Zitto: Kikwete ni Rais wa ajabu.

[h=5]JamiiForums
[/h][h=5]Kutoka Rasimu ya Katiba Mpya Tanzania:
- Tume inapendekeza mgombea binafsi aruhusiwe!
- Tume inapendekeza Rais asiwe na umri chini ya miaka 40
- Inapendekezwa Rais aunde Serikali ndogo iliyo na Mawaziri wasiozidi 15 na mawaziri hao wasiwe wabunge!

hapo kwenye red ndo kumemkata maini zitto na kuona ndoto zake zimefifia huku akiwa ametangaza kustaafu ubunge,ameamua kujipendekeza kwa jk angalau atafutiwe kinafasi kwenye taasisi za serikali

[/h]
 
Hivi aliyesema kwanzia leo ni marufuku CHADEMA kuisifia selekali si ndo huyu huyu au?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
Pale zitto alishikwa na hasira akawa anatumia Jazba Lakini kwa kuwa waaminifu; ni kweli kwamba katika awamu Hii ya Rais Kikwete; Watanzania wamekuwa na uhuru zaidi wa kutoa maoni yao kuliko nyakat nyengne. Kwa hili yatupasa kuwa fair.
 
Hebu fafanua vizuri hekima zipi unazozizungumzia hapa au nizakuuza nchi kwa wachina kwa mastahi ya mtoto wake? Hivi wewe ukiacha ukikibaraka ulishawahi kumuelewa rais wetu.

tusiyaone mabaya tu mazuri tuyakubali. Jk kuna mambo kayafanya kiukweli ila mengine bado. La kufahamu ni kuwa, huwezi kutimiza haja ya kila mtu nchini. Kumridhisha kila mtanzania kwa itikadi yako,uchumi wake n.k haiwezekani. Udhaifu upo lakani tutaje na strength zake.
 
hii story ni ile ya scratch my orifice and i scratch yours

wenye nidhani wanasema scratch my a$$ and i scratch your a$$ too.... THE FEELING IS MUTUAL
 
pale zitto alishikwa na hasira akawa anatumia jazba lakini kwa kuwa waaminifu; ni kweli kwamba katika awamu hii ya rais kikwete; watanzania wamekuwa na uhuru zaidi wa kutoa maoni yao kuliko nyakat nyengne. Kwa hili yatupasa kuwa fair.

zitto kigeugeu alisema atawazuia wabunge wa chadema kusifia serikali ya ccm......au huyu sio zitto yule aliyesema hivyo!!!!? Tafakari!
 
-Kwenye Sera za Mambo ya Nje hatuangalii matukio ya kutembelewa.Sera yetu ya Mambo ya Nje ambayo tenets zake ni za tangu enzi za Mwl.Nyerere zinatakiwa kufanyiwa overhaul.

Leo hii unashindwa kumtofautisha Rais na Waziri wa Mambo ya Nje.

Ikiwa unawezesha Marais 2 wa Mataifa makubwa ambayo yana ambitions za kuchota raslimali(Ambition za kibeberu) huku mikataba ikiwa ya Siri na huthubutu kuweka wazi ili watanzania wajue kama tumenufaika ama la,does it make you a vibrant leader? Huo ni udhaifu

Hatuwezi kujivunia kutembelewa na Mabeberu ikiwa hatujui na wala hatushirikishwi katika mikataba iliyosainiwa.Hapo wananchi tutakua tumemsaidia Chifu Mangungo.

2:Economic Diplomacy:Hadi sasa sera zetu za mambo ya nje zimeshindwa kwenda kasi na trend ya Dunia.Kenya wamelichukulua hili kwa umakini.Wizara imeshindwa ku-intergrate wizara ya Fedha na uchumi,viwanda na Biashara,Kilimo,Mali asili na Utalii na wizara ya Uwezeshaji.Tumekomalia uzururaji wa Rais kama nguzo kuu ya sera za Mambo ya nje.Tunatekeleza Sera ya Kuomba na Kushukuru

Membe ni msomi mzuri kwenye International Relations na ana uwezo lakini Rais hawezi kukwepa lawama za kuingilia Foreign Affairs.

Katika mamia ya Ziara za Rais nje ya nchi isije kuonekana kuwa ndiyo utekelezaji wa Sera za Mambo ya nje.Hapana!

Kukiwa na Sera imara kila jambo linaenda vizuri badala ya kutegemea kipaji cha kutembea cha Rais.Sera ni institutional Mechanism.Taasisi imara na sio watu imara wa kukata mbuga halafu wanarejea na matunda mwitu yenye sumu na kuiangamiza familia pole pole kwa miaka mingi ijayo.

