Zitto Kabwe: Adui, Rafiki, Kipenzi

Zitto Kabwe: Adui, Rafiki, Kipenzi

Hiyo lugha ya kutaka kuchunguzwa,au mwenye ushahidi aulete, ni lugha ya kifisadi.
Zitto ajitokeze hadharani, aeleze mambo yote hadharani, aorodheshe mali na majumba yake, atueleze biashara alizofanya mpaka akamiliki mali na nyumba hizo na kodi alizolipa.
Vinginevyo akae kimya.
Mwigulu Nchemba, rafiki yake Zitto ametueleza hapo juu kuwa daima tutawaliwe na akili kubwa, kama yeye anavyotaliwa na akili kubwa ya Wakuu wa CCM.
Inaingia akilini?

Ashasema hana biashara yeyete nje au ndan ya nchi hii. Hapa dar anaishi nyumba ya kupanga kule tabata. Nadhan ya NHC/NSSF.

Kuhusu magari ya kifahari na majumba kama unavosema anamiliki, alishatoa fursa kwa walio na ushahidi. kwahiyo we mwenzetu kwakua una ushahidi, uweke hapa ili kukata mzizi wa fitna. Vinginevyo, ni muendelezo wa hekaya zile zile tulizozizoea.

Hadi asilia (Natural justice) Inasema you can be judge of your own case. Kwa maana kwamba Zitto hawezi kujichunguza mwenyewe. Kwa msingi huo ametoa fursa kwa vyombo na taasisi husika kufanya kazi yao...to avoid biase as it is inherent.

We leo unatwambia kuchunguzwa na chombo kingine ni kauli za kifisadi...are you serious?? Kwahyo Tibaijuka, chenge,.Ngereja na genge lao walipaswa kujichunguza wenyewe?

Je tungepata kujua ukweli hadi leo?

Think it again
 
Uhuru wa kutoa maoni unaruhusu watu waseme kwa uhuru juu ya viongozi wao.

Zitto is a public figure, na anafanya kazi za umma. Kuna watu watamsifu na kuna watu watamtoa kasoro.

Niambie kiongozi gani ambaye anasifiwa tu?
 
March ndio hii,afanye maamuzi magumu asepe,kuna vijana wengi wamekuwa groomed,zamani nilidhani ni charismatic leader,niligundua I was wrong,hana mvuto kumfikia Salim Mwalimu ama vijana wengine waliochipukia.Aende zake his time his over.Subiri bunge la 2016 uone vijana kibao watakaoingia kupitia CHADEMA watakavyowapandisha pressure wabunge wachache wa vyama vya upinzani wakati huo [ CCM,TLP na ACT]
 
Kiukweli Zitto ni mwanamapinduzi sikuwahi penda siasa huyu jamaa ndio kanifanya nipende siasa
 
Kuna kashfa inaenda na kujirudia kuwa Bwana Zitto Zuberi Kabwe (Mwanasiasa msafi kuliko wanasiasa wote kuwahi kutokea Tanzania) ni moja ya watu walionufaika na mgao wa fedha za escrow, japo sijawahi msikia akitamka kwa ulimi wake kuwa hajapokea, ameishia kusema watu wachunguze, nitaendelea kuamini katika misingi ya mtu ni huru mpaka pale itakapothibitika kua ana makosa.

Lakini kaka yangu huyu amekuwa ni mtaalamu mzuri wa matumizi ya "fallacy" kwa waliosoma falsafa wataelewa. Zinapozuka kashfa dhidi yake, huwa anatumia A kujibu swali B.

Tundu Lissu alipomkashifu kwa kupokea pesa toka kwa Mkono na mpaka sasa ana miliki magari mawili ya Mkono, Bwana Zitto aliishia kuhamishia kashfa kwa Mh. Mbowe, na kusema haongei na kifaranga yaani Lissu, hii kwenye falsafa inaitwa appeal to mockery ab absurdo lakini pia mbinu nyengine mheshimiwa hutumia ni Argumentum ad misericordiam au kwa lughanyepesi appeal to pity (inatafsiriwa kama kuweza kushinda mjadala kwa kuvuta hisia na huruma ya walio wengi) Ilipozuka kashfa kuwa bwana Zitto Kabwe kuna ufisadi anafanya kupitia kampuni ya Gombe advisors, Bwana Zitto alijibu ameumizwa sana kwa kuwa yupo busy anamuuguza mama ( Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema Peponi aamin) ilipoibuka tena bungeni kashfa ya kupokea hela za escrow alisema tumuache mama apumzike kwa amani.

