Zitto: Kikwete ni Rais wa ajabu.

Zitto: Kikwete ni Rais wa ajabu.

Kikwete our perfect president

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Zitto anaongea nini?

Anaongea jinsi JMK alivyo wa ajabu kwa kuwa wakubwa wa dunia walikuja na akitukanwa anacheka. Kwa kifupi saana nataka Zitto aelewe kuwa ukiona hao viongozi wanakupenda sana una walakini. Walishasema hawana permanent friend wala enemy. Kuhusu kutukanwa ni kwamba kama angetenda sawasawa asingetukanwa. Alisema ana list ya wauza unga. Aliwafanya nini? Aliruhusu wezi wa EPA warudishe pesa walioiba kimya kimya na hakuna kesi. Nchu gani unaweza kufanya haya. Alisema haijui Richmond, Lowasa kasema hakuna asichojua. Kama Zitto anataka afanyiwe kampeni ya urais kwa kuwa umri umependekezwa kuwwwa 40 aseme. Hayo mengine aachane nayo. Akumbuke kuwa ukitaka kuuza ugumbo nzi ni lazima na tena makalio ya sufuria hayaogopi moto.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Rais Jakaya Kikwete ni mtu wa ajabu na kueleza kuwa kama si uvumilivu wake nchi ingekuwa katika machafuko makubwa.

Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.

Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.

Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.

"Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.

"Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa," alibainisha Zitto.

Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.

"Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu," alisema mbunge huyo.

Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.

Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kung'oa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.

"Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu," alisema.

Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.

"Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa," alisisitiza Zitto.

Habari: JAMBO LEO.

Kwa mara ya kwanza labda naweza kusema naungana na Bw.Zito Kabwe kwa kiasi kikubwa, pamoja na mambo mengine yote Bw.Kikwete anapaswa sana kusifiwa kwa hilo, watu wengi wanachoshindwa kuelewa ni kwamba Raisi wa Tanzania ana nguvu sana, Raisi Kikwete anaweza kuamua sasa hivi kusiwe na Chama cha Upinzani ikawa hivyo, anaweza kuamua Bw.Tundu Lisu awekwe jela maisha na ikawa hivyo, kwa kosa tu la kuhoji muungano, au Bw.Msigwa kumuita Bw.Kinana jangili.

Bw. Slaa amesema mara nyingi sana Majukwaani kwamba Raisi ni Fisadi yeye pamoja na Familia yake, amemdhalilisha sana Raisi Kikwete, lakini ameachwa aseme anavyotaka, watu wengi wanachosahau ni kwamba Raisi Kikwete anaweza kuamua sasa hivi tu CHADEMA ifutwe na hakuna kitu mtafanya mtaishia kulalamika humu basi, anaweza kuamua tu kumshughulikia Bw.Slaa na msimsikie tena na hakuna kitu mtafanya!

Watu wengi wanasahau CHADEMA wanakuwa na kesi wanakwenda Mahakamani na mara nyingine wanashinda kama kesi za Ubunge, kitu ambacho kwa nguvu na ushawishi alionao Raisi wa Tanzania angeweza kuingilia Mahakama na kuzuia, lkn hakufanya hivyo, Bw. Slaa amesema mara nyingi kwamba Nchi haitawalika wakati kuna Raisi wa nchi hilo peke yake lingetosha hata kumpa kesi ya Uhaini lkn ameachwa!

CHADEMA wameanzisha Ukanda kinyume na Katiba ya TZ jambo ambalo wangeweza hata kushitakiwa kwa uhaini wakati wa Mlm Nyerere lkn wameachwa!

Wanaandamana wanavyotaka, kitu ambacho wakati wa mlm Nyerere wasingeweza kufanya wameachwa, kwanza katika hali ya kawaida kama Raisi angeamua kutokana na nguvu aliyokuwa nayo hata hao Wabunge kama akina Bw.Nasari au Lema wasingeshinda Uchaguzi, lkn bado Raisi Kikwete akawaambia watu waacheni tu washinde!

