Nduka
JF-Expert Member
- Dec 3, 2008
- 8,552
- 2,359
Wenzeni wa EA wameanza kwenda huko na kutengeneza nafasi za kujasiria mali toka mwaka jana! Kwa sasa sidhani kama kuna nafasi tena!
Niliwaaandikia hapa mapema kuwa Sudani ya kusini wenzenu Wakenya, Waganda na Wanyagwesi wameshaanza kujikita huko lakini sisi tuko kwenye ushabiki maandazi bado!!
Kisha mwisho wa siku tutakuja kusema hapa EA haituthamini!
Wenzetu wanatoka kutafuta nafasi, sisi tunasubiri nafasi zije!!!
Ndio maana migodi yetu inajaa wageni kisha wasomi wetu wanalalamika hawapati ajira!!
Sisi mambo ya msingi kwa sasa ni POSHO za wabunge, zamani kidogo ilikuwa katiba na Dowans na zamani saaana ilikuwa EPA hayo mengine waachieni wakenya sawa?