Zitto Kabwe kuwa kiongozi wa Upinzani Bungeni?

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,076
7,824
Kuna habari kuwa Zitto Kabwe anagombea nafasi ya kuwa kiongozi wa Upinzani Bungeni.

Taarifa zaidi, watch this space!
 

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,950
Zitto ana harufu ya CCM, i don't trust him anymore esp baada ya hoja zake kuhusu mitambo ya Dowans! Pia ni mfagiliaji mzuri wa CCM siku hizi!
 

Kituko

JF-Expert Member
Jan 12, 2009
9,558
9,283
Sijui ni kwa nini sijaipenda hiyo, Zitto angekaa pembeni tu
 

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,696
1,682
Kama Mwenyekiti wake yuko Bungeni, je isingekuwa busara na hekima amuachie Mbowe awe kiongozi wa upinzani? Unless kama Mbowe hagombei nafasi hii, nahisi inaweza tena ikawagawa katika makundi.

Kuna vijana wawili walioondoka Chadema wameshinda Kigoma. Wangekuwa CHADEMA ushindi ungeongezeka.
 

Anfaal

JF-Expert Member
Jan 19, 2010
1,154
113
Kama Mwenyekiti wake yuko Bungeni, je isingekuwa busara na hekima amuachie Mbowe awe kiongozi wa upinzani? Unless kama Mbowe hagombei nafasi hii, nahisi inaweza tena ikawagawa katika makundi.

Kuna vijana wawili walioondoka Chadema wameshinda Kigoma. Wangekuwa CHADEMA ushindi ungeongezeka.
Anaweza kufaa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA lakini si Kiongozi wa Upinzani. Hana uwezo huo, itakuwa aibu kwake na kwa CHADEMA.
 

Kituko

JF-Expert Member
Jan 12, 2009
9,558
9,283
japokuwa Kuna wabunge wengi wa upinzani, lakini CCM wanaanza kutumia strategy za chinichini za kuzima nguvu ya Bunge, just imagine Bunge litakuwaje, maana kuna RA, EL spika awe Chenge na naibu spika say Kinana (Kama akigombea) na msemaji wa upinzani awe Zitto
 

Mzee Wa Rubisi

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
1,758
437
Niliwai chart na mr zitto facebook kuhusu kugombea nafsi ya kiongozi wa kambi ya upinzani bunge alisema bado hajaamua na atatoa mwelekeo siyo sasa. Je katoa tamko hilo mkuuu ?
 

Facts1

JF-Expert Member
Dec 23, 2009
307
28
Siungi mkono busara ni kumwachia Mwenyekiti wa chama kuwa kiongozi wa upinzani angalia bunge la UK inapendeza kiongozi wa upinzani bungeni anakuwa kiongozi mkuu wa chama chake.
 

Anfaal

JF-Expert Member
Jan 19, 2010
1,154
113
Siungi mkono busara ni kumwachia Mwenyekiti wa chama kuwa kiongozi wa upinzani angalia bunge la UK inapendeza kiongozi wa upinzani bungeni anakuwa kiongozi mkuu wa chama chake.
Sio kila mfumo unaweza kufaa kila mahali. Kiukweli hana hata sifa za kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA. Angalau ndani ya CHADEMA anaweza kuvumilika ila si nje ya CHADEMA.
 

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,076
7,824
Niliwai chart na mr zitto facebook kuhusu kugombea nafsi ya kiongozi wa kambi ya upinzani bunge alisema bado hajaamua na atatoa mwelekeo siyo sasa. Je katoa tamko hilo mkuuu ?
Mkuu,

Sijakurupuka! Watch this space nakupa 24hrs utaona kama hajatoa tamko hilo
 

Butola

JF-Expert Member
Jan 19, 2010
2,290
749
Kama Mwenyekiti wake yuko Bungeni, je isingekuwa busara na hekima amuachie Mbowe awe kiongozi wa upinzani? Unless kama Mbowe hagombei nafasi hii, nahisi inaweza tena ikawagawa katika makundi.

Kuna vijana wawili walioondoka Chadema wameshinda Kigoma. Wangekuwa CHADEMA ushindi ungeongezeka.

