Zitto sasa unakera

Zitto sasa unakera

Retired, analeta hoja zisizo na msingi ; zenye lengo la kupotosha umma na; kuonyesha watu wengine umuhimu wao ni mdogo katika jamii- TAKE HOME- UMBEYA
Fine, umbeya ni nini? Kusema ukweli au kusema uongo. Kati ya hivyo anafanya kipi?
Huku mitaani UMBEYA ni kusema ukweli usiokuhusu! Namkuta mtu anazini natangaza, ni ukweli lakini haunihusu. Does this example hold true for Zito?
 
chige, wakurugenzi wanalipwa mishahara na makampuni yao; kwa vile wanalipwa mishahara wanakatwa PAYE; na kwa kuwa wanamiliki makampuni makampuni waliyoyaanzisha kwa mitaji yao wanalipa kodi ya makampuni nk
Huyo Mkurugenzi aliye kwenye payroll anaingia kwenye kundi la WAFANYAKAZI wote Tanzania ambao ndio hao wanachangia 75% lakini biashara yake inaingia kwenye kundi la biashara zote Tanzania ambazo kwa ujumla wao ndo wanachangia hiyo 25%!

So, hoja ya Zitto, hata huyu Mkurugenzi anaposimama kama Mfanyakazi; nae anastahili kupunguziwa huu mzigo wa PAYE!

Lakini kwa upande wa pili; kama kuna ujanja ujanja huwa anafanya kwenye biashara yake basi aache huo ujanja ujanja na aanze kulipa kodi stahili za biashara zake ili biashara yake yeye na zingine zote Tanzania; wawe wanalipa kodi kubwa zaidi... ili, let's say, ipande from 25% ya sasa to 65%!!

Lakini kama hakuna janja janja yoyote; basi azalishe zaidi na auze zaidi ili hatimae aweze kulipa kodi kubwa zaidi kupitia hiyo biashara!

Of course, kwa hiyo hoja ya mwisho kutimia panahitaji factors zaidi ya moja!

But all in all, hoja ya Zitto inamaanisha jambo moja la msingi: kwamba, mchango wa kodi unaotoka moja kwa moja kwenye mauzo ya makampuni ni mdogo... inawezekana wengi wanakwepa kulipa kodi au ufanisi wa biashara ni mdogo au yote kwa pamoja! Matokeo yake, mlipa kodi mkubwa ni Mfanyakazi kwa sababu yeye hana namna ya kukwepa kodi kama ambavyo Mkurugenzi uliyemtaja anavyofanya kukwepa kulipa kodi stahiki ya biashara yake!

Anything missing?!
 
Zitto ni moja ya wapika data wazuri, usipokuwa msomaji na mfuatiliaji wa mambo utamwamini kwa 100%.

Ukweli ni kuwa zitto ni moja ya wapiga hela wakubwa wa nchi hii.

Hana credibility ya kukosoa ujinga wa serikali.
All are the same.
Sina imani naye na ndo maana binafsi sina muda wa kumsikiliza. Zitto anahangaika kusoma data za wengine. Yeye mwenyewe hajawahi hata siku moja kutengeneza data. Yupo wa pili Bashe ambaye pia sasa ni kila siku data za internet na contradiction kibao!
 
Huyo Mkurugenzi aliye kwenye payroll anaingia kwenye kundi la WAFANYAKAZI wote Tanzania ambao ndio hao wanachangia 75% lakini biashara yake inaingia kwenye kundi la biashara zote Tanzania ambazo kwa ujumla wao ndo wanachangia hiyo 25%!

So, hoja ya Zitto, hata huyu Mkurugenzi anaposimama kama Mfanyakazi; nae anastahili kupunguziwa huu mzigo wa PAYE!

Lakini kwa upande wa pili; kama kuna ujanja ujanja huwa anafanya kwenye biashara yake basi aache huo ujanja ujanja na aanze kulipa kodi stahili za biashara zake ili biashara yake yeye na zingine zote Tanzania; wawe wanalipa kodi kubwa zaidi... ili, let's say, ipande from 25% ya sasa to 65%!!

Lakini kama hakuna janja janja yoyote; basi azalishe zaidi na auze zaidi ili hatimae aweze kulipa kodi kubwa zaidi kupitia hiyo biashara!

Of course, kwa hiyo hoja ya mwisho kutimia panahitaji factors zaidi ya moja!