Hivyo pamoja na mapungufu yake naweza kusema Raisi Kikwete ni moja kati ya Maraisi ambao ni wavulimivu sana na labda hajui au hataki kutumia madaraka yake MAKUBWA sana ambayo Katiba inampa kuwashughulikia wanaombeza na kumdharau hata kumuita dhaifu, hilo peke yake nchi nyingine hata TZ yetu ni Uhaini lkn akina Bw.Mnyika bado wanatembea huru, tena siku nyingine wanaalikwa Ikulu na wnashikana mikono, hilo linawezekana Tanzania tu!
 
-Kwenye Sera za Mambo ya Nje hatuangalii matukio ya kutembelewa.Sera yetu ya Mambo ya Nje ambayo tenets zake ni za tangu enzi za Mwl.Nyerere zinatakiwa kufanyiwa overhaul.Leo hii unashindwa kumtofautisha Rais na Waziri wa Mambo ya Nje.Ikiwa unawezesha Marais 2 wa Mataifa makubwa ambayo yana ambitions za kuchota raslimali(Ambition za kibeberu) huku mikataba ikiwa ya Siri na huthubutu kuweka wazi ili watanzania wajue kama tumenufaika ama la,does it make you a vibrant leader? Huo ni udhaifuHatuwezi kujivunia kutembelewa na Mabeberu ikiwa hatujui na wala hatushirikishwi katika mikataba iliyosainiwa.Hapo wananchi tutakua tumemsaidia Chifu Mangungo.2:Economic Diplomacy:Hadi sasa sera zetu za mambo ya nje zimeshindwa kwenda kasi na trend ya Dunia.Kenya wamelichukulua hili kwa umakini.Wizara imeshindwa ku-intergrate wizara ya Fedha na uchumi,viwanda na Biashara,Kilimo,Mali asili na Utalii na wizara ya Uwezeshaji.Tumekomalia uzururaji wa Rais kama nguzo kuu ya sera za Mambo ya nje.Tunatekeleza Sera ya Kuomba na KushukuruMembe ni msomi mzuri kwenye International Relations na ana uwezo lakini Rais hawezi kukwepa lawama za kuingilia Foreign Affairs.Katika mamia ya Ziara za Rais nje ya nchi isije kuonekana kuwa ndiyo utekelezaji wa Sera za Mambo ya nje.Hapana!Kukiwa na Sera imara kila jambo linaenda vizuri badala ya kutegemea kipaji cha kutembea cha Rais.Sera ni institutional Mechanism.Taasisi imara na sio watu imara wa kukata mbuga halafu wanarejea na matunda mwitu yenye sumu na kuiangamiza familia pole pole kwa miaka mingi ijayo.Ni nini sera yetu kwa Afrika?Nini sera yetu specific kwa EU?Ni nini sera yetu kwa Middle East?Ni nini Sera Yetu kwa SADC.Ni ipi sera yetu kwa Latin America?Ni utashi na kipaji cha Rais kuweza kuweka pozi la Picha na wakuu wa nchi hizo tu?Uimara wa Rais hapa Siuoni zaidi ya kipaji chake tu cha kutembea na kuimarisha AlbumActually Rais asingekua na njia nyingine ya kuficha udhaifu wake zaidi ya kutoa uhuru wa maoni ambao ni constitutional Right.Siyo Hisani.
Asante Ben, umewakilisha sehemu kubwa ya mawazo/mchango niliotaka kuutoa. Zitto bana! amefanya uchambuzi kama mojawapo ya magamba!
 
huyu Zitto aliishapoteza consistency matokeo yake anaonekana kama Mnafiki, ni Majuzi tu kwa sauti kali kwelikweli alitoa amri kwa wabunge wa Chama chake kutokuipa serikali hii appreciation kwa namna yoyote ile? Apa anafanya nini? au anataka yeye binafsi ndio aonekane balanced politician?

Alafu anapodai kwamba Jakaya kawa mvumilivu kwa kuruhusu uhuru wa watu kutoa maoni yao anamaanisha nini? uhuru huu tunautumia kikatiba pale unaposhamiri ni katiba yetu inapaswa kupongezwa na pale unapokandamizwa tutamlaani kiongozi anaoukandamiza.

Zitto na Kikwete wanapaswa kukumbuka kwamba hata sisi watanzania tumekuwa wavumilivu sana kwake kwa kutumia madaraka yake vibaya kukwepa majukumu yake ya msingi katika kuisimamia serikali kuboresha maisha ya watanzania.

