Zitto Kabwe ailipua Airtel bungeni dhidi ya TTCL

Zitto Kabwe ailipua Airtel bungeni dhidi ya TTCL

Hilo shirika liachwe life tu ndio solution

Maana huo mkopo waliopewa na serikali hazijarudi mnataka wapewe pesa ingine

Wacha shirika life au livunjwe vipande vipande wapewe wanaoweza kuendesha.
 
Na umeme wa Tanesco si biashara?au Tanesco si ya Serikali?

Usiwe na papara. Serikali haifanyi biashara kwa mafanikio zaidi ya ufujaji mali kupita kiasi mashirika ya umma unadhani ni tanesco peke yake? Yako kibao yaliyokufa au umezaliwa tisini?....sorry for being behind. Tanesco will not last longer either...
 
mkuu hakutoa hata senti kuwekeza ttcl kama m bia zaidi anataka alipwe bilioni 21 ili aondoke
ATCL ingine hii, mtu anakusababishia hasara na bado anakudai!!
 
Hivi sisi tunaweza nini jamani? ATCL, TRL, TTCL zote bure kabisa? Tatizo ni nini??
Hakuna committed long term objectives plus poor managements,atlest watetezi wa TTCL wanakesi ya kurubuniwa na viongozi wa serikari. Still I dont buy the argument ya Airtel kuwahujumu kwa sababu on their part their interest in the company could be strategic partnership kufikia malengo yao, what were TTCL own plans to compete on the market.

Maana kuna watu wanaungana kwa sababu ya infrastructure tu, serikari za dunia ya kwanza zina miliki infrastructure karibu zote kwenye utility sector na kuna mashirika binafsi na ya serikari yanatumia infrastrucutre hizo hizo lakini uwezi kusikia taasisi za serikari zikilaumu washindani; ukishindwa ni kwa sababu auna good business plan simple na wala serikari azina muda wa kukusaidia provided jamii aiathiriki kutokuwepo kwako. Kwa upande wetu tunadhani tukiitoa infrastructure ya kusambaza umeme mikononi mwa TANESCO inaweza kuwa bora wakati issue ni poor management isyokuwa na long terms wala clear short term target yaani haya mashirika yamekuwa yakishepiwa na kamati PAC na ripoti za CAG sasa uongozi una ubunifu gani wa ndani.

Jamaa inabidi wazinduke na enough of this competition blame wamepewa pumzi na hao Hauewi which is good news but then tayari jamaa anadai part of the agreement TTCL itauza simu za Hauwei tu, kama wateja wanapendezewa na makers wengine lakini are happy with their phone tarrifs inabidi wachague kati ya simu na service uoni tayari washaanza mkataba at disadvatage. Halafu baadae waanze tena kumlaumu mwekezaji why act so desperate bila ya kuangalia terms and conditions za kibiashara na kufanya vitu kwa objectives zako ni mtu asiye ni mikakati yake ya muda mrefu ndio anaweza yumbishwa on strategy.

The irony ni kwamba waziri pekee aliekuja na jitihada za ku-introduce framework za kuhakikisha mikataba ya serikari ina faida kwa watanzania ata kama yeye akitoka, TANESCO inabadilisha mbinu za uzalishaji ndio tumemuwekea mizwenge atoke only in Tanzania.
 
na ukweli ni kuwa tukuziwa na sisi tutaamia huko na kutumia mtandao huo.

Tena haraka sana!

Na hutasikia kitu kinaitwa Vodacom au Tigo ndani ya mwaka mmoja ,muhimu kuwa na accountable management and strong Board Member-ambao lazima wanashare ndiyo watakao wa weka Ofisini na hii ikiwa pamoja na CEO


Mfumo kama huu;ulifaa uanze na Taasisi kama NSSF,PPF nk kwamba CEO na Board yake siyo wakuteuliwa na Serikali bali nafasi iombwe na Mwananachama wawe wapiga kura.
 
Nimei like kwa sababu kujitambua lakini siyo kwamba hilo jibu la tatizo la msingi.
Nani kawaweka Ofisini CCM-siyo mimi ,wewe na Watanzania wengine?

