Zitto Kabwe More Than Meets the Eye!

Zitto Kabwe More Than Meets the Eye!

ha ha., sasa hapo ukipata nafasi ya kuzungumza na zitto muulize atakuelezea., lakini ndivyo alivyo andika kwenye thread yake ile.. ila nadhani point ya msingi pale ni kwamba aliomba radhi tena mara mbili kwa makosa aliyo mfanyia marehemu.

Nadhani alikuwa anauhabarisha umma kuwa humo ndani sabotage ni mchezo wa kila siku na yeye kajifunzia humo! !!!!!

Only that them masters are good in that than him!!!!!
 
Kama mjadala umefungwa, mbona viongozi wanaendelea kutoa matamko na wanasambaza ripoti ya siri juunya zitto kabwe

Ndio tuungane kuhoji!!!!

May be aliyetumwa kuwasha moto katumia kuni kubwa sasa mapishi yameiva na moto unakolea as wind keeps blowing
 
DISCLAIMER
Beware the phrases you are about to read below are very sweet to read but deadly to believe. It is a spinning document written by the masters of deceptions branded as Character X. - Mandela.

ha ha ha., i still laugh each time i go through this!., - "Mandela"
 
Mbowe analijua hilo la uwezo mkubwa wa Zitto na linamtia woga sana, maana nyota ya Zitto inaongezeka kung'ara wakati ya kwake inaonekana imeshachokwa. Tatizo ni kuwa, kwa Mbowe, CHADEMA ni sawa na Bilcanas, yaani ni mali ya familia na hayuko tayari kuiachia mtu mwingine nje ya familia aiongoze.
Kubwajinga
Nakubaliana na uwezo wa ZZK, lkn mbona tuna wasomi wengi kama yeye na bado nchi yetu inastruggle tu. How do you measure umaarufu na uwezo wa zitto machoni mwa watz wa kawaida na ukaeleweka? Kama ZZK ni mbunge pekee wa CDM mkoani Kigoma alikozaliwa hutasemaje huyu mtu ni maarufu. ZZK anajitengeneza yeye kama yeye na sio zaidi ya hapo. Kwa watu wanaelewa na wanaofuatilia mambo ya kisiasa hapa nchini hatuna anayemuonea huruma ZZK kwa mambo yaliyotokea.
 
Last edited by a moderator:
Wewe unachotaka nikutuumiza vichwa kuwaza ujinga wa Zitto amaonewa hajaonewa atajua mwenyewe na waliomtuma kikubwa ni kwamba atupishe njia,kama itatokea tukakwama tutamtafuta kwani anakufa akifukuzwa Chadema?
Zitto out!
 
Wewe unachotaka nikutuumiza vichwa kuwaza ujinga wa Zitto amaonewa hajaonewa atajua mwenyewe na waliomtuma kikubwa ni kwamba atupishe njia,kama itatokea tukakwama tutamtafuta kwani anakufa akifukuzwa Chadema?
Zitto out!

Nirahisi kusema hayo ukiwa kama mwanachama wa kawaida lakini ungejiweka katika nafasi ya uongozi ndipo ungegundua maamuzi kama haya simarahisi sana kama unavyodhani., hiki nikipindi kigumu kwa Zitto kabwe lakini nataka kukuhakikishia nikigumu zaidi kwa Mh. Mbowe!! Kuliko unavyodhani
 
Ndugu yangu niliiona hiyo pia kipindi flani kilichopita., Mwingulu akaulizwa na akasema ni uzushi mtupu, lakini haiondoi uwezekano wa hayo kuwa kweli, chombo kilicho na nguvu ya kusema ukweli halisi hasa inapokuja kwenye maswala ya kimawasiliano ya namna hii ni mamlaka ya mawasiliano, na hao ndio wenye taarifa hizi kwa uasilia wake, lakini wamekaa kimya,. na kama CHADEMA tunadhani tunahujumiwa mimi nadhani tulitakiwa kubisha hodi huko nakupata maelezo sahihi na ukweli wa habari hizi kitu ambacho sijui kama kimefanyika.
lakini kabla Mamlaka hiyo haija sema wazi nini ukweli wa taarifa hizi basi bado si authority sahihi kujengea hoja wala kufanyia maamuzi.
nimtazamo wangu.

Kianchosumbua nchi hii ni ushahidi. Unafikiri Mwigulu anaweza kusema kuwa ni kweli?? hiyo mamlaka ya mawasiliano iko huru kiasi gani gani hadi ithibitishe hayo?? Siasa chafu tu ndio naziona hapo.
 
