Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

Hivi kulikuwa na ugumu gani kusema tu kuwa "kwa sasa sitaki kuzungumzia mambo hayo; chama changu kiko vitani; tunauchaguzi kwa hiyo sitaki kulizungumzia; niulize kuhusu uchaguzi mdogo nitakujibu".. but noo...
 
Zito umeshasema haya,usijetuambia nimebadili nia oh nimeombwa..2takuona mbabaishaji.
 
Yeye tayari kashasema anautaka urais. Hivi vyeo vya chini tena vya kichama ni kujishusha hadhi.
Kuutaka urais si dhambi na hakusema yeye ndiye anayefaa kuliko yeyote ndani ya chama chake, alichosema ni kwamba katiba iliyoko inawanyima fursa vijana kugombea urais na kama fursa hiyoingekuwepo naye angejitosa kuuwania. Kwa hiyo silioni kosa hapo. Nature ya binadamu ni progressive yaani ni endelevu kwa hiyo si vibaya na kuwa na malengo ya baadae. Baada ya kumpima sawasawa kijana huyu imegundua ni makini kwelikweli na yuko commited na chama chake kulikowatu wanavyofikiria. Ni mkweli, jasiri na mvumilivu na ni hazina tosha ndani ya chama chake, chama cha ukombozi mpya wa Tanzania - CHADEMA.
 
Hivi kulikuwa na ugumu gani kusema tu kuwa "kwa sasa sitaki kuzungumzia mambo hayo; chama changu kiko vitani; tunauchaguzi kwa hiyo sitaki kulizungumzia; niulize kuhusu uchaguzi mdogo nitakujibu".. but noo...
Akisema hivyo unavyoshauri wewe atabeba vipi headlines za vyombo vya habari? hapa ndipo hoja ya umri wa mgombea Urais inapozidi kuwa na mashiko, nina hakika kwa mtu mzima ambaye akili zake zimekomaa hawezi kuongea upumbavu kama wa Zitto.
 
Hivi kulikuwa na ugumu gani kusema tu kuwa "kwa sasa sitaki kuzungumzia mambo hayo; chama changu kiko vitani; tunauchaguzi kwa hiyo sitaki kulizungumzia; niulize kuhusu uchaguzi mdogo nitakujibu".. but noo...

Wewe unabusara sana, unajua watu wengi humu wamekaa kujibu hoja kipropaganda zaidi na kuwachafulia bila kuelewa nao ni wanadamu na wanamapungufu tofauti. Ingawa kwa Mtu makini kama Zitto sikutegemea kama angekuja kukurupuka tena kutonesha makovu ya wabaya wake ambao naona wanaongezeka kila kukicha
 
For this I concur with Zitto.Subira siku zote yavuta heri.Mbowe na Slaa siku zinakuja watamaliza awamu zao.Zitto bado ni kijana sana.You can imagine ten years to come bado Zitto atakuwa chini ya miaka hamsini na ndio muda muafaka kwake na vijana wenzie kukabidhiwa mikoba.Zitto kwa hili ulilosema hongera sana.Tuwaachie lile genge la wahuni litafute mbinu nyingine kufarakanisha viongozi.
 

Nimesikitika sana kujua/kugundua kuwa wewe ni kijana.......

Siyo lazima kila thread hapa JF uchangie.



Shardcole,

Unateseka bure.Ukifanya kazi ya kunifuatilia mbona utapata ugonjwa wa moyo. Tumia muda wako vizuri,kama unanifuatilia mimi na kujiaminisha kwamba unajenga chama basi unatumia muda wako vibaya.Chama ni Taasisi siyo Ben Saanane au mtu mwingine yeyote.

Unaonyesha ulivyo na fikra za ajabu kutaka kutuonyesha chadema kuwa tuko desparate sana hadi kila mtu awe Arumeru.

