Mkuu
jmushi1, hii picha nasikia tetesi imeamuliwa itumike katika kikao maalum katika harakati za kuisambaratisha Chadema na jeshi maalum limeundwa kutekeleza kazi hiyo. Ukienda Michuzi blogs hii picha ndiyo hiyo imetumika hata huko ikiambatana na Zitto kutangaza nia yake ya kugombea Uraisi 2015.
Kwangu mimi hiyo nia yake sina tatizo nalo, ni haki yake kikatiba ndani ya nchi ingawa siku haki yake kikanuni ndani ya chama, kila chama kina kanuni zake. Tatizo ni lengo la huu mpango unaosimamiwa na mahasimu wanaojulikana ndani na nje ya chama, kuwagawa wanachama wa Chadema.
Ukweli ni kwamba picha za aina hii zimetayarishwa na ziko nyingi na zote zilipigwa kwenye matukio tofauti lakini ya kweli tangu mwaka 2010 hadi 2012. Ajabu ni kwamba zilizochaguliwa ni zile tu zinazomwonesha Zitto, lengo likiwa ni kujenga taswira kwamba Chadema bila Zitto si lolote si chochote.
Mimi binafsi ninavyoamini, Chadema imevuka inayoitwa "threshhold" ya kuweza kusambaratishwa kwa mbinu za kipuuzi kama hizi. Hebu waangalie wote wanaotokwa mapovu kumtetea Zitto humu ndani, ni wale wale na bado wataongezeka. Wanachosahau ni kuwa Chadema ni zaidi ya Mbowe, Zitto na Dr. Slaa.
Dai la ukabila lilishindwa, dai la ukanda lilishindwa, dai la udini lilishindwa na sasa turufu iliyobaki ni hiyo moja...fitina na uchonganishi. Nashindwa kuamini mtu kama Zitto kukubali kutumika kwa namna hii...wenzio wahangaike juani kuitangaza na kuijenga chama, wewe unakesha kivulini kusubiri mavuno! La hapana, si Zitto!