Taifa letu halijawahi kuwa na agenda ya kimataifa ya kukaribisha marais wa mataifa makubwa wala kuwatembelea, wala kubalance mahusiano yetu na wao, achilia mbali kwamba hii haijawahi kuwa kwenye ilani ya chama chake wala katika ahadi zake, sana sana jinsi anavyolazimisha kudevelop mahusiano ya karibu na mataifa makubwa hasa China na Marekani ndio jinsi anavyotuweka kwenye loosing side, sisi hatuna bargaining power ya namna yoyote ile ya kustrike a win win deal na marekani wala China, tunatumika tu, a wise president should have known that better.
 
ZZK will always be him and one can come close to his mental qualities and stability among our current opposition leaders. anachonishangaza huyu dogo ni kuwa yaani hawaogopi kabisa akina MANGI.. na kama vile anawona akina mnyika kama MBURULA flani hivi.. big up ZZK
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), amesema Rais Jakaya Kikwete ni mtu wa ajabu na kueleza kuwa kama si uvumilivu wake nchi ingekuwa katika machafuko makubwa.

Zitto ametoa kauli hiyo juzi, wakati akizungumza katika Kipindi cha Makutano kinachorushwa na Redio Magic FM ya jijini, Dar es Salaam ambapo alitakiwa kuelezea kipindi cha uongozi wa rais huyo ambaye amebakiza miaka miwili madarakani.

Akijibu swali hilo, Zitto alisema kiongozi huyo wa nchi anapaswa kuheshimiwa kutokana na uamuzi wake wa kuruhusu uhuru wa maoni tofauti na ilivyo kwa viongozi wengi duniani.

Mbunge huyo alisema, huchukia watu wanaposema, Rais Kikwete ni dhaifu na kuwataka kutotumia vibaya uhuru wa kutoa maoni.

“Naomba nisieleweke vibaya, lakini ukweli ni kwamba, Rais Kikwete ameacha kiasi kikubwa uhuru wa watu kutoa maoni. Sasa rais anaweza kutukanwa lakini yeye hachukii. Ni vema wananchi wakaacha kutumia vibaya uhuru huo.

“Kikwete ni mkuu wa nchi aliyejaribu kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa huru. Kama rais angekuwa ni mtu mwenye hasira, ni wazi kwamba nchi ingekuwa katika machafuko makubwa,” alibainisha Zitto.

Pia alimwagia sifa, Rais Kikwete kwa kuimarisha uhusiano wa kimataifa na kuwezesha katika kipindi kifupi viongozi wawili wa mataifa makubwa kuja nchini.

“Rais ame balance (ameweka uwiano sawa) wa uhusiano wa kimataifa. Tunashuhudia ndani ya miezi mitatu marais wawili wanakuja nchini yani Rais wa China, Xi Jinping ambaye alikuja mapema mwaka huu na Rais wa Marekani, Barack Obama anayetarajia kuja nchini, Julai Mosi mwaka huu,” alisema mbunge huyo.

Mbali na sifa hizo, alimtahadharisha rais kuwa anapaswa kuwa makini na watu aliowaita wafaidhina ambao wanateka watu maarufu wakiwamo waandishi wa habari.

Alisema watu hao wanaweza kufuta sifa za uongozi wa Rais Kikwete kutokana na tabia iliyoanza kujengeka nchini hususan ya utekaji, kung’oa kucha na kutoa macho kama alivyofanyiwa Mhariri Mtendaji wa New Habari, Absolom Kibanda.

“Matukio yanayoendelea nchini yanaweza kumwondolea sifa rais. Sasa tunashuhudia waandishi wanaanza kuuawa na wengine kuzuriwa ni vema akakemea vitendo hivyo visiendelee kuwepo ndani ya jamii yetu,” alisema.

Zitto alimtaka rais kuhakikisha vurugu za kidini ambazo zimeanza kuchipukia nchini zinakomeshwa kwa nguvu zote ili Watanzania waendelee kuishi kwa kupendana kama ilivyokuwa miaka iliyopita.