Lakini kwa kuwa vifaranga vimekuwa, na hana anayemuuguza, tunaomba sasa atujibu kwa ufasaha kwa kuwa maelezo yake ya awali yalijaa na uuguzi, kuhusu mikataba wa leka Dutigite kwa upande mmoja na NSSF na TANAPA kwa upande mwengine

Kampuni ya Leka Dutigite ina wana hisa 16, 15 kati yao ni wasanii wa kizazi kipya wenye hisa asilimia 5 kila mmoja hivyo kuwa idadi ya asilimia 75 na asilimia 25 zilizobakia zinamilikiwa na Gombe advisors. Swali huyu Gombe ni nani?

Ukienda kuangalia makabrasha ya Brela Gombe advisors inamilikiwa na watu wawili, mtu mmoja mwenye jina la kikenya mwenye asilimia 25 na Bwana Zitto kabwe ambae kwenye fomu amejijaza kama mchumi badala ya kiongozi wa Umma

Kwa hiyo kumbe NSSF na TANAPA mashirika ya Umma ambayo yanakaguliwa yasifanye ufisadi na Bwana Zitto kabwe kwa mkono wa kulia, ukija mkono wa kushoto unakuta Bwana Zitto kabwe ndo mwanahisa mkuu kwenye mikataba ya kibiashara baina ya NSSF, TANAPA na leka dutigite, japo yeye anadai hakuna mgongano wa kimaslahi.

Katika tenda moja, NSSF iliilipa Leka Dutigite shilingi milioni 120, milioni 90 kati ya hizo zilitolewa siku moja baada ya kuwekwa, siku moja kabla ya uchaguzi wa kamati ya hesabu za mashirika ya umma PAC uliomfanya Bwana Zitto kuwa mwenyekiti wa kamati na kumng'oa mzee Cheyo aliyekuwa anafanya kazi kwa weledi mkubwa. Coincidence?

Na ni bahati nzuri kuwa hizo pesa zilienda kutolewa na Habib Mchange, (bank statement inaeleza hivyo) aliyefukuzwa Chadema kwa kosa la kuwa kibaraka wa Zitto na kupanga mapinduzi ndani ya Chama, leo ndio katibu mkuu wa LekaDutigite kampuni ambayo Zitto anasema hana maslahi humo, kwa nini aweke watu wake?

Sasa hapa kuna maswali yanajitokeza

1. Je NSSF na TANAPA ni mashirika ya Umma au hapana? Na je Zitto ni kiongozi wa Umma au Hapana?

2. Je Zitto anayakagua haya mashirika au hapana?

3. Je katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 sura ya 6 sehemu ya 2 Na sheria ya utumishi wa Umma inamruhusu kiongozi kama yeye kuingia mkataba na mashirika ya Umma ukiachila mbali mashirika yanayoripoti chini yake?

4. Kama Gombe advisors si kampuni ya faida, kwa nini ijimilikishe hisa asilimia 25% Za Leka Dutigite? Je si ingekuwa sahihi ingebaki kuwa mshauri tu na wasanii wakagawana asilimia 100 ya kampuni ili wanapogawana faida wagawane kwa uwiano sawa kutokana na mgawanyo wa hisa zao.

5. Kwanini aweke watu wake wa karibu kuwa ndio viongozi wa Leka Dutigite kama yeye ni mdhamini tu na mshauri wa wanamuziki?

Mimi naamini hakuna ujanja ujanja unaodumu kwa muda mrefu nchi hii kabla haujagundulika, Chama Chake kimeshamjua, ipo siku hao anaowatumia kwenye ujanja ujanja wake watamgeuke na ukweli utawekwa hadharani. lakini hadi hapo yatakoapotokea hayo, bado nasubiri siku nione Zitto Kabwe akiikosoa NSSF na TANAPA kwa kuwa mpaka sasa kila akiongea mifano mema hutolea mashirika haya mawili. Mimi ndio yule yule niliyemtabiria kufukuzwa kwenye chama siku aliyochaguliwa kuwa kiongozi wa chama

Yaani kwa matatizo yote ya akina Chenge na escrow na CCM bado akili zako zinakutuma umtaje au kumuongelea zitto!!

1. kwanza amekutawala, ndio maana at this point of time, umeingia kwenye kundi lile lile la wanaosema na hawasikilizwi jamii inakupuuza watakaokuunga mkono ni hao hao wachache

2. leta hizo document za Brela, pia useme ni wakati gani kiongozi wa umma anatakiwa kuwa na kampuni na wakati gani hatakiwi! na piga picha kubwa kwa watanzania wote, unaweza ukawa unazungumza kitu unaonekana mshamba; uongozi wa zitto ni wa kudumu??