Ni nini sera yetu kwa Afrika?Nini sera yetu specific kwa EU?Ni nini sera yetu kwa Middle East?Ni nini Sera Yetu kwa SADC.Ni ipi sera yetu kwa Latin America?Ni utashi na kipaji cha Rais kuweza kuweka pozi la Picha na wakuu wa nchi hizo tu?Uimara wa Rais hapa Siuoni zaidi ya kipaji chake tu cha kutembea na kuimarisha Album

Actually Rais asingekua na njia nyingine ya kuficha udhaifu wake zaidi ya kutoa uhuru wa maoni ambao ni constitutional Right.Siyo Hisani.


Nakubaliana na wewe kwa 100%.
 
Nakubaliana na wewe kwa 100%.

tungeshangaa kama ungempinga huyo mwenzako nyie wote akili yenu si moja,halafu aweda pole ulikuwa unahangaika kuandaa mazingira ya kugombea ubunge naona rasimu ya katiba imekutanzi pole mkuu,endelea kuitumikia plan tu.
 
Huyu zzk ni kama vile ana kichwa cha mende,maana anaweza leo akaja na mambo ya kumtuhumu JAKAYA, Kesho akaja na mambo ya kukanusha alichokisema.Ila contradiction zote hizo huwa anazifanya bila ya yeye kujua kuwa nini anachokifanya.Huyu huyu zzk kichwa chake tayari kimefuta kumbukumbu ya maovu ya sirikali ya huyu baba mkwe wake inayoyafanya kwa wananchi?.Kwa uelewa wa bwana ZZK yeye anajua vurugu ni mpaka zifikie kiwango gani ndo aite kuwa hayo ni MACHAFUKO?,Mtwara,Mbeya,Mwanza,Arusha,Iringa Zanzibar na Geita machafuko yote yaliyotokea sehemu hizo yeye anaona hiyo ndo Amani?.Issue hapa cyo kwamba JAKAYA ni mvumilivu ila sisi wananchi ndo ni WAVUM
ILIVU.

Zitto anaongea nini?
 
Zitto ana Stress...ndoto zake za U Rais 2015 zimeoteshwa Mbawa na Judge Warioba na Tume yake
 
Kwamba Rais hachukii akitukanwa, ni sawa kabisa na hatakiwi kuchukia kwa kuwa hatukanwi bali anachoambiwa ni kwamba serikali yake na taasisi ya urais iliyo mikononi mwake imekuwa dhaifu! Huo ni ukweli ulio wazi, sasa achukie ili iweje na hata akichukia ni kwamba ameonesha kutokuwa na uwezo wa kuchukua hatua, atafanya nini?! Mambo mangapi yametokea nchi hii na kufanywa na watendaji walio wateule wake lakini haoneshi kushtuka na yuko happy tuu....., sasa kama si rais wa ajabu ni nini! Mamlaka tuliyompa katika awamu ya kwanza na mamlaka aliyopewa na Lipumba katika awamu ya pili hatuoni alichofanya kuonesha kwamba nchi ina rais madhubuti! Lipumba mwenyewe amekiri wazi kwamba jitihada alizofanya kuwaingiza mkenge waliomwamini hazioneshi kuzaa matunda aliyotarajia, na bado hakuna hata tamko kutoka ikulu juu ya madai haya ya Lipumba, bado kweli usiseme rais JK si mtu wa ajabu....
 
leo hii mpo mtandaoni na kutoa maoni sababu ya kikwete .. kikwete ni mvumilivu sana atakuja kukumbukwa atakapoondoka .. kuna nchi nyingine mitandao kama jamii forums wangeshaifunga kitambo...
kama ilivyo facebook kwa baadhi ya nchi

bravo zito! hakika weye ni mwanasiasa uliyekomaa
kwahiyo jk ndio ametupa mamlaka ya kutumia mtandao?? mzee hii inaitwa www na serikali ya tz haina machinery ya kufunga mtandao hawana hata uwezo wa kuwapa raia wao maji ya kunywa safi na salama unazungumzia suala kufunga mtandao?? jk has nothig to do with our right to use online technology.
 
Political tolerance --- sio udhaifu ndg.... Hongera Zitto kwa kuliweka hili vizuri.
True mkuu tumeona political tolerance kwenye EPA, Rada, David Jairo, Luhanjo, Dr Ulimboka, Mwangosi, Kibanda, Richmond na DOWANS - kamtolerate Rostam mpaka anatudai mabilioni sasa, Kinana na pembe za ndovu, Katolerate ndege ya QATAR na waarabu kubeba Twiga wetu, kamtolorate Kamuhanda na sasa kamzawadia cheo. Kweli JK ni rais wa ajabu. tutamkumbuka kweli tutakapompata Rais ambaye hatatolerate haya.
 
Back
Top Bottom