Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Kiongozi mstaafu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, ametoa onyo kali kwa maafisa wa polisi na watendaji wengine wa serikali wanaoshiriki katika kile alichokiita uingizaji wa kura bandia kwenye uchaguzi, akisema chama hicho hakitasita kuchukua hatua hata kama mhusika ni askari wa vyombo vya ulinzi na usalama.
Akihutubia iku ya Alhamisi Julai 10, 2025 katika Jimbo la Tunduru Kaskazini, wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma katika mwendelezo wa Operesheni Majimaji ya chama hicho, Zitto ameeleza kuwa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024, ACT Wazalendo ilimkamata afisa wa polisi akiwa amepakia kura bandia kwa lengo la kuzisambaza kwenye kituo cha kupigia kura.
"Tunajua CCM wanatumia kura bandia, kura bandia zinapigwa halafu zinaletwa kwenye kituo cha kupigia kura. Isivyo bahati, kule Kigoma tulimkamata Afisa wa Polisi akiwa amepakia kura bandia. Afisa yule alichokipata sidhani kama atarudia jambo lile," amesema Zitto.
Katika kauli hiyo, Zitto amesema chama hicho hakitavumilia tena majaribio yoyote ya kuvuruga uchaguzi kwa mbinu chafu kama hizo.
"Ninataka nitangaze rasmi hapa, na maafisa wa polisi watusikie: hatutajali magwanda yao, hatutajali nyota zao, hatutajali mitutu yao. Polisi atakayebeba kura bandia ni halali yetu," ameongeza kwa msisitizo.
Suala la maafisa wa usalama kuhusishwa na uingizaji wa kura bandia ni mojawapo ya hoja kubwa zilizowasilishwa na ACT Wazalendo katika mashauri kadhaa waliyoyafungua kupinga matokeo ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024, hasa katika baadhi ya maeneo ya Kigoma.
Zitto amesisitiza kuwa Operesheni Majimaji inalenga kulinda demokrasia na kuhakikisha kuwa uchaguzi wa mwaka 2025 unakuwa huru na wa haki.
Akihutubia iku ya Alhamisi Julai 10, 2025 katika Jimbo la Tunduru Kaskazini, wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma katika mwendelezo wa Operesheni Majimaji ya chama hicho, Zitto ameeleza kuwa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024, ACT Wazalendo ilimkamata afisa wa polisi akiwa amepakia kura bandia kwa lengo la kuzisambaza kwenye kituo cha kupigia kura.
"Tunajua CCM wanatumia kura bandia, kura bandia zinapigwa halafu zinaletwa kwenye kituo cha kupigia kura. Isivyo bahati, kule Kigoma tulimkamata Afisa wa Polisi akiwa amepakia kura bandia. Afisa yule alichokipata sidhani kama atarudia jambo lile," amesema Zitto.
Katika kauli hiyo, Zitto amesema chama hicho hakitavumilia tena majaribio yoyote ya kuvuruga uchaguzi kwa mbinu chafu kama hizo.
"Ninataka nitangaze rasmi hapa, na maafisa wa polisi watusikie: hatutajali magwanda yao, hatutajali nyota zao, hatutajali mitutu yao. Polisi atakayebeba kura bandia ni halali yetu," ameongeza kwa msisitizo.
Suala la maafisa wa usalama kuhusishwa na uingizaji wa kura bandia ni mojawapo ya hoja kubwa zilizowasilishwa na ACT Wazalendo katika mashauri kadhaa waliyoyafungua kupinga matokeo ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024, hasa katika baadhi ya maeneo ya Kigoma.
Zitto amesisitiza kuwa Operesheni Majimaji inalenga kulinda demokrasia na kuhakikisha kuwa uchaguzi wa mwaka 2025 unakuwa huru na wa haki.