Arumeru kuna vijana wanafanya kazi,kwenye chaguzi za madiwani kuna vijana wanafanya kazi.Njoo leo kirumba Mwanza kama unadhani ni lazima kila mtu awe eneo ambalo unataka.Njooni kirumba tufunge kampeni

Kuhusu facebook na mitandao,inakuumiza nini mimi kuwa kwenye mitandao?Nikipata muda au ratiba yangu ikikaa vizuri sitaki akili yangu iwe idle ni lazima nibadilishane mawazo na watu kutoka kona mbalimbali za dunia(Ila masaa 24 facebook tena? ha ha haa,Hillarious). Kwa mara ya kwanza JF nimejikuta najibu post ya kijinga kama hii

Naomba uonyeshe post hata moja niliyotukana viongozi wangu wa upinzani.Onyesha mahali nilikomtukana kiongozi specific kwa jina lake .Vinginevyo huu ni muendelezo wa hisia za kutojiamini na kutaka kulazimisha watu waseme unachotaka/mnachotaka kusikia

Nawaheshimu sana viongozi wangu.Heshima ninayowapa viongozi wangu haina ubaguzi.kipimo kile kile ndicho ninachotumia kwa viongozi wote.siwezi kuvumilia au kuwa mnafiki nione mtu anachafua viongozi wa chama changu(kiongozi yeyote yule ndani ya chadema) katika mazingira ya upotoshaji/kumchafua halafu nikaka kimya.Kama hilo unadhani ni jeuri basi wacha niendelee kuwa nayo.Lucky Enough,JF kuna watu wazima,wasomi na wanaojua kuchambua jambo lolote linaloandikwa hapa.

Wiki iliyopita imeaisha watu wakitumia muda mwingi kulalamika kuwa makala ya Zitto inaondoa concentration Arumreu.Niliwauliza Tatizo hapa ni Zitto ama ni sisii tunaoendeleza mjadala ule?watu hawakujibu sasa nifanyeje? Mtu kajibu makala ya mwandishi mwingine,sisi huku nje tunatoa mapovu.Yeyote aliyechangia kwa njia ya mtandao au vyombo vya habari na kutoa maoni juu ya makala ile amechangia kwa kiasi kikubwa kuondoa attention ya uchaguzi wa Arumeru (kama kweli ilikuwa na madhara kiasia hicho)

Nimesikitika sana kugundua kwamba wewe ni kijana mwenye mawazo kama haya katika karne hii.Tunapigania kukomboa vijana kifikra kumbe kazi hii ni ngumu kuliko tunavyofikiria.Ndiyo maana hadi sasa baadhi ya wanasiasa wanajibaraguza kusema juu ya matatizo ya vijana kama vile ajira.Wanajaribu kujijengea Aura ya masiha ajaye huku tukijua wao walisha-mess up na system.Wao ni chanzo cha ukosofu wa ajira.Wanasiasa wa aina hiyo wanataka kuwatumia vijana kama ninyi kama daraja tu.Unashindwa kuhoji ni kwa nini mtu huyu alikuwa kwa mfano waziri mkuu akahusishwa kwenye tuhuma ya kuruhusu mktaba tata ulioligharimu taifa hadi leo suala la ukosefu wa ajira mtu huyo anashindwa kuona uhusiano uliokuwapo kati ya uzembe wake na ukosefu wa ajira.

Wewe kama kijana unashindwa kuhoji haya halafu unajiita mwanachadema?Kama kweli wewe ni mwanachadema basi tambua hatuko vitani baina yetu ila tuna vita dhidi ya sytem mbovu inayozalisha kwa wingi matatizo tuliyo nayo

I pity for this country. We are all being taken for a ride. Tanzania is in a crisis of immense proportions. Some politicians are determined to grab power by all means and if they fail, bring the country down.vijana tunashindwa kuungana kulimamia hili.Tunaingia kwenye bandwagon ya petty politics.Ni aibu iliyoje!
 
Hivi kulikuwa na ugumu gani kusema tu kuwa "kwa sasa sitaki kuzungumzia mambo hayo; chama changu kiko vitani; tunauchaguzi kwa hiyo sitaki kulizungumzia; niulize kuhusu uchaguzi mdogo nitakujibu".. but noo...
MKJJ, thank you for the useful post, sielewi kwanini wengine huwa wanataka kukuza mambo, kuna majibu ya kiuongozi ambayo inabidi mtu ujifunze, 'mimi si msemaji', 'nipe muda nitafuatilia', 'siko ofisini', 'swali hilo linahitaji utafiti' nk.