Unacho kisema watu wenye muda wa kufiki na si kufikiri tu wanaofikiri sawasawa wanakuelewa, Tatizo tulilonalo hatupendi kufikiri na kufanyia jambo utafiti wa kina tumekuwa watu wakushabikia kila jambo bila kujua tunacho shabikia ni kwa masilahi ya nani mimi ninavyomwangalia zitto naona kama ni mtu mzalendo mwenye kupenda taifa lake na hii imeonekana wazi akitetea maslahi ya taifa hili hata kuliko wanaojitokeza na kumpinga.

Ndugu zangu siasa si uadui na yeyote anaedhani siasa ni uadui hajui siasa sisi sote ni watanzania na tutaendelea kuwa sote watanzania, hivyo ukaribu wa mtu na mtu usije ukabatizwa kuwa dhambi kama itikadi zao zinatofautiana kwani wote ni watanzania mtu kuwa GAMBA na mwingine kuwa GWANDA kusituzuie kukaa meza moja kwani si uadui na isitoshe siasa tunashindana kwa hoja si kwa upanga lkn leo naona tunakoelekea ni kubaya ni kuwagawa watanzania kwa vyama vyao sasa ni kwa faida ya nani? na nina ya sema haya kwa sababu kosa kubwa la zitto ni kuwa karibu na MAGAMBA haya mengine yamebebwa ndani ya hili maana kashfa kubwa ni anatumiwa na MAGAMBA lkn inawezekana kabisa wapo wanaotumiwa na MAGAMBA na hatuwaoni na kitakacho kuanbia wanatumiwa ni matendo yao kuwa mwisho wasiku hayana faida kwa taifa chama wala wanachama wenyewe sasa ni kwa faida ya nani?

Kama nilivyoanza kusema wanaofikiri sawasawa wataelewa tu kuwa zitto hatakiwi kwasababu anaonekana kuwa mzalendo sana, mwanademokrasia sana kwani kila uongozi au nafasi inayojitokeza ndani ya chama anataka kugombea alianza kutaka nafasi ya Mwenyekiti tunaona akaitwa mpaka na wazee, Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni akaitwa kiherehere, amesikika anataka urais maneno kibao mimi na dhani balaa zitto unalitafuta mwenyewe hizi nafasi zina wenyewe na pia usije na hoja zenye nguvu zinazokufanya uonekane uko juu sana utashushwa bila kupitia kwenye ngazi ulizo pandia kaka lakini usikate tamaa kama unachokifanya una amini ni kwa maslahi ya watanzania basi amini mungu yuko na wewe na hata wale wanaokupinga leo siku watakapo kuja kufahamu ukweli watakuwa nyuma yako.
 
Unacho kisema watu wenye muda wa kufiki na si kufikiri tu wanaofikiri sawasawa wanakuelewa, Tatizo tulilonalo hatupendi kufikiri na kufanyia jambo utafiti wa kina tumekuwa watu wakushabikia kila jambo bila kujua tunacho shabikia ni kwa masilahi ya nani mimi ninavyomwangalia zitto naona kama ni mtu mzalendo mwenye kupenda taifa lake na hii imeonekana wazi akitetea maslahi ya taifa hili hata kuliko wanaojitokeza na kumpinga.

Ndugu zangu siasa si uadui na yeyote anaedhani siasa ni uadui hajui siasa sisi sote ni watanzania na tutaendelea kuwa sote watanzania, hivyo ukaribu wa mtu na mtu usije ukabatizwa kuwa dhambi kama itikadi zao zinatofautiana kwani wote ni watanzania mtu kuwa GAMBA na mwingine kuwa GWANDA kusituzuie kukaa meza moja kwani si uadui na isitoshe siasa tunashindana kwa hoja si kwa upanga lkn leo naona tunakoelekea ni kubaya ni kuwagawa watanzania kwa vyama vyao sasa ni kwa faida ya nani? na nina ya sema haya kwa sababu kosa kubwa la zitto ni kuwa karibu na MAGAMBA haya mengine yamebebwa ndani ya hili maana kashfa kubwa ni anatumiwa na MAGAMBA lkn inawezekana kabisa wapo wanaotumiwa na MAGAMBA na hatuwaoni na kitakacho kuanbia wanatumiwa ni matendo yao kuwa mwisho wasiku hayana faida kwa taifa chama wala wanachama wenyewe sasa ni kwa faida ya nani?

Kama nilivyoanza kusema wanaofikiri sawasawa wataelewa tu kuwa zitto hatakiwi kwasababu anaonekana kuwa mzalendo sana, mwanademokrasia sana kwani kila uongozi au nafasi inayojitokeza ndani ya chama anataka kugombea alianza kutaka nafasi ya Mwenyekiti tunaona akaitwa mpaka na wazee, Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni akaitwa kiherehere, amesikika anataka urais maneno kibao mimi na dhani balaa zitto unalitafuta mwenyewe hizi nafasi zina wenyewe na pia usije na hoja zenye nguvu zinazokufanya uonekane uko juu sana utashushwa bila kupitia kwenye ngazi ulizo pandia kaka lakini usikate tamaa kama unachokifanya una amini ni kwa maslahi ya watanzania basi amini mungu yuko na wewe na hata wale wanaokupinga leo siku watakapo kuja kufahamu ukweli watakuwa nyuma yako.
 
