Zitto Kabwe ailipua Airtel bungeni dhidi ya TTCL

Zitto Kabwe ailipua Airtel bungeni dhidi ya TTCL

Unataka kuturudisha jehanamu?

TTCL ifufuke tufurahie huduma maridhawa na kwa bei nafuu. Airtel ikiwezekana apokonywe hizo hisa

TTCL inaweza fanya vizuri sana lakini tatizo ni je, viongozi wa CCM ambao wamezoea kuomba wataacha kuomba airtime za bure???

Kumbuka hata nguvu ya airtel sasa hivi ni matokeo ya hao hao, kuanzia enzi za akina Mwandosya. Ufisadi na kuwinda shares kwenye mashirika.
 
TTCL inaweza fanya vizuri sana lakini tatizo ni je, viongozi wa CCM ambao wamezoea kuomba wataacha kuomba airtime za bure???

Kumbuka hata nguvu ya airtel sasa hivi ni matokeo ya hao hao, kuanzia enzi za akina Mwandosya. Ufisadi na kuwinda shares kwenye mashirika.

Nilishasema hapa na narudia tena. Matatizo ya TTCL Mwandosya alihusika sana, baada ya huo ufisadi alipewa asante na hao mabepari ya kusomeshewa mtoto wake chuo kikuu Afrika Kusini. Afadhali na wewe unalijua hilo
 
Nilishasema hapa na narudia tena. Matatizo ya TTCL Mwandosya alihusika sana, baada ya huo ufisadi alipewa asante na hao mabepari ya kusomeshewa mtoto wake chuo kikuu Afrika Kusini. Afadhali na wewe unalijua hilo

Mwandosya ni sehemu ya maProfesa hovyo kabisa! Kumbuka akiwa wizara hiyo ndo alimuleta Prof. Nkoma wa TCRA ambaye ikaja julikana kwamba siyo raia wa nchi hii. Sababu ya kumuleta anaijua mwenyewe na bahati mbaya CCM hupeana shavu bila hata sababu.

Eti Mwandosya naye akatamani kuwa Rais! Hii nchi ni bwabwa. Kila mtu analawiti atakavyo.
 
bad idea

NHC ni disaster in the making... mark my words
Wachache sana watakuelewa wambiye madeni wanayo daiwa NHC ni ebola!!
Ila TTCL ingefufuliwa alafu wakatuambia kampuni ni ya watanzania na wakaepuka ufisadi watanzania wote tungeungana tungechukuwa line za TTCL hao wezi wangekimbia tu bila kukimbizwa!
 
Shida siyo makampuni ya toka Nje Shida ni sisi Watanzania-Tabia hii ya kuwaacha watendaji kugeuza Taasisi ya Umma kama kamapuni zao binafsi matokeo yake ndiyo haya.

Well said mkuu,tatizo kubwa la Taifa letu ndilo hilo i.e ku-personalise Taasisi za Umma na kuzi-run kama mali ya ukoo, tukikwama tunasingizia wawekezaji.
 
Wachache sana watakuelewa wambiye madeni wanayo daiwa NHC ni ebola!!
Ila TTCL ingefufuliwa alafu wakatuambia kampuni ni ya watanzania na wakaepuka ufisadi watanzania wote tungeungana tungechukuwa line za TTCL hao wezi wangekimbia tu bila kukimbizwa!

Mkuu, kwa sasa NHC wanaangaliwa na kupimwa kwa kuwa na inventory, but after so time, things will change, kitakachoongea ni liquidity and positive finances/business scenario... If not carefully watched, NHC itaenda under water na zile nyumba zitauzwa kwa bei ya Mark II
 
Watanzania tunaipenda nchi yetu sana ila shetani ccm anatupeleka motoni jinsi watanzania tunavyo ipenda inchi yetu tulitakiwa kuwa mfano wa kuigwa na mataifa makubwa ila tamaa mbaya za walafi ccm zimetunyima hiyo sifa mungu awalani
 
TTCL walitutesa sana kabla ya uwepo ya kampuni za simu za mikononi. Kuunganishwa line hadi rushwa,line ikikorofisha matengezo rushwa. Wachie wafe natural death. Ndio yale yale ya TANESCO ineffective inefficient.
 
Mwandosya ni sehemu ya maProfesa hovyo kabisa! Kumbuka akiwa wizara hiyo ndo alimuleta Prof. Nkoma wa TCRA ambaye ikaja julikana kwamba siyo raia wa nchi hii. Sababu ya kumuleta anaijua mwenyewe na bahati mbaya CCM hupeana shavu bila hata sababu.

