Hizi story zenu za ajabu kweli....
Kama unachokifikiri ni sahihi, kwamba, Zito kamteka huyo bwana na kisha kuanza kufanya unachokisema "kuichafua serikali!!????"......Huyo Zito yuko Somalia kwani? Si yuko nchini na leo alikuwa kajaa tele ofisini kwake akitoa tamko? Mnamwogopa??
By the way, si huyo mkurugenzi wa usalama wa taifa angeshamtaarifu IGP mara moja kumtia nguvuni Zito saa na siku ileile aliyofika ofisini kwake?
Matendo ya kuteka na kutekwa watu yamezidi sana chini ya utawala huu, yet serikali na vyombo vya usalama havifanyi lolote kukomesha matendo haya, shida iko wapi?
Watu ku - insinuate kuwa usalama wa taifa waliovalishwa magwanda ya kijani ya CCM ndiyo wahusika wa upuuzi huu, nani atabisha?
Na hivi mnaposema Zitto kafanya hili "ili kuichafua serikali" mnakuwa na maana gani? Na ni serikali gani iyo inayochafuliwa? Hii hii chini ya Bwana Pombe na CCM ya Magufuli?
Aisee, wewe lazima utakuwa na matatizo upstairs na umeamua kwa makusudi kabisaaaa kututania wanajukwaa, siyo bure!!
Hivi inawezekana vipi serikali inayojiharishia na kujipaka kinyesi yenyewe kwa matendo yake maovu na ya hovyo kama kutenda mambo kinyume cha katiba na sharia, yet ichafuliwe na mtu mwingine tena???
Please,give us a break!!.
Pelekeni upuuzi wenu huu hukohuko kwenye corridor za Lumumba!!