Safari hii demokrasia ichukue mkondo, atakayeshindwa amuunge mkono mwenzake.

Binafsi ninaamini Zitto ana uwezo wa kuwaunganisha wabunge wa vyama vyote vya upinzani vilivyoko bungeni kuliko Mbowe, na ni muhimu sana kwa wabunge wote wa upinzani kuwa na sauti moja.
 

Membensamba

Senior Member
Nov 4, 2010
157
10
Sina tatizo Zito kuwa kiongozi wa upinzani bungeni, ila nadhani kuwa watu kama Lisu, kwa kuwa ni mwanasheria na mwenye uwezo na upeo mkubwa katika maswala ya jamii angefaa zaidi. Mwingine kwa sababu za ukomavu (maturity) wa kisiasa ni Mbowe.
 

Bulesi

Platinum Member
May 14, 2008
12,638
11,339
Siungi mkono busara ni kumwachia Mwenyekiti wa chama kuwa kiongozi wa upinzani angalia bunge la UK inapendeza kiongozi wa upinzani bungeni anakuwa kiongozi mkuu wa chama chake.

Chadema ni lazima wawe careful kwani nimekwisha ona mbinu za ccm zikianza kutaka kuwagawa hawa wabunge katika makundi kupitia kuutafuta uongozi wa upinzani!! Zitto ana baggage nyingi za ccm toka enzi za Dowans haaminiki; kama sio Mbowe basi hata Halima Mdee ana uzoefu anaweza kuwa kiongozi wa upinzani na akamudu zaidi ya Zitto!!
 

Kaa la Moto

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
7,896
1,029
Kama Mwenyekiti wake yuko Bungeni, je isingekuwa busara na hekima amuachie Mbowe awe kiongozi wa upinzani? Unless kama Mbowe hagombei nafasi hii, nahisi inaweza tena ikawagawa katika makundi.

Kuna vijana wawili walioondoka Chadema wameshinda Kigoma. Wangekuwa CHADEMA ushindi ungeongezeka.
Lakini ni vijana wasio na displine. Ni afadhali wakakaa mbali nasi kuliko kuwa nao kama mzigo ndani ya chama. Mi nadhani tutashirikiana nao vizuri wakiwa nje ya chama kuliko walivyokuwa ndani ya chama. Mnamkumbuka Kafulila na battle ya zitto na wenyekiti? Wacha akae na Mbatia huyo watawezana maana ni wale wale tu, undisciplined.
 

Anfaal

JF-Expert Member
Jan 19, 2010
1,154
113
Chadema ni lazima wawe careful kwani nimekwisha ona mbinu za ccm zikianza kutaka kuwagawa hawa wabunge katika makundi kupitia kuutafuta uongozi wa upinzani!! Zitto ana baggage nyingi za ccm toka enzi za Dowans haaminiki; kama sio Mbowe basi hata Halima Mdee ana uzoefu anaweza kuwa kiongozi wa upinzani na akamudu zaidi ya Zitto!!
Hapa tunachanganya vitu. Si kwamba Zitto haaminiki, la hasha, Zitto anasema ukweli muda woote hata kama ukweli huo unawaudhi wenzake ndani ya CHAMA. Kwa ujumla Zitto anasimamia maslahi ya Watanzania zaidi kuliko maslahi ya kisiasa ndio maana kwake hata kugombea ubunge haikuwa kazi ngumu. Ipo mifano mingi tu juu ya utendaji wake na muono wake ila mfano mkubwa atakuwa ni Kafulila aliyeshinda ubunge huko Kigoma.
 

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
795
hawa chadema waangalie wasije wakaharibu mambo

Je, Chenge kugombea nafasi ya Spika ni sahihi? Maana ninaanza kupata mashaka kwamba nawe mgombea ubunge kupitia CCM mawazo yako yamekaa kiitikadi zaidi. Angalieni na ninyi, mkienda kwa mwendo huu hata huko vijijini moto wa mabadiliko unakuja, hamtaendelea kuwadanganya wananchi kwa sera za kiungo uongo kwa kutumia ujinga na umasikini wao kama mtaji.
 
0 Reactions
Reply
Top Bottom