Sielewi nini hasa mantiki yako mkuu,.siamini kama ni kweli umekaa na kutafakari kwa mda mpaka kufikia kuandika uzi huu au kwa sababu ya chuki zako tu umeamua kuandka. Kaka mimi sio shabiki wa Zitto bali mimi naamini katika umuhimu wa upinzani katika maendeleo ya nchi. Alichosema Zitto juzi ilikua UPINZANI kuwa na nguvu na kuondoa mfumo dhalimu wa chama tawala, UKAWA wamekaa wakasema hawamkaribishi Zitto kwao, ACT bado ni wapinzani, UKAWA bado ni wapinzani, Alichosema Zitto leo ni kuwa pamoja na kutokukaribishwa UKAWA bado chama chake kitaendelea kusimama kama miongoni mwa vyama vya upinzani. Sasa hapo kakosa nini? Jamani MNYONGE MNYONGENI, HAKI YAKE MPENI, Kuna wakati chuki zetu binafsi zinatufanya kutokuangalia katika ukweli na haki.