3. nieleze kiburi cha zitto cha kuibua uchafu huo wote anaousema kila siku anautoa wapi?? ni swali ninalojiuliza kila siku

4. ulichosema unaonyesha zitto ana makosa, mbona wabunge, serikali, na wananchi wote wako kimya ( kunani?) hata maadui zake kisiasa wako kimya? na wewe thread yako itapita tu kama juzi ( dont you have an extra plan to at least go far than just writing???) unaonekana kituko na umeandika so innocently but so low! very low

tuanze kazi sasa, leta hizo document za Brela ukizipata ni PM

Then uliza kwa wataalamu wa sheria uhalali au usio uhalali unaweza ukawa unachekesha ( nimerudia hapa)

Huyu zitto anawasumbua sana
 
...............We leo unatwambia kuchunguzwa na chombo kingine ni kauli za kifisadi...are you serious?? Kwahyo Tibaijuka, chenge,.Ngereja na genge lao walipaswa kujichunguza wenyewe?

Je tungepata kujua ukweli hadi leo?

Think it again
Prof. Anna Tibaijuka, Chenge, Ngeleja na wenzao hawakutajwa wala kugunduliwa na hivyo "vyombo vya uchunguzi".
Walitajwana vyombo vya habari vyenye ujasiri.
Ndiyo maana mpaka sasa hivyo vyombo vya uchunguzi unavyovisema wewe na Zitto, havijagundua majina ya mafisadi wa Escrow kupitia Stanbik.
Think it again
 
Jakaya Mrisho Kikwete ni mtu mwenye roho nzuri sana. Lakini bwana huyu ni kiongozi mbaya sana - ana mapungufu mengi sana kiuongozi na kwahahikika hana sifa za uongozi. He lacks leadership charisma, talent, skills and qualities.

Zito Kabwe on the other hand, is the oposite of Mr Kikwete. He has leadership charisma, talent, skills and qualities - BUT he is not a good person perse'. Ana tamaa sana, ubinafsi uliopitiliza, umimi, masifa, majivuno na majigambo - sifa hizi zote (ambazo origin yake ni ukigoma) pamoja anapokuwa nazo mtu mmoja it is a leathal combination. Sifa mbaya za Zitto Kabwe zinafunika kabisa uwezo wake wa kiuongozi na ndizo zitakuja kusababisha anguko kuu la Bwana Zitto Kabwe. Mark my word!

Matatizo mengine ya Zitto

Ana pupa na papara zinazomfanya ashindwe kuelewa principal za msingi sana kwenye maisha. Principal hizo ni pamoja na ile ya Timming is everything.

Hakuna kitu muhimu kama kuelewa umuhimu wa timming especialy kwenye uongozi na siasa. Ukishindwa kuelewa hili always utakuwa unateleza kisha unaanguka. Nyerere aliwahi kujiuzulu uongozi na kumuachia Kawawa for a while ili kuweka mambo sawa - timming. Nyerere aling'atuka mwaka 1985 kwa hiyari yake kwakuelewa the essence of time.

Principal ingine ya msingi ni ukweli kuwa life is all about choices and decisions. Zitto ana tendance ya kufanya wrong choices at a right time au right choices at a wrong time - big mistake.

Katika uwanja wa polical calculations, Zitto amefeli and he will always fail because mapungufu yake ya kibinadamu yanafunika sana sana sifa zake za uongozi na kwakuwa yeye haambiliki na aamini kuwa anajua sana basi hakuna lingine la kufamnya bali kumuangalia anavyoanguka kama ajali ya train - train wreck. Ukiangalia sana matendo ya Zitto utagundua kuwa - anaamini kuwa yeye ana akili na uwezo mkubwa kiuongozi kuliko mtu yeyeto ndani ya Bunge, Chadema na Tanzania. Akiwa hajatimiza miaka 40 Zitto anaamini kuwa Tanzania nzima ni yeye tu ndio anafaa kuwa Rais na kwaongoza watanzania wengine wote - haamni vinginevyo. Pia anaamini kuwa Chadema nzima ni yeye tu ndio mwenye uwezo mkubwa kuliko kila mtu na hivyo anatakiwa kuongoza kila mtu. Kijana huyu ana upofu wa akili na maono.
 
The guy is talented...kwa anayoyafanya kwa tanzania ya sasa hakuna mwanasiasa wa upinzan anayewez kufanya....put evidence nasio siasa zile zile za kuzushiana....zitto ni mpiganaji na haitaji akili za ziada kujua hilo....ameifanyia mengi tanzania yetu...swala je hao unaowaabudu wameifanyia nin tanzania zaidi ya kuvuruga amani ya nchi....niwakat sasa wa kuamini mtu nasi chama tena....
 