Hapa ndio huwa siwaamini sasa na.kuwaona kama.wanafiki nyie hao hao mnamuita muhaini na msaliti halafu moto umekolea sasa tunataka kujua A to Z mnaanza ngonjera za kukata mjadala sababu mnazuia kumdhalilisha zaidi eti...double standard you!!!!!

Kama ni msaliti beyond reasonable doubts na ni muhaini why the hell do you care sparing him????!!!!!Huu ni unafiki wa hali ya juu sana na nyie ndio wasaliti wa Taifa sababu mnamtoa kwenye chama sababu hamumuamini lakini mnataka umma umuamini na kumuheshimu!!!!!! How do you draw this thin line????!!!!

You can not be this smart not to be caught of guard;come.out clean or shut the gob up and we close the session you dudes spin this shet for long now,this Nation deserve some respects despite the fact that you now run the sphere but never undermine peoples capacity to think and straighten facts!!!!!
Wastaarabu wanajua hilo..si kila kimkutacho adui utapenda kitangazwe hadharani..
 
Kwa mtazamo wangu ZZK is no longer a truly revolutionary and focused politician to depend on. Mimi ni mtz nayefanya kazi ktk shirika kubwa hapa nchini. Kwa maoni ya wafanyakazi wenzangu wengi ZZK hana tena ushawishi kama zamani kutoka na mtazamo wa watu mbalimbali. Kwa ufupi ZZK haelewi kwa maana hiyo ana madhara/impact kidogo sana hata akifukuzwa uanachama. Ila Ushauri wangu kwa CDM ni kuwa ZZK apewe onyo kali na aendelee kama mwanachama wa kawaida kwa sababu he is no longer entrusted member kupewa majukumu ya uongozi ndani ya CDM. To me anamuona ZZK kama mtz mwingine mbali na sifa nyingi anazopewa na magazeti. Maana kwa tz kuwa maarufu huitaji kufanya jambo kubwa sanaaaa ila ni pale utakapoweza kucheza na vyombo vya habari. That is it.

Yeah well, sijui huo mtazamo wa wafanyakazi wenzako uko valid kiasi gani lakini hasa hapa nataka tu fanye analysis si ya gharama ya kumtoa zitto chadema ila analysis juu ya uhalali wa kumtoa zitto,
kwa mtazamo wangu sijali zitto ataondoka na watu wengi kiasi gani hata wakiondoka Kigoma yote!! I don't care LAKINI je ni HAKI!?
Uamuzi wakumuondoa utakuwa umefanyika juu ya information sahihi na za uhakika na kujiridhisha beyond reasonable doubt kwamba zitto amesaliti?? Kwasababu langu mimi hapa ni kutaka kuona tu kwamba maamuzi yafanyike not on mere hear say! Au juu ya fununu fununu ambazo hazija thibitishwa na upande wowote, Chadema wanasema hawaujui waraka huo wa siri, wala hawaja mtuma mtu kufanya iyo kazi, wakati huo huo zitto anasema yote yaliyo andikwa humo ni uwongo mtupu, sasa kutumia hayo hayo kusema zitto msaliti, anatumiwa na ccm sijui kqfanyaje,. Afu tunamfukuza nasema hatutakuwa tumetenda haki., langu mimi ni hilo tu! Lakini kukionyeshwa uthibitisho na pakawa na hakika nikweli uchunguzi huru umefanyika na huyu bwana kapatikana na hatia hii hapa na vielelezo hivi hapa na beyond reasonable doubt akawa implicated kwa usaliti, mimi nasema afukuzwe uwanachama and I don't care who goes with him!! Sijali., waende wote! Ila yafanyike hayo kwa haki.
 
Wastaarabu wanajua hilo..si kila kimkutacho adui utapenda kitangazwe hadharani..

Na ustaarabu ni kumstiri mtu na kukaa kimya kama hakijatokea kitu sio kumstiri halafu unaweka mabango!!!!!!! Hypocricy kaka mkubwa!!!!!

Mnacho mnakifanya gizani,otherwise cast the light
 
Zito hajawahi kukatazwa kutoa maoni yake popote; yeye alikuwa na fursa ya kuingia kwenye vikao vyoote vya chama chake, Kama anauwezo wa kusema na kutoa hoja zake bungeni nani alimkataza asizitoe Chamani na kwenye vikao halali kosa lake ni Intention yake sio kuboresha ni kupindua; je angejaribu mapinduzi halafu yasifanikiwe angefanya nini, huoni angepasua chama hana akili, afukuzwe.
 
