Zitto Kabwe: Nani anaongoza nchi yetu?

Zitto Kabwe: Nani anaongoza nchi yetu?

So contradictory!

Zitto unasema Viongozi wa juu wako kimya, wakati huo huo unasem PM ametoa kauli, pia VP ametoa kauli. Sasa hapo issue ni ukimya wa viongozi, au huwaamini?

Pia unataka serikali itoe maelezo. Nani tena atoe maelezo ikiwa Mkuu wa shughuli za serikali ameshatoa kauli?

Usizunguke mbuyu, issue uitakayo ni rais kujitokeza hadharani.
Amesema wametoa kauli zenye kukanganya zaidi kuliko kuondoa taharuki. Rejea kauli ya VP akiwa Tanga ndio ilizidi kuleta minong'ono kuliko kutuliza.
 
Huyu naye, eti rais anaumwa, uumwe mwenyewe! Mungu aendelee kumlinda rais wetu mpendwa Mh Dr JPM huko alipo! Na ninyi jichanganyeni tu muone atakapowatokea gwafla na kubwabwaja kwenu!
Hivyi vipengele vya katiba wote tunavijua, lakini hawina kazi kwa sasa maana rais wetu yupo salama na buheri wa afya!
".....huko alipo" ina maana hajulikani alipo sio? Mkuu mbona wananchi tumezoea siku zote kujua kama mhe. Rais yupo Dodoma ama Dar ama Chato lakini safari haijulkani ndo maana unaona kelele zimeibuka.
 
Unaweza ukawa rahisi mengine makubwa usiyaone ndomana ilifikiwa hapo ,kwani ccm inaweza ikawa na washauri woga wasikwambie ukweli,upande wapili ukakusaidia.mfano corona IPO unasema haipo mwisho wasiku inakukamata na kukufundisha mwenyewe
Waziri wa Afya wa Znz ni ACT umeona amekiri kuwa kuna corona?
 
Naheshimu mtazamo na maoni yako hata kama sikubaliani nayo. Kamwe sitakuita "hamna kitu"
Jamaa wa DW wanakuitaga mchambuzi kumbe hamna kitu kabisa watu wanamuulizia Rais sio Magufuli urais ni zaidi ya Magufuli...hata kama watu hatukumchagua nec ambao ndio wenye mamlaka kwa Katiba hii mbovu ndio wamemtangaza kuwa Rais so ana dhamana ya Nchi sio kikundi cha wajinga wanaodhani urais ni hatimiliki ya Magufuli ni ujinga! hakuna mtu anaeweza kufanya kazi ya Rais bila kupewa mamlaka kisheria Samia hawezi kufanya maamuzi yoyote ya urais japo yeye ni makamu so muwe mnaondoa utando wa ujinga kwa vitu vidogo hivi...Nchi ikiporwa au kuvamiwa Rais ndio atawajibika so wanaotaka kujua Rais yuko wapi ni kwa maslahi mapana ya Nchi kama afya imekuwa mbovu wasaidizi wapewe mamlaka kisheria yakufanya kazi ya Rais jielimisheni

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Mimi binafsi naona mtoa mada hajaridhika na majibu ya Makamu wa Rais and Waziri Mkuu. Atulie mambo yapo salama na Rais popote alipo bana yupo in control of the state otherwise hizo hatua anazozisema zingekuwa zimechukuliwa. Uongozi wa juu wa nchi wanazijua vifungu hivyo vya katiba vyema tu. Tuondoe hofu upo mikononi vya viongozi makini.
 
Umetoa ushauri wenye busara na uungwana. Hayo ndiyo maoni yanayojenga na kuheshimu mitazamo na maoni ya wengine
Mimi binafsi naona mtoa mada hajaridhika na majibu ya Makamu wa Rais and Waziri Mkuu. Atulie mambo yapo salama na Rais popote alipo bana yupo in control of the state otherwise hizo hatua anazozisema zingekuwa zimechukuliwa. Uongozi wa juu wa nchi wanazijua vifungu hivyo vya katiba vyema tu. Tuondoe hofu upo mikononi vya viongozi makini.
 
Zitto bhana! Uambiwe na nani sasa hali ya Rais?

Waziri mkuu kasema yuko fiti
Makamu Rais kasema rais yuko fiti

Unataka uambiwe na nani sasa?

Huu upumbavu kumbe hadi kwa wasomi upo?
Sidhani kama unajua ulichoandika!
Ungemsoma Zitto kisha ujipe muda wa kulitafakari andiko lake kabla ya kukurupuka
 
Bungeni tuko bize kupitisha mjadala wa kilimo cha "Bange"... soko la uhakika lipo na tunayo ardhi njema....Amiri jeshi yuko salama....suala la muda tuu....sawa mheshimiwa ZZK
 
Zitto bhana! Uambiwe na nani sasa hali ya Rais?

Waziri mkuu kasema yuko fiti
Makamu Rais kasema rais yuko fiti

Unataka uambiwe na nani sasa?

Huu upumbavu kumbe hadi kwa wasomi upo?
No hata kama Waziri Mkuu kasema na Waziri Mkuu kwamba Rais yuko salama lakini mazingira yanaonyesha kwamba lipo jambo ambalo halipo sawa mkuu. No we need clarification, hili liko wazi.
 
Mimi nafikiri wanajaribu kuvuta muda tu kuitekeleza hyo ibara ya 37(3) ili hata kama anaumwa aweze pata nafuu, halafu katika hiyo ibara haijasema ktk kipindi ani akiumwa aweza kupewa mtu mwingine madaraka sasa ni wiki ya pili au tatu hajaonekana labda tusubiri zaidi atatokea
 
Au tumpatie Zitto Kabwe kwa wiki moja tu urais, sipati picha atakavyopiga dili za madini
 
Transition inatakiwa iweje, kuna hafla inatakiwa ifanyike kuna viapo vipya? Inawezekana anayehusika kesh dhika usukani.Tuzikibali kauli za viongozi waliopo kila kitu ni shwarina tuendelee na yetu
 
Naww unaamini huu ujinga kwamba Polis wanalinda Raia na mali zao

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Sio ujinga mkuu ndio kazi yao na wanaifanya kikamilifu, pata picha wasingekuwepo sisi tungekuwa katika hali gani na mali zetu.
Hayo mambo mengine ya 'kupigana virungu' naona ni politics tu
Mkuu ebu nisaidie hili tafadhali, kwa mfano ikiwa raisi yupo kwenye coma, IGP na CDF watapokea order kutoka kwa nani?
 
Back
Top Bottom