Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,306
- 271,600
Kiongozi Mkuu mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa zamani Zitto Kabwe amefunguliwa Kesi na Harbinder Singh Seth akidaiwa kumkashifu mfanyabiashara huyo na kumvunjia heshima mbele ya jamii
Akizungumza na wanahabari leo Zitto Kabwe amesema kuwa kesi hiyo imetokana na yeye kuzungumzia sakata la IPTL (Kampuni ya kufua umeme) ambapo Seth ameomba kulipwa ‘mabilioni’ ya fedha
"Nimewaita hivi leo kwasababu ya kesi ambayo nimefunguliwa na mtu anayeitwa bwana Harbinder Singh Seth kuwa nimemkashifu na kumshushia heshima mbele ya jamii kwa vile eti nimezungumzia sakata la IPTL (Kampuni ya kufua umeme), na ameomba mahakama mbali na mambo mengine nimlipe ‘mabilioni’ ya fedha"
"Tuhuma hizo za bwana Seth kwanza si za kweli, kwasababu sijamkashifu na wala kumshushia heshima, lakini ninampongeza sana na kumshukuru kwa ujasiri wake wa kunishitaki kwasababu kesi hii itatoa fursa ya kumaliza jambo hili linaloweka wingu kwa muda mrefu sana katika taifa letu, lakini pia kesi hii itanipa nafasi ya kuweka ukweli wote wazi na mwisho kuufukia kabisa huu mzoga unaoitwa sakata la IPTL"
"Binafsi sikatai kuandika maneno ambayo bwana Seth (Harbinder Seth- Mmiliki wa kampuni ya IPTL ya ufuaji wa umeme) ananituhumu nayo kwamba nimemkashifu , maneno hayo niliyaandika na kuyachapisha katika akaunti yangu ya X zamani Twitter, na maneno yale yanaakisi picha halisi na yenye ukweli wa jambo zima hili la IPTL"
"Pili maneno haya mimi niliyaongea kwa nia njema kabisa, ya kutaka kupata ufumbuzi wa sakata hili, na tatu, maneno yale niliyasema kwavile mimi nilibahatika kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyoshughulikia sakata la IPTL"
"Kama unakumbuka wakati ule maarufu lilivyojulikana kama sakata la Escrow, hivyo nilitumia fursa hiyo kuwaeleza Watanzania wenzangu ukweli wa jambo hili, kwasababu ninafahamu ukweli wa jambo hilo, na ni wajibu wangu kama raia kulinda rasilimali za taifa dhidi ya njama zozote zile za kupora rasilimali hizo kwa kisingizio cha uwekezaji".
Akizungumza na wanahabari leo Zitto Kabwe amesema kuwa kesi hiyo imetokana na yeye kuzungumzia sakata la IPTL (Kampuni ya kufua umeme) ambapo Seth ameomba kulipwa ‘mabilioni’ ya fedha
"Nimewaita hivi leo kwasababu ya kesi ambayo nimefunguliwa na mtu anayeitwa bwana Harbinder Singh Seth kuwa nimemkashifu na kumshushia heshima mbele ya jamii kwa vile eti nimezungumzia sakata la IPTL (Kampuni ya kufua umeme), na ameomba mahakama mbali na mambo mengine nimlipe ‘mabilioni’ ya fedha"
"Tuhuma hizo za bwana Seth kwanza si za kweli, kwasababu sijamkashifu na wala kumshushia heshima, lakini ninampongeza sana na kumshukuru kwa ujasiri wake wa kunishitaki kwasababu kesi hii itatoa fursa ya kumaliza jambo hili linaloweka wingu kwa muda mrefu sana katika taifa letu, lakini pia kesi hii itanipa nafasi ya kuweka ukweli wote wazi na mwisho kuufukia kabisa huu mzoga unaoitwa sakata la IPTL"
"Binafsi sikatai kuandika maneno ambayo bwana Seth (Harbinder Seth- Mmiliki wa kampuni ya IPTL ya ufuaji wa umeme) ananituhumu nayo kwamba nimemkashifu , maneno hayo niliyaandika na kuyachapisha katika akaunti yangu ya X zamani Twitter, na maneno yale yanaakisi picha halisi na yenye ukweli wa jambo zima hili la IPTL"
"Pili maneno haya mimi niliyaongea kwa nia njema kabisa, ya kutaka kupata ufumbuzi wa sakata hili, na tatu, maneno yale niliyasema kwavile mimi nilibahatika kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyoshughulikia sakata la IPTL"
"Kama unakumbuka wakati ule maarufu lilivyojulikana kama sakata la Escrow, hivyo nilitumia fursa hiyo kuwaeleza Watanzania wenzangu ukweli wa jambo hili, kwasababu ninafahamu ukweli wa jambo hilo, na ni wajibu wangu kama raia kulinda rasilimali za taifa dhidi ya njama zozote zile za kupora rasilimali hizo kwa kisingizio cha uwekezaji".