaya it was just utani ili kusogeza maisha mbele....STOP ZITOPHOBIA WEWE KIJANA
 
Who knew that was jokes! Yeye mwenyewe ndio anasema ilikuwa utani na isitoshe tukichukulia hali ya siasa kwa sasa hasa upande wake! Huwezi ukalaumu watu kwa kuhoji ni maneno mangapi yanasemwa bungeni wewe una chukulia utani?

this is what zitto had to respond to one of his tweet followers.

kama great thinkers hatuwezi kupoteza muda kujadili 'jokes Bungeni'

Mods kuweni serious bana. toa hii kitu, au peleka mahala pake

View attachment 60461
 
Hapo kaongea upuuzi na kweli kama kasema hivyo, kuna kazi ambayo katumwa kuitekeleza na inabidi ashughulikiwe mapema
 
Mwenyewe amesha tweet kwamba ni "joke"... basi watu wasitanie hata kwa sekunde..!! Sawa bungeni is a serious place, lakini watu ndio wasicheke? Niambie bunge gani duniani hamna mtu aloyewahi kutoa jokes!
 
Back
Top Bottom