“Kuhusu suala la udini na vitendo vya rushwa, namuomba Rais Kikwete awe mkali kwa kuvidhibiti. Iwapo vitadhibitiwa mapema ni wazi atamaliza uongozi wake na heshima kubwa,” alisisitiza Zitto.

Habari: JAMBO LEO.
Ngoja Raia wakosee na kumpa mzee Laigwanani EL, Mtaona moto wake...Ukikohoa tuu ndani/lupango/unaozea segerea. Anakulaga mori na maamuzi yake ndio kama alivyosema magumu,haangalii madhara yatokanayo/what's next. Yangu macho.
 
Zito, siku hizi hizi umeanza kuwa na hoja Nyepesi sana, tatizo nini!
 
Ni kawaida kwa marafiki kusifiana! Usishangae naye mkuu wa kaya akamsifia Zzk siku za usoni!!
 
Tuukubali ukweli kwamba Kikwete hakuwa chaguo muafaka kwa Watanzania, bali nguvu za pesa na kufuata mkumbo ndio kuliomweka madarakani. Ni vema Watanzania tukawa na umakini wakati wa kuteua viongozi wa juu kwa kuwapima na kuhakiki uwezo wao. Angalia Wakenya walivyoendesha midahalo ya wagombea. Mhe ZZK mtazamo wako huu sio objective.
 
leo hii mpo mtandaoni na kutoa maoni sababu ya kikwete .. kikwete ni mvumilivu sana atakuja kukumbukwa atakapoondoka .. kuna nchi nyingine mitandao kama jamii forums wangeshaifunga kitambo...
kama ilivyo facebook kwa baadhi ya nchi

bravo zito! hakika weye ni mwanasiasa uliyekomaa

We kweli wa juzijuzi kwenye JF. Hivi unafikiri JF ndiyo mtandao wa kwanza Tanzania???

Kwa taarifa yako watu walianza zamani kutoa maoni yao mtandaoni hata kabla ya JK kuwa rais. Kama ni uwazi basi tunaweza kusema ulianza wakati wa Mkapa. Tulikuwa na mtandao unaitwa BCS ambao ulikuwa chini ya magazeti ya majira na Business Times.............. kwa vile Nyaurawa (RIP) alikuwa too much CCM wakashindwa kuwa kumaintain situation ndipo Jambo Forums ambayo ndiyo hii Jamii Forums ilipokuja kutake over. JF inasurvive kwa vile iko independent ................... Kwa taarifa yako CCM hawaipendi JF lakini hawana jinsi..............!!! Tumechangia BCS toka enzi za 2003!!
 
-Kwenye Sera za Mambo ya Nje hatuangalii matukio ya kutembelewa.Sera yetu ya Mambo ya Nje ambayo tenets zake ni za tangu enzi za Mwl.Nyerere zinatakiwa kufanyiwa overhaul.

Leo hii unashindwa kumtofautisha Rais na Waziri wa Mambo ya Nje.

Ikiwa unawezesha Marais 2 wa Mataifa makubwa ambayo yana ambitions za kuchota raslimali(Ambition za kibeberu) huku mikataba ikiwa ya Siri na huthubutu kuweka wazi ili watanzania wajue kama tumenufaika ama la,does it make you a vibrant leader? Huo ni udhaifu

Hatuwezi kujivunia kutembelewa na Mabeberu ikiwa hatujui na wala hatushirikishwi katika mikataba iliyosainiwa.Hapo wananchi tutakua tumemsaidia Chifu Mangungo.

2:Economic Diplomacy:Hadi sasa sera zetu za mambo ya nje zimeshindwa kwenda kasi na trend ya Dunia.Kenya wamelichukulua hili kwa umakini.Wizara imeshindwa ku-intergrate wizara ya Fedha na uchumi,viwanda na Biashara,Kilimo,Mali asili na Utalii na wizara ya Uwezeshaji.Tumekomalia uzururaji wa Rais kama nguzo kuu ya sera za Mambo ya nje.Tunatekeleza Sera ya Kuomba na Kushukuru

Membe ni msomi mzuri kwenye International Relations na ana uwezo lakini Rais hawezi kukwepa lawama za kuingilia Foreign Affairs.