Character X
The issue here sio mtazamo wa wafanyakazi wenzangu huko valid kiasi gani. Huu ndio ukweli kwa watz wasiokuwa wanachama halisi. Vyama vinatakiwa kuwekeza ktk wapenda mageuzi kuliko watu wanaojifanya kuvaa magwanda kumbe ni nyoka. Unachotakiwa kutambua ni kwamba watz wengi hasa wasomi/wafanyakazi serikalini na kwenye private sectors hatuko active kwenye siasa za kila siku lkn we are watching the tanzanian political games very close. Unachotakiwa kujua ni kwamba wanachama wenye kadi za vyama vyote hivi yaani ccm, cdm, cuf, nccr na nk. ni asilimia ndogo sana ukicompare na idadi ya watz wasiokuwa na kadi za vyama more than 45 milion. For your information ccm, yenye more than 50 years ktk game tangu kuanzishwa kwake tangu enzi za TANU haina zaidi ya wanachama zaidi hata million sita. Hii inamaana kuwa usiogope hizo kelele zinazotokea sijui lindi m/kiti kajiuzuru, sijui arusha, sijui singida!!! Upinzani imara ulisababishwa na cdm kwa ccm ni jambo muhimu kwa maendeleo ya taifa letu bila kuwa na magomvi yoyote.

Kuhusu, tuhuma za ZZK kama ni kweli au la, hii sio kazi yetu. CDM ni taasisi huru inayojiendesha kwa utaratibu na sheria waliojiwekea. Sio haki hata kidogo mimi mwananchi asiye na kadi ya cdm kuquestion maamuzi halali ya chama. Hii ni fujo. Wangapi ktk vyama wamefutiwa hadi uanachama na hakuna kelele. Umesahau ya Mhe. Mansour wa zanzibar kwa kutoa mawazo tu ya kutaka serikali tatu ktk mchakato halali wa katiba mpya. Kwa maoni yangu ZZK na wenzake walistahili adhabu kali sana ili kuleta nidhamu ndani ya vyama.
 
Character X
The issue here sio mtazamo wa wafanyakazi wenzangu huko valid kiasi gani. Huu ndio ukweli kwa watz wasiokuwa wanachama halisi. Vyama vinatakiwa kuwekeza ktk wapenda mageuzi kuliko watu wanaojifanya kuvaa magwanda kumbe ni nyoka. Unachotakiwa kutambua ni kwamba watz wengi hasa wasomi/wafanyakazi serikalini na kwenye private sectors hatuko active kwenye siasa za kila siku lkn we are watching the tanzanian political games very close. Unachotakiwa kujua ni kwamba wanachama wenye kadi za vyama vyote hivi yaani ccm, cdm, cuf, nccr na nk. ni asilimia ndogo sana ukicompare na idadi ya watz wasiokuwa na kadi za vyama more than 45 milion. For your information ccm, yenye more than 50 years ktk game tangu kuanzishwa kwake tangu enzi za TANU haina zaidi ya wanachama zaidi hata million sita. Hii inamaana kuwa usiogope hizo kelele zinazotokea sijui lindi m/kiti kajiuzuru, sijui arusha, sijui singida!!! Upinzani imara ulisababishwa na cdm kwa ccm ni jambo muhimu kwa maendeleo ya taifa letu bila kuwa na magomvi yoyote.

Kuhusu, tuhuma za ZZK kama ni kweli au la, hii sio kazi yetu. CDM ni taasisi huru inayojiendesha kwa utaratibu na sheria waliojiwekea. Sio haki hata kidogo mimi mwananchi asiye na kadi ya cdm kuquestion maamuzi halali ya chama. Hii ni fujo. Wangapi ktk vyama wamefutiwa hadi uanachama na hakuna kelele. Umesahau ya Mhe. Mansour wa zanzibar kwa kutoa mawazo tu ya kutaka serikali tatu ktk mchakato halali wa katiba mpya. Kwa maoni yangu ZZK na wenzake walistahili adhabu kali sana ili kuleta nidhamu ndani ya vyama.

ok.
Sina tatizo na mtazamo Wako,kama unadhani Zitto anastahili adhabu kali mimi pia nadhani hivyo hivyo,. ila ninasisitiza,. Maamuzi yoyote juu ya hili lazima ya fikiwe na kujengwa juu ya taarifa zenye uthibitisho thabiti!! Sio maneno ya mtaani matupu ya kuskia skia!!
halafu kama wewe huna kadi ya chama na hivyo unadhani huna haki ya kuhoji maamuzi yoyote ya chama basi angalau jua Una uhuru wakutoa maoni. Uhuru uliyopewa na katiba ya jamuhuri., mimi kadi ninayo!
 
Back
Top Bottom