Niombe radhi kaka. Mimi sijawaweka CCM ofisini. Wala sitakaa nitende dhambi hiyo. Anyway, point yangu ni kwamba tatizo la TTCL ni systemic and I think it will be misleading to put all the blame on TTCL management. And I am not at all saying that TTCL management is not part of the system responsible for cannibalizing the oldest telecommunication company in Tanzania.
 
Kwanza kabisa napenda kuishukuru kamati ya bunge a PAC wa kazi nzuri wanayoifanya. Na hakika pasipo wao hili swala la TTCL -ATCL lingeendelea kuwa escrow nyingine ambayo wataalam wetu kama nd. Kamugisha hupuuzwa na wanasiasa kwa sababu wao nia na malengo yao wanataka kuyauwa mashirika haya ili miradi yao binafsi walowekeza katika mashirka kama Voda na Tigo yasipate ushindani toka serikali. Tumeyaona kwenye TRA ambayo inapigwa vita kutoweza kujiendesha kwa sababu viongozi wengi wamewekeza kwenye usafiri wa watu na mizigo. ATC pia viongozi wamewekeza ktk mashirka ya ndege binafsi na hawataki ushindani isipokuwa monopoly maana wanajua hawawezi kushindana na seirkali katika nchi maskini.

Mimi nayakumbuka vizuri sana maneno ya mwalimu alipokuwa akizungumzia Ubepari na uwezo wetu ya kwamba hatuwezi kushindana na nchi matajiri, akatoa mfano wa mabondia ya kwamba hatuwezi kuingia ulingoni kushindana na na Heavy weight (nchi tajiri) ilihali sisi ni Flyweight (nchi maskini). Na ilionekana wazi wakati wa Ujamaa kwani shule za serikali zilikuwa na elimu bora zaidi kuliko shule za private, Hospital za serikali zilikuwa na uwezo zaidi ya private na hii ni kutokana na uwezo mdogo wa wananchi wenyewe katika uwekezaji binafsi. Kinachotokea leo ni kwamba viongozi wanaiba mtaji toka serikalini na kuwekeza wao kama vile hii ni mali ya urithi!

Sasa leo hii baada ya kuingia ubebari, tunakuta adui wetu ni viongozi wetu wenyewe ambao ni maskini lakini wako radhi kufanya kila hila kuzuia ushindani na serikali kwa sababu wanajua nguvu ya serikali ni kubwa tofauti na nchi tajiri ambako vyanzo vya uwekezaji (financial institution) wameisha jenga mahusano makubwa na matajiri hivyo ubunifu wowote wa tajiri mmoja ana uwezo wa kutosha kumiliki sekta nzima ya kutoa huduma bora.

Hatuwezi kuupamba Ubepari kwa kuyapaka tope mashirika ya Umma na haswa pale tunapofahamu kwamba ni viongozi wetu wanaoipiga vita miradi ya serikali. Mimi naamini kwamba hadi hapo atakapo patikana Sokoine mwingine, kiongozi atakaye anza kutazama uongozi wa ndani na kupiga vita Grand corruption na economic sabotage hapo ndipo watu kama Kamugisha wataweza kuifanya kazi.

Mkuu Mkandara nafahamu uchungu unaoupata linapokuja suala la TTCL na hasa jambo linaloonekana kumwondolea 'sifa' rafiki yako Dr. Kamu.

Nikueleze wazi tu kuwa Kamugisha ni moja ya 'brains' chache sana tulizonazo watanzania. Sina shaka na uwezo wake wa kufikiri na kufanya maamuzi. Nimefanya nae kazi kwa ukaribu namfahamu.