Katika mamia ya Ziara za Rais nje ya nchi isije kuonekana kuwa ndiyo utekelezaji wa Sera za Mambo ya nje.Hapana!

Kukiwa na Sera imara kila jambo linaenda vizuri badala ya kutegemea kipaji cha kutembea cha Rais.Sera ni institutional Mechanism.Taasisi imara na sio watu imara wa kukata mbuga halafu wanarejea na matunda mwitu yenye sumu na kuiangamiza familia pole pole kwa miaka mingi ijayo.

Ni nini sera yetu kwa Afrika?Nini sera yetu specific kwa EU?Ni nini sera yetu kwa Middle East?Ni nini Sera Yetu kwa SADC.Ni ipi sera yetu kwa Latin America?Ni utashi na kipaji cha Rais kuweza kuweka pozi la Picha na wakuu wa nchi hizo tu?Uimara wa Rais hapa Siuoni zaidi ya kipaji chake tu cha kutembea na kuimarisha Album

Actually Rais asingekua na njia nyingine ya kuficha udhaifu wake zaidi ya kutoa uhuru wa maoni ambao ni constitutional Right.Siyo Hisani.

Haya maneno kamwambie naibu katibu mkuu wako paleee ofisini halafu kingine ben punguza hii kitu:kev:
 
Kwa mara ya kwanza labda naweza kusema naungana na Bw.Zito Kabwe kwa kiasi kikubwa, pamoja na mambo mengine yote Bw.Kikwete anapaswa sana kusifiwa kwa hilo, watu wengi wanachoshindwa kuelewa ni kwamba Raisi wa Tanzania ana nguvu sana, Raisi Kikwete anaweza kuamua sasa hivi kusiwe na Chama cha Upinzani ikawa hivyo, anaweza kuamua Bw.Tundu Lisu awekwe jela maisha na ikawa hivyo, kwa kosa tu la kuhoji muungano, au Bw.Msigwa kumuita Bw.Kinana jangili.

Bw. Slaa amesema mara nyingi sana Majukwaani kwamba Raisi ni Fisadi yeye pamoja na Familia yake, amemdhalilisha sana Raisi Kikwete, lakini ameachwa aseme anavyotaka, watu wengi wanachosahau ni kwamba Raisi Kikwete anaweza kuamua sasa hivi tu CHADEMA ifutwe na hakuna kitu mtafanya mtaishia kulalamika humu basi, anaweza kuamua tu kumshughulikia Bw.Slaa na msimsikie tena na hakuna kitu mtafanya!

Watu wengi wanasahau CHADEMA wanakuwa na kesi wanakwenda Mahakamani na mara nyingine wanashinda kama kesi za Ubunge, kitu ambacho kwa nguvu na ushawishi alionao Raisi wa Tanzania angeweza kuingilia Mahakama na kuzuia, lkn hakufanya hivyo, Bw. Slaa amesema mara nyingi kwamba Nchi haitawalika wakati kuna Raisi wa nchi hilo peke yake lingetosha hata kumpa kesi ya Uhaini lkn ameachwa!

CHADEMA wameanzisha Ukanda kinyume na Katiba ya TZ jambo ambalo wangeweza hata kushitakiwa kwa uhaini wakati wa Mlm Nyerere lkn wameachwa!

Wanaandamana wanavyotaka, kitu ambacho wakati wa mlm Nyerere wasingeweza kufanya wameachwa, kwanza katika hali ya kawaida kama Raisi angeamua kutokana na nguvu aliyokuwa nayo hata hao Wabunge kama akina Bw.Nasari au Lema wasingeshinda Uchaguzi, lkn bado Raisi Kikwete akawaambia watu waacheni tu washinde!