But all in all, hoja ya Zitto inamaanisha jambo moja la msingi: kwamba, mchango wa kodi unaotoka moja kwa moja kwenye mauzo ya makampuni ni mdogo... inawezekana wengi wanakwepa kulipa kodi au ufanisi wa biashara ni mdogo au yote kwa pamoja! Matokeo yake, mlipa kodi mkubwa ni Mfanyakazi kwa sababu yeye hana namna ya kukwepa kodi kama ambavyo Mkurugenzi uliyemtaja anavyofanya kukwepa kulipa kodi stahiki ya biashara yake!

Anything missing?!
chige, UNAONGELEAJE MSHAHARA NJE YA MWAJIR?
 
Kama akaunti yake haijadukuliwa Mheshiwa Zitto AMENDIKA haya:

mwaka 2016/17 Wafanyakazi wote wa sekta ya Umma na Sekta Binafsi walichangia jumla ya shilingi trilioni 3 kwenye mapato yote ya Serikali kulinganisha na Wenye mitaji ambao watachangia jumla ya shilingi bilioni 900 tu kutoka kwenye kodi za faida/gawio, ongezeko la mitaji na riba (taxes on income/interests, profits and capital gains ). Kwa hiyo 75% ya Makusanyo ya Kodi ya Mapato inatoka kwa Wafayakazi na 25% inatoka kwa Waajiri.

TUCTA inapaswa kutumia takwimu kujenga hoja za kutaka nyongeza za mishahara na kupunguza makato ya Kodi, Hifadhi ya Jamii na hili la 15% ya Bodi ya Mikopo

Swali langu kwake-
Bhakresa na Mengi anawaweka wapi maana wao wanalipwa mishahara na makampuni yao inayotokana na mitaji yao; faida wanayotengeneza inakatwa kodi tena 30%
Bakhresa na Mengi wanaingia humo kwa mishahara ya sekta binafsi. Ni uonevu kutowapandishia wafanyakazi mishahara miaka minne mfululizo. TUCTA hawafanyi yanayowapasa. Wamekuwa kama idara ya Serikali!
 
Sasa hujaelewa nini?..... Makampuni ya Bakhresa na Mengi yamo kwenye hiyo 25% na Wafanyakazi wao wamo kwenye 75% fullstop!
Nashukuru kumwelewesha japo kwa ufupi sana...makampuni ya madini haya ambayo wanayaita ya mapepari wa Lisu kipindi cha nyuma tulipiga kelele sana kuwa wanalipa kodi kidogo ukilinganisha na kodi wanayolipa wafanyakazi wa o, tunahitaji zaidi tujikite hapa tuone uhalisi kulingana na uchambuzi wa kitaalam
 
Zitto ni moja ya wapika data wazuri, usipokuwa msomaji na mfuatiliaji wa mambo utamwamini kwa 100%.

Ukweli ni kuwa zitto ni moja ya wapiga hela wakubwa wa nchi hii.

Hana credibility ya kukosoa ujinga wa serikali.
All are the same.
Kaka si uthibishe kwa kuchambua alichoandika? So simple. Hao waliotishia kumkamata mbona hawajafnya hivyo mpaka sasa?
 
Rafiki asante umeuliza swali zuri wala hakuna haja ya kusubiri Zitto akujibu ntakujibu hapahapa.

Kuna kodi za aina 2 hapo moja analipa Employer ( Corporation Tax=30% ya faida ya kampuni baada ya kutoa matumizi yote ikiwemo mishahara ya wafanyakazi)
Alafu kodi nyingine( PAYE) analipa/anakatwa employee au mfanyakazi kiwango kuanzia 9% ( Anaepata kuanzia Tsh.170,000) mpaka 30% kama anapata kipato kuanzia Tsh.720,000 kwa mwezi.
Kwahiyo Bhakresa na Mengi watakatwa kodi ya PAYE( Pay As You Earn) maana yake lipa kodi kwa Mshahara kulingana na kipato unachopata kama wafanyakazi wengine.

Then, Kampuni italipa kivyake kama imepata faida kodi ya 30% ya mapato yake kama Corporation Tax. Sasa ujue kampuni ikiundwa kisheria haina tena uhusiano wa moja kwamoja na tajiri aliyeianzisha. Kila mtu kivyake.
Hope umenipata mku?
Mjulishe pia kama kampuni imepata hasara hailipi corporation tax
 
Back
Top Bottom