Kamu ni 'mtoto wa Ikulu'. Nadhani hilo peke limechangia kuisaidia TTCL. Amelelewa katika mifumo ya kimamlaka na utawala uliopo sasa. Kwangu mimi hilo limenifanya niamini kuwa hata masafa haya ambayo TTCL imeyapata ni kutokana na hilo. Unajua Mkandara haya masafa ambayo TTCL wamepewa TCRA walitaka kuyapeleka kwenye mnada. Eti TTCL ishindane na Vodacom na Airtel kwenye mnada wa wazi wa kupata hayo masafa. Utaona ni wazi kuww hata TCRA yenyewe haina dhamira njema na TTCL kampuni ya simu ya Taifa. Lakini tunaelezwa kuwa Kamu aliinfluence TTCL wapate hayo masafa 'kiubwete'.
Kabla ya Kamu wamepita ma-CEO kadha wakiwa na slogan ya kumtoa mnyonyaji Airtel. Wamechemsha. Kamu amefanikiwa kuwatoa. Amepambana na sasa wana finalize vitu vidogo sana Airtel atoke. Kimsingi ameshatoka na ndio maana sasa TTCL imeanza kuingia mikataba mizito na stakeholders wakubwa.
Jambo kubwa ambalo TTCL inaliishi ni kutokujua 'kesho kutatokea nini'! Maisha haya yamekuwa yakiisongasonga TTCL tangu ilipotenganishwa na Posta.
Zipo taarifa kuwa Kamu anatakiwa kuondoka TTCL 'apangiwe kazi nyingine' mahali pengine. Kama hilo litatekelezwa unaweza kuona TTCL itarudishwa nyuma kwa umbali gani. Lingine ni kuwa TTCL haijui kesho serikali itaamua nini. Nasikia hata Mikopo kwenye mabenki wametoa sharti kuweka dhamana ya majengo ya TTCL yaliyotapakaa nchi nzima wenyewe wanayaita 'telephone houses'. Sababu tu ni kuwa serikali inasuasua kuidhamini TTCL.
Na yapo maelezo ambayo hayasemwi lakini yapo kuwa hata hapa TTCL ipo hapa ilipo kutokana na attitude binafsi za JK towards TTCL. Inasemwa kuwa JK ana interest binafsi(positive interest) na TTCL na ndio maana alimwita Kamu aongozan e naye kwenye safari yake ya China na hivi karibuni ambapo China imekubali kusaidia TTCL kwenye mambo mengi ya kiufundi.
Hofu ni kuwa 'kesho' JK anaondoka madarakani. Huyo atakayekuja atakuwa kama JK?
 
Last edited by a moderator:
haa haaa mkuu we bado mchanga sana kwenye hizi mambo, yan uko nyuma mno ndugu,, but kwa leo let me devote my time nikulishe madini kidogo ila next time just shut your mouth if u dont understand, mimi nimeongelea "a series chip " manufacturing we unaleta habari za copy cat, kwa taarifa yako naelewa kesi kibao za patents btw the two companies, ila kwa hili uko chaka mbaaaya and u need to learn from me.

hapa nakupa link ukasome

Apple is one of Samsung's biggest customers for processors and memory chips. But the two firms compete directly in the mobile-phone market and have spent the better part of the past two years suing and countersuing over the look,(http://www.wsj.com/)

[h=1]Apple’s A7 chip again made by Samsung, camera by Sony and non-descript ‘M7′ chip by NXP(9to5Mac: Apple iPhone, Mac and iPad News Breaking All Day)[/h]

Kim Ki-nam, president of the Korean electronic giant's semiconductor business and head of System LSI business, told reporters at Samsung's headquarters in Seoul that once the company begins to supply Apple with chips using its latest technology, profits "will improve positively"(http://www.zdnet.com/)

FYI
Samsung S5 using 2.5GHZ quad-core processor
Iphone was using A7 but now are using M7 &A8 processor manufactured by TSMC(EXCLUSIVE MANUFACTURER OF APPLE'S PROCESSORS) NOW ARE DESIGNING M8 PROCESSOR
Hutaki kunya boga
 
FYI
Samsung S5 using 2.5GHZ quad-core processor
Iphone was using A7 but now are using M7 &A8 processor manufactured by TSMC(EXCLUSIVE MANUFACTURER OF APPLE'S PROCESSORS) NOW ARE DESIGNING M8 PROCESSOR
Hutaki kunya boga
am glad sa hivi umejifunza kitu ...
hiyo A7 ya apple ilitengenzwa na nani ? toa jibu alafu rudi kwenye post yako ya kwanza ..
 
Nyepesi zinasema kua, izo hisa 30% ni za vigogo fln fln wa serikali. Kuwanyang'anya ni vita nzito
 
Watanzania hatujambo kwa kushughulikia OUTCOMES ... Huyu Mwandosya alie facilitate ubinafsishaji wa TTCL na deals za Celtel/Zain/Airtel anapeta maisha yanakwenda... Lema amesema kweli tupu kuwa Nchi imegeuka GHETO! Kila mwenye nafasi anajichukulia atakacho ...
 