Hivyo pamoja na mapungufu yake naweza kusema Raisi Kikwete ni moja kati ya Maraisi ambao ni wavulimivu sana na labda hajui au hataki kutumia madaraka yake MAKUBWA sana ambayo Katiba inampa kuwashughulikia wanaombeza na kumdharau hata kumuita dhaifu, hilo peke yake nchi nyingine hata TZ yetu ni Uhaini lkn akina Bw.Mnyika bado wanatembea huru, tena siku nyingine wanaalikwa Ikulu na wnashikana mikono, hilo linawezekana Tanzania tu!

ni wachache sana wanaweza kuangalia hili kwa mapana zaidi.. Naungana na wewe mkuu.. Umesema vema naamini hao wengine wataona haya..
 
leo hii mpo mtandaoni na kutoa maoni sababu ya kikwete .. kikwete ni mvumilivu sana atakuja kukumbukwa atakapoondoka .. kuna nchi nyingine mitandao kama jamii forums wangeshaifunga kitambo...
kama ilivyo facebook kwa baadhi ya nchi

bravo zito! hakika weye ni mwanasiasa uliyekomaa

Tatizo wabongo mmezoea kupokwa haki zenu kiasi kwamba pale mtakapopewa haki hiyo mnashukuru utadhani mmepewa hisani ilhali ni haki yako. Kuzuia uhuru wa watu kutoa maoni yao na kupashana habari ni ukiukwaji wa haki za binadamu na kuuacha uhuru huo kuwepo sio hisani of which somebody can take credit...
 
Kwa mara ya kwanza labda naweza kusema naungana na Bw.Zito Kabwe kwa kiasi kikubwa, pamoja na mambo mengine yote Bw.Kikwete anapaswa sana kusifiwa kwa hilo, watu wengi wanachoshindwa kuelewa ni kwamba Raisi wa Tanzania ana nguvu sana, Raisi Kikwete anaweza kuamua sasa hivi kusiwe na Chama cha Upinzani ikawa hivyo, anaweza kuamua Bw.Tundu Lisu awekwe jela maisha na ikawa hivyo, kwa kosa tu la kuhoji muungano, au Bw.Msigwa kumuita Bw.Kinana jangili.

Bw. Slaa amesema mara nyingi sana Majukwaani kwamba Raisi ni Fisadi yeye pamoja na Familia yake, amemdhalilisha sana Raisi Kikwete, lakini ameachwa aseme anavyotaka, watu wengi wanachosahau ni kwamba Raisi Kikwete anaweza kuamua sasa hivi tu CHADEMA ifutwe na hakuna kitu mtafanya mtaishia kulalamika humu basi, anaweza kuamua tu kumshughulikia Bw.Slaa na msimsikie tena na hakuna kitu mtafanya!

Watu wengi wanasahau CHADEMA wanakuwa na kesi wanakwenda Mahakamani na mara nyingine wanashinda kama kesi za Ubunge, kitu ambacho kwa nguvu na ushawishi alionao Raisi wa Tanzania angeweza kuingilia Mahakama na kuzuia, lkn hakufanya hivyo, Bw. Slaa amesema mara nyingi kwamba Nchi haitawalika wakati kuna Raisi wa nchi hilo peke yake lingetosha hata kumpa kesi ya Uhaini lkn ameachwa!

CHADEMA wameanzisha Ukanda kinyume na Katiba ya TZ jambo ambalo wangeweza hata kushitakiwa kwa uhaini wakati wa Mlm Nyerere lkn wameachwa!

Wanaandamana wanavyotaka, kitu ambacho wakati wa mlm Nyerere wasingeweza kufanya wameachwa, kwanza katika hali ya kawaida kama Raisi angeamua kutokana na nguvu aliyokuwa nayo hata hao Wabunge kama akina Bw.Nasari au Lema wasingeshinda Uchaguzi, lkn bado Raisi Kikwete akawaambia watu waacheni tu washinde!

Hivyo pamoja na mapungufu yake naweza kusema Raisi Kikwete ni moja kati ya Maraisi ambao ni wavulimivu sana na labda hajui au hataki kutumia madaraka yake MAKUBWA sana ambayo Katiba inampa kuwashughulikia wanaombeza na kumdharau hata kumuita dhaifu, hilo peke yake nchi nyingine hata TZ yetu ni Uhaini lkn akina Bw.Mnyika bado wanatembea huru, tena siku nyingine wanaalikwa Ikulu na wnashikana mikono, hilo linawezekana Tanzania tu!

