Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 80,914
- 93,671
GoodUmemaliza kazi
GoodUmemaliza kazi
Chadema huwa haikosei kila inachosema na kufanya siku zote huwa ni sahihi tu, na upinzani ndio wenye akili nchi hii na ukizingatia chadema ndio chama pekee cha kweli cha upinzani Tanzania na vyengine vyote ni mamluki tu wa ccm.Tatizo la ZITO ni kuwadhidi akili CDM wote....ZZK ana akili nyingi kuliko chadema wengi....
Leo humu CDM wanamuita ZZK ndumilakuwili wanasahau ile issue ya Lowassa na kumsaliti kamanda wao Dr Slaa ndio inawafanya ndumilakuwili namba moja duniani..
Kila siku CDM mnapokea masalia kutoka CCM na watu wenu wengi kila siku wanakimbilia CCM tena wenye hadhi na nyadhifa halafu bado mnamuita ZZK CCM...
Kwani Zitto yupo ccm au mnasema anatumika na ccm? Sasa na Maalim seif ilikuaje akaenda kujiunga na mamluki wa ccm na tena akakubali cheo ambacho mlitegemea hatokikubali kwa sababu ya kilichotokea kwenye uchaguzi ila wapi Maalim aliamua kukikubali hicho cheo.
Sasa sijui ni nini unataka kutetea wakati kila kitu kipo wazi, Maalim aliungana na mamluki wa ccm na mwishowe akapewa cheo na akakikubali ni sawa vilevile Lissu alivyomsema Anna Mgwila kwamba alipewa zawadi ya cheo baada ya kutekeleza kazi ya ccm.
Tuwekane sawa hapa, hivi wakati Maalim seif alipoamua kujiunga na Act alijua kwamba Act ni mamluki au hakujua? Kama alijua kulikuwa na sababu gani ya msingi ya yeye kulazimika kujiunga na mamluki kwani chadema hakuiona ambayo si mamluki?Maalim sasa alijiunga na ACT akiwa na full control ya huko Zanzibar, hajawahi kuwa na moto sana na huku Bara. Hicho cheo alichopewa kilikuwa na power zote, na hakuna lolote Zito angeweza kuamua bila Maalim Seif kukubali.
Tuwekane sawa hapa, hivi wakati Maalim seif alipoamua kujiunga na Act alijua kwamba Act ni mamluki au hakujua? Kama alijua kulikuwa na sababu gani ya msingi ya yeye kulazimika kujiunga na mamluki kwani chadema hakuiona ambayo si mamluki?
Au Maalim seif hakuwa akitambua kwamba Act ni mamluki? Au kwamba alijiunga na Act ili tu apate nafasi ya kugombea urais zanzibar na hakuwa akijali kuhusu umamluki wa Act?
Na vp kuhusu cheo alichopewa ambacho mlitegemea kwamba hatokikubali na ataonesha upinzani wa kweli kwa kukikataa ila mwisho wa siku akakubali kile cheo, je hili unalizungumziaje?
Una maanisha Chadema kuna wenyewe hivyo isingewekana mafahari wawili kukaa pamoja ndio maana akaona bora aungane na mamluki wa ccm na kweli alifanikiwa kupata cheo.Kwa taarifa yako nguvu aliyokuwa nayo Maalim Seif asingeweza kuipata akiwa cdm, hivyo akatafuta chama ambacho atakuwa na maamuzi nayo. Hicho cheo unachosema tulidhani atakikataa Kwanza mimi sio mmoja wa dhana hiyo. Hata hivyo cheo alichopata bado alikuwa na maamuzi kuliko huyo Zito. Na ndio maana Zito Membe agombee urais, lakini Maalim Seif alimgomea na kumtaka Lisu.
Una maanisha Chadema kuna wenyewe hivyo isingewekana mafahari wawili kukaa pamoja ndio maana akaona bora aungane na mamluki wa ccm na kweli alifanikiwa kupata cheo.
Kiujumla unachoeleza ni kwamba Maalim alikuwa anaangalia masilahi yake binafsi.
Kwahiyo Chadema angeshindwa kudhibiti ambayo angeona si sawa ndio maana ukasema asingekuwa na nguvu chadema ambayo alikuwa nayo Act, hapo umenikumbusha sakata la Maalim na Lipumba.Nguvu waliyonayo cdm hata bila ushirikiano na yoyote wanajimudu. Maalim Seif angejikuta kwenye sehemu ngumu kuwa na maamuzi aliyokuwa nayo ACT. Na kwa taarifa yako kuna ACT na Zito, maamuzi ya ACT yanafanywa na wapemba, ila Zito kwakuwa ndio mwenye chama huwa ana ajenda zake toka kwa waanzilishi halisi wa ACT ambao ni JK, Membe, Mwigulu, Januari, Nape nk. Maalim Seif aliweza kwenda ACT kwani ni chama kidogo, na kiongozi wake ni muislamu tofauti na ilivyo Nccr, TLP, UDP nk. Hivyo kutokana na muda kuwa umeisha asingeweza kuanzisha chama, hivyo ilibidi atafute chama kilicho tayari, ndio zali likawaangukia ACT. Hao wanaccm wafadhili wa ccm Maalim Seif alijua atawadhibiti akiwa ndani, mfano alivyomdhibiti Membe na Zito hakufanya lolote.