Jana nilifurahi Mwigulu alivyomjibu mwandishi wa habari kuhusu Sioi kutopiga kura alisema, "hilo sijui lolote naomba unipe muda wa kulifanyia uchunguzi kwa sasa niko mkutanoni" Alijibu hivyo si kwamba alikuwa hajui kuwa Sioi hatapiga kura ila ilikuwa si muda mwafaka kujibu hivyo. Vitu kama hivi vinaonekana kama ukiritimba lakini kwa upande mwingine vinasaidia katika utendaji. Kwa hiyo kama ulivyosema Zitto alikuwa na jibu zuri sana kwa swali aliloulizwa lakini hakulitumia, it was simple.... 'kwa sasa macho yetu yako kwenye uchaguzi nitafute baada ya uchaguzi'.
 
wewe kuwa makini unapotoa maoni yako,mbona hueleweki inamaa haumkubali Zitto au? acha ubaguzi wewe? tumeshakushitukia kuwa wewe mamluki,Zitto kaona mbali ndo maana hagombei,ila kwa wewe huwezijua coz unachuki binafsi.
 

kwani urais ni uongozi ndani ya chama? Au ni wewe usiyejua kupima maneno unapoyasikia?
 
Tunaochangia hoja tuwe makini na tunachochangia sio tunakurupuka tu jamani,sasa huyu anaempinga Zitto wa wapi huyu mbona haeleweki?Zitto kichwa wewe wenzako wanalijua hilo,na kuto kugombea kwake uchaguzi wa ndani ana malengo yake,sio mrohoo wa madaraka,ameshakuwa na dhamira ya urais uwenyekiti au ukatibu wa nini? wacha wagombee werngine,yeye anataka urais tu.mmemuelewa jamani?
 
Zitto kwa hili ulilosema hongera sana.Tuwaachie lile genge la wahuni litafute mbinu nyingine kufarakanisha viongozi.
Zitto kaona isiwe taabu maana ilikuwa too much sasa wengine wakawa wanampa sifa za kumsanifu hadi wana CCM wakajiunga ikawa kama kum kejeri vile, lengo kumchonganisha na viongozi wakuu. Eti uongozi wa juu haufai ni Zitto tu anaweza kuwa mwenyekiti. Zitto kaliona hilo vibaraka wameachwa peupe wamebaki kulalamika pembeni labda waje na singo nyingine.
 
Nani anayeteseka Shardcole au wewe unayeshinda JF ku attack watu kwa kuandika post ndefu kama gazeti la Mzalendo.
 
Hahaha Chadema ni wabaguzi balaa.Muislam mwenyewe mmoja na hawamtaki. Angalau ficheni true colors basi.

Umeliona hilo eee!! Yaani chadema na waislam wapi na wapi?? Chama kimejaa ukabila na udini kinoma, kila mtu analielewa hilo.
 
Nani anayeteseka Shardcole au wewe unayeshinda JF ku attack watu kwa kuandika post ndefu kama gazeti la Mzalendo.

Unalalamika post ndefu eeh...acha kusoma vichwa vya habari na magazeti ya udaku.Ndiyo maana wamewagundua wakaamua kuwatumia tu kuchafua watu hovyo hovyo.Ninyi mnakubali tu

Infact,your posts are laden with so much bigotry that it rarely makes sense for those who do not live in your mind there. only sycophants will support your malicious and scandalous post that can never make impact in the general view anyways.

You are worth to be ignored for now.....! endeleeni kumfanyia Ben monitoring!
 
Chama ni watu na Zitto ni miongoni mwa wanaokijenga Chama Cha Demokrasia na Maendeleo- Kusema anautaka urais hakibomoi chama. Mwentekiti na Katibu na Baraaza la Wazee watakuwepo kukikuza chama Zitto ataongoza Nchi kupitia CHADEMa tatizo liko wapi? Au kuna mtu mmesha muandaa kugombea urais 2015? The early the better tukuze emokrasia ndani ya chama. wajitokeze wanaotaka watangaze nia, tuwachuje mapema kama walikuwa na madhambi wapiga kura tujue. Mnaogopa chama kitasambaratika, hamjakomaa kupambana na misukosuko ya kisiasa? Lazima tutofautiane mawazo, fikra, mitazamo na hisia mwisho wa siku tukubaliane kukubaliana. MAMBO YA ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI HATUZITAKI.
 
Mkuu Ben, punguza kutumia maneno mengi ya kiingereza kwa mtu aliyekujibu kiswahili. Naamini wewe ni mtanzania na unakijua kiswahili vizuri sana. ukipiga ngeli sana unatuchanganya tunaofuatilia mambo humu. Naomba sana mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…