Ulisoma shule ipi wewe?? JK siyo Mungu au hujui hilo!! JK ni mwanadamu aliyeomba yeye mwenyewe urais japo kwa razima ashinde! Hayo uliyoongea napata taabu sana kukujua jinsi ulivyo! kuishi Tanzania siyo hisani ya watawala!!
 
Hivi aliyesema kwanzia leo ni marufuku CHADEMA kuisifia selekali si ndo huyu huyu au?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Walahi kanda ya magharibi tulilamba galasa. Huyu Zitto mbona mnafiki sana huyu alizaliwa wapi kwanza? Mwanasiasa gani una rangi mbili mbili kama kinyonga? Hivi hata huo Urais unaoutaka ni mwendawazimu gan atakupa mnafiki kama ww?
 
Last edited by a moderator:
Zitto sio mnafiki kama Dr Slaa, Dr Slaa ana mkubali Kikwete kiaina, akiwa na misukule yake ana mponda, akijipeleka Ikulu kunywa juice ana baki kujichekesha chekesha.
 
-Kwenye Sera za Mambo ya Nje hatuangalii matukio ya kutembelewa.Sera yetu ya Mambo ya Nje ambayo tenets zake ni za tangu enzi za Mwl.Nyerere zinatakiwa kufanyiwa overhaul.

Leo hii unashindwa kumtofautisha Rais na Waziri wa Mambo ya Nje.

Ikiwa unawezesha Marais 2 wa Mataifa makubwa ambayo yana ambitions za kuchota raslimali(Ambition za kibeberu) huku mikataba ikiwa ya Siri na huthubutu kuweka wazi ili watanzania wajue kama tumenufaika ama la,does it make you a vibrant leader? Huo ni udhaifu

Hatuwezi kujivunia kutembelewa na Mabeberu ikiwa hatujui na wala hatushirikishwi katika mikataba iliyosainiwa.Hapo wananchi tutakua tumemsaidia Chifu Mangungo.

2:Economic Diplomacy:Hadi sasa sera zetu za mambo ya nje zimeshindwa kwenda kasi na trend ya Dunia.Kenya wamelichukulua hili kwa umakini.Wizara imeshindwa ku-intergrate wizara ya Fedha na uchumi,viwanda na Biashara,Kilimo,Mali asili na Utalii na wizara ya Uwezeshaji.Tumekomalia uzururaji wa Rais kama nguzo kuu ya sera za Mambo ya nje.Tunatekeleza Sera ya Kuomba na Kushukuru

Membe ni msomi mzuri kwenye International Relations na ana uwezo lakini Rais hawezi kukwepa lawama za kuingilia Foreign Affairs.

Katika mamia ya Ziara za Rais nje ya nchi isije kuonekana kuwa ndiyo utekelezaji wa Sera za Mambo ya nje.Hapana!

Kukiwa na Sera imara kila jambo linaenda vizuri badala ya kutegemea kipaji cha kutembea cha Rais.Sera ni institutional Mechanism.Taasisi imara na sio watu imara wa kukata mbuga halafu wanarejea na matunda mwitu yenye sumu na kuiangamiza familia pole pole kwa miaka mingi ijayo.

Ni nini sera yetu kwa Afrika?Nini sera yetu specific kwa EU?Ni nini sera yetu kwa Middle East?Ni nini Sera Yetu kwa SADC.Ni ipi sera yetu kwa Latin America?Ni utashi na kipaji cha Rais kuweza kuweka pozi la Picha na wakuu wa nchi hizo tu?Uimara wa Rais hapa Siuoni zaidi ya kipaji chake tu cha kutembea na kuimarisha Album

Actually Rais asingekua na njia nyingine ya kuficha udhaifu wake zaidi ya kutoa uhuru wa maoni ambao ni constitutional Right.Siyo Hisani.

Kwa maneno machache nakubaliana na wewe. Hivi mie kutoa maoni yangu ni hisani ya rais? Au je nikisema Zitto ni dhaifu ni tusi? Jamani tuwe makini kama watu kama Zitto wanasifia mambo haya je tunao uongozi?
Ngoja nimuulize Zitto swali dogo hivi kama yeye angelikuwa Kikwete angefanyaje kwa changamoto anazokutana nazo Kikwete? Pppptuuu....
 
Back
Top Bottom