Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,354
- 1,943
- Mkuu Dr. Kitila, maneno mazito sana isipokuwa tatizo moja ni kwamba kwanza Congress ya US wanajali sana Seniority ya mgombea, na pia heshima yake mjengoni hasa kwa upande wa pili kama ataweza ku-reach out na kusikilizwa, pia ability yake na compromise kwa masilahi ya taifa, bila kuathiri msimamo wa chama chake.
- Ushindani ndani ya vyama vya siasa ni muhimu sana, lakini ukweli ni kwamba masilahi ya chama ni lazima siku zote yawe mbele kuliko ukubwa wa kiongozi, infact hata huku US vyama hutumia tabia ya kulinda chama, ndio maana Gavana wa sasa anayemaliza muda wake New York State, alipotaka kugombea tena Rais Obama alimtumia ujumbe kwamba asichukue fomu kukilinda chama, Tent Lot aliambiwa na chama chake Republican kwamba asichukue fomu ya Minority Leader kwa sababu ya kashfa yake on Blacks kulinda chama, Gingrich aliweza kuwapenya Republicans bila kuchunguzwa vizuri mwennendo wake, matokeo yake akaishia kuwaingiza kwenye matatizo makubwa sana na kuishia kushindwa uchaguzi uliofuata wa Congress.
- Otherwise, Dr. Kitila una points nyingi sana na nzito sana, isipokuwa ninaomba kusema hivi, kwa maoni yangu tatizo linalotusumbua wa-Tanzania sio ushindani ndani ya vyama, isipokuwa kuambiana ukweli kiongozi anapokosea akiwa kwenye nafasi ya juu ya uongozi, ni wakati muafaka sasa tukajiwekea system ya kumuondoa kiongozi yoyote wa nafasi ya juu anapokosea, badala ya kusubiri mpaka uchaguzi ufike halafu kuanza kuchakachuana, kiongozi akikosea na kukiletea chama hasara kubwa mbele ya wananchi awajibishwe hapo hapao na haraka sana, Wenzetu ukitokea uchaguzi mdogo chama kikishindwa wahusika wanajiondoa au wanaondolewa haraka sana, sisi tunaanza kutafutana uchawi na kelele nyingi na yote ni kukwepa tu uwajibikaji.
Thanks.
William.
Brilliant! Ahsante sana. Nami nakubaliana kabisa mtu anayechaguliwa awe ni mtu anayeweza ku-command respect from all corners of the house. Mjadala mzuri na hoja ni murua. Ni vizuri mjadala wetu ukajikita kwenye misingi ya hoja, tuachane na majina kwa sasa. Tukishakuwa clear na principles za mtu tunayemtaka kuwa kiongozi wa upinzani bungeni, then tutaangalia ni nani katika waliopo anaye-fit katika hizo principles.