Eti Mwandosya naye akatamani kuwa Rais! Hii nchi ni bwabwa. Kila mtu analawiti atakavyo.

kumbuka alipewa bakshishi ya kusomeshea mtoto
 
TTCL walitutesa sana kabla ya uwepo ya kampuni za simu za mikononi. Kuunganishwa line hadi rushwa,line ikikorofisha matengezo rushwa. Wachie wafe natural death. Ndio yale yale ya TANESCO ineffective inefficient.
Makaburu yanajuwa kiswahili siku hizi au we ni m.......
 
Makamba yeye yuko busy kutangaza ki-booklet chake kwenye media akijipambanua kuwa mchapakazi hodari.

Ilhali wizara anayoisimamia iko full madudu.
 
Mkuu, kwa sasa NHC wanaangaliwa na kupimwa kwa kuwa na inventory, but after so time, things will change, kitakachoongea ni liquidity and positive finances/business scenario... If not carefully watched, NHC itaenda under water na zile nyumba zitauzwa kwa bei ya Mark II
Mkuu kasim kangu hakana kitufe cha like NHC ni Janga kweli kweli miradi ya nyumba za kipuuzi kweli kweli kwa wale wenye uwezo wa kuangalia kwa jicho la tatu!
hizi nyumba za mikopo ya $ wakati kila mtu anakiwanja chake anajenga ni hatari kweli kweli sijuwi tumemkosea nini mungu!!
 
Kwanza kabisa napenda kuishukuru kamati ya bunge a PAC wa kazi nzuri wanayoifanya. Na hakika pasipo wao hili swala la TTCL -ATCL lingeendelea kuwa escrow nyingine ambayo wataalam wetu kama nd. Kamugisha hupuuzwa na wanasiasa kwa sababu wao nia na malengo yao wanataka kuyauwa mashirika haya ili miradi yao binafsi walowekeza katika mashirka kama Voda na Tigo yasipate ushindani toka serikali. Tumeyaona kwenye TRA ambayo inapigwa vita kutoweza kujiendesha kwa sababu viongozi wengi wamewekeza kwenye usafiri wa watu na mizigo. ATC pia viongozi wamewekeza ktk mashirka ya ndege binafsi na hawataki ushindani isipokuwa monopoly maana wanajua hawawezi kushindana na seirkali katika nchi maskini.

Mimi nayakumbuka vizuri sana maneno ya mwalimu alipokuwa akizungumzia Ubepari na uwezo wetu ya kwamba hatuwezi kushindana na nchi matajiri, akatoa mfano wa mabondia ya kwamba hatuwezi kuingia ulingoni kushindana na na Heavy weight (nchi tajiri) ilihali sisi ni Flyweight (nchi maskini). Na ilionekana wazi wakati wa Ujamaa kwani shule za serikali zilikuwa na elimu bora zaidi kuliko shule za private, Hospital za serikali zilikuwa na uwezo zaidi ya private na hii ni kutokana na uwezo mdogo wa wananchi wenyewe katika uwekezaji binafsi. Kinachotokea leo ni kwamba viongozi wanaiba mtaji toka serikalini na kuwekeza wao kama vile hii ni mali ya urithi!

Sasa leo hii baada ya kuingia ubebari, tunakuta adui wetu ni viongozi wetu wenyewe ambao ni maskini lakini wako radhi kufanya kila hila kuzuia ushindani na serikali kwa sababu wanajua nguvu ya serikali ni kubwa tofauti na nchi tajiri ambako vyanzo vya uwekezaji (financial institution) wameisha jenga mahusano makubwa na matajiri hivyo ubunifu wowote wa tajiri mmoja ana uwezo wa kutosha kumiliki sekta nzima ya kutoa huduma bora.

Hatuwezi kuupamba Ubepari kwa kuyapaka tope mashirika ya Umma na haswa pale tunapofahamu kwamba ni viongozi wetu wanaoipiga vita miradi ya serikali. Mimi naamini kwamba hadi hapo atakapo patikana Sokoine mwingine, kiongozi atakaye anza kutazama uongozi wa ndani na kupiga vita Grand corruption na economic sabotage hapo ndipo watu kama Kamugisha wataweza kuifanya kazi.
 
Nadhani hakuna cha maana hapa zitto mkurupukaji tu wala hajua kutazama mambo kwa mbali.
 
Shida siyo makampuni ya toka Nje Shida ni sisi Watanzania-Tabia hii ya kuwaacha watendaji kugeuza Taasisi ya Umma kama kamapuni zao binafsi matokeo yake ndiyo haya.

Hakika hujayaelewa matatizo ya ATCL.
 
Back
Top Bottom