Juliana Shonza,

Kuna wakati nilimuona Zitto kuwa ni kijana mwenye akili na mwenye mvuto kisiasa na nikajuwa yupo kwa ajili ya wananchi. Lakini baada ya sakata la Barrick na alipoanza kuelekezewa misaada jimboni kwake na Barrick na baada ya muda wa kuingizwa kwenye kamati ya madini na Kikwete akaanza kutembelea vogue, nikawa nna doubt nilivyomfikiria awali.

Juzi kuhusu suala la escrow na aliposhindwa kutetea hoja zake bungeni na mpaka alipoulizwa kuhusu na yeye kupokea fedha kutoka kwa Seth akajidai kujiliza bungeni na kusingizia kifo cha mama'ke, isitoshe, ile kukubali kila kilicho azimiwa awali na kamati yake kubadilishwa na nafasi yake kuchukuliwa bungeni na Anna Kilango, nikapata uhakika kabisa kuwa kijana ni bogus tena hafai kabisa na hana zaidi ya maslahi yake binafsi.

HAHAH HATA FaizaFoxy amemuonesha ZITTO kama adui. Adui wa kina FaizaFoxy.
 
Last edited by a moderator:
Ni mara nyingi sana huwa nawaambia vijana masikini wenye limited resources.Ni njia mbaya sana kutumia akiba ndogo kuwekeza ktk viwanja vya matajiri ili kujenga jina halafu baadae wategemee kupata dili.

Wengi sana huishia kupata mfadhaiko mkubwa ktk maisha.Kwani huw ani shida sana kukubalika na hao ktk makundi.

Vijana hao huwa hawajui sana kuwa matajiri walifika hapo kwa kuthamini hela ndogo.Na si wepesi sana kuwapa dili(kuwekeza mali) kwa wabadhirifu.

Huwa nawashauri sana vijana kuwekeza hicho kidogo ktk mradi fulani, na huo mradi aupiganie kwa juhudi kubwa sana.Juhudi,ubinifu uwajibikaji na mafanikio ndio yatamkutanisha na hao matajiri,na utamfikisha akiwa na heshima.

Atafika kwa matajiri kumuona kuwa mtu sahihi wa kuwekeza mali kwa usalama.Zitto kajilazimisha kuingia ktk kundi la waliofanikiwa bila kujifunza Vitu fulani ambavyo vingemsaidia sana kujitathmini km kweli amefikia na kustahili alipokuwa kasimama.
 
Mtoa post unatupotosha,aliyestukia dili.hakuwa Mbowe,alikuwa ni Christopher Ole Sendeka.Ndo alisimama na kupinga pendekezo wala sio Mbowe.Baada ya Sendeka kupinga ndo Zitto akasema akili.yake imechoka
 
Juzi wakati anahojiwa na vyombo vya habari kuhusu kufukuzwa kwake uanachama wa Chadema,pamoja na mambo mengine aliyoeleza pale,moja ni hili la kujigamba kwamba namnukuu;"kazi nnazofanya mimi(zitto) siwezi kulinganishwa na mbunge yeyote yule". Kwa mtazamo wangu finyu,hili ni tusi kwa wabunge wote! Yaani mh. Zitto anafanyakazi zaidi kuliko wote!? Haya ni majigambo yaliyopitiliza.

Kuna mbunge mmoja nilikuwa naongea nae jana ambae pia ni mjumbe wa PAC anasema,zitto inahitaji roho ya chuma kumvumilia ni mtu ambae kila kitu anachofikiria yeye anataka kiwe hivyo. Me namshauri zitto,kwa vile Kitila Mkumbo kitaaluma ni mwanasaikolojia na ni rafiki yake ampe tiba ya tatizo hilo la kujiona yeye ni bora kuliko wengine. Nawasilisha!
 
Last edited by a moderator:
Mmeshamfukuza mbona bado mnaendelea kufuatilia mwacheni aendelee na maisha yake au ndo mwendelezo wa siasa za maji taka
 
Ana matatizo sana yule jamaa, sijui labda tutumie msemo wa wahenga, Akikua ataacha" Lakini ashakua tayari 39yrs si mchezo labda na useja ndio unamsumbua. Unajua umri huo kutokuwa na mke ni mapungufu makubwa sana katika kujitambua. Ebu tumuache maana wakati ukuta.
 
zitto ni adui wa wasaka tonge wa upinzani

Mimi kma mwananchi wa kawaida naona mchango wake
Hata mimi nilimpenda ila kwa sasa nasema mapema mno kuona anafaa.Kirago alicho kitupa jirani yako usikalie kwanza lazima UKIKUNGUTE
 
Back
Top Bottom