MHE MAZINDU MSAMBULE; hakukuwa na uzembe upande wa watendaji wa ttcl hata kwenye hilo la simu zinazoanzia 073. unachatakiwa kujua ni kuwa TTCL ndio ilikuwa kampuni ya kwanza kumiliki licence ya mobile hapa nchini kwenye masafa ya GSM, lkn viongozi tajwa walifanya mbinu chafu, airtel ilianzishwa na kutumia masafa hayo aya TTCL, huku ikitumia kila rasilimali zoote za TTCL hadi kiuimama tukiamini ni mali ya TTCL, viongozi hao kwa kile walichokuwa wanakijua ,baada ya celtel (airtel/zain)kusimama ,ndio wakaitoa isiwe tena ndani ya TTCL. ukumbuke wakati huo viongozi waliokuwepo ttcl ni wazungu waliowekwa kwa makusudi maalum, kwa hiyo haukuwepo uwekezaji wa kuipeleka mbele TTCL, baada ya wafanyakazi kupiga kelele, ndio serikali ili kupunguza kelele hizo ikaawapa masafa ya CDMA ambayo hadi leo ni kimeo, sasa kwa juhudi za managment ya wazawa wakishirikiana na chama cha wafanyakzi TEWUTA wamefikisha TTCL hapa unapoiona , kwa ufupi TTCL kwa sasa iko ktk kufufuka hasa baada ya huyo mbia mnyonyaji kutimua vumbi kwa kelele za umma. muda si mrefu pamoja na hujuma tuliokuwa tunafanyiwa VODA , TIGO. AIRTEL . watasoma namba.

Nimekuelewa vizuri sana ndugu yangu, is like tunazungumza lugha moja; historia ya TTCL ninaifahamu vizuri sana tokea day 1 zilipotengana na shirika la posta huo mwaka 1993, ulichokisema hapa ni kweli tu na kuna na mengine hujayasema nadhani kwa nia nzuri tu, mfano ni hili moja; Celtel hawakuja na mtaji wa kuwekeza kwenye mobile phones achilia mbali kibali cha uendeshaji wa simu za mkononi, walichokifanya hawa jamaa ni kukusanya madeni yote ya TTCL (kama utakumbuka, waliwahi kukata mawasiliano hadi ya Ikulu, nadhini ilikua mwaka 2001 hadi Ikulu ilipolipa deni/bills ilizokua ikidaiwa) madeni yote waliyokua wakilipwa wakawa wanajenga minara ya simu za Celtel, wengi wetu tukanunua line za Celtel tukijua hi ndio TTCL wakati, mara walipoona wameanza kujijenga vya kutosha, wakagoma kulipa malipo ya mwisho ya ununuzi wa hizo hisa 35, wakaiacha TTCL hivi hivi, point yangu nilio walaumu hawa viongozi wa TTCL wa sasa ni hi; mbona hawasikiki kabisa kwenye matangazo ya biashara? Watu wengi hawajui kama hili shirika lao la kizalendo linatoa huduma ya simu za mkononi na hizi kubwa kubwa za mezani but wireless, kwa siye wenye watoto nyumbani na baba na mama tupo busy ni nzuri sana hizo simu, mimi ninayo 1 but hivi ni lini uliwahi kusikia wanajitangaza? Hilo moja, linguine ni hili; kwanini hizo simu zao za mkononi na hizo wireless li lazima uende ukanunue kwao tu? Chip wauze wao, hand set nazo wauze wao, mbaya zaidi hand set za aina nyingine yoyote line zao hazisomi? hivi huo ni ubunifu wa kuifanya kampuni isonge mbele au kuiua? Ndio maana nikatolea mfano wa Start TV na ving'amuzi vyao, kwa hili TTCL wamechemka, wenzao tiGo, Airtel Voda (sina hakika na Zantel) wanatoa simu za promosheni and then line nyingine hazisomi kwenye hizo hand set zao ingawa line hiyo hiyo unaweza kuweka kwenye hand set nyingine na ikasoma pia, huo ndio ubunifu!
 
Back
Top Bottom