Zitto ameweka msimamo wake kuwa hawez jiunga na ukawa na kwamba anawashangaa wanatafuta mgombea humo ndani hadi leo kwani anatoka mbinguni! Kaka yuko vizuri hajabadili msimamo wake tangu atoke bungeni. Zitto katika ubora wake. Go go brother....
Jmaa karushiwa mbuchuchu na ccm akaiokota, sasa hajielewi .
Mh. jamaa kituko tupu, ................ Anasikitisha sana.
Ni ITV habari leo alipokuwa akiongea na watiania wa nafasi mbalimbali wa chama chake.Aliwahi sema pia ACT iko tayari.So?
Sielewi nini hasa mantiki yako mkuu,.siamini kama ni kweli umekaa na kutafakari kwa mda mpaka kufikia kuandika uzi huu au kwa sababu ya chuki zako tu umeamua kuandka. Kaka mimi sio shabiki wa Zitto bali mimi naamini katika umuhimu wa upinzani katika maendeleo ya nchi. Alichosema Zitto juzi ilikua UPINZANI kuwa na nguvu na kuondoa mfumo dhalimu wa chama tawala, UKAWA wamekaa wakasema hawamkaribishi Zitto kwao, ACT bado ni wapinzani, UKAWA bado ni wapinzani, Alichosema Zitto leo ni kuwa pamoja na kutokukaribishwa UKAWA bado chama chake kitaendelea kusimama kama miongoni mwa vyama vya upinzani. Sasa hapo kakosa nini? Jamani MNYONGE MNYONGENI, HAKI YAKE MPENI, Kuna wakati chuki zetu binafsi zinatufanya kutokuangalia katika ukweli na haki.
Ile barua aliwaandikia ukawa kuomba kujiunga nayo anaikumbuka?
Amani iwe kwenu wana ukumbi:
Mkuu wa chama cha ACT wazalendo Zitto Kabwe amesema hawana mpango wa kujiunga na ukawa kwa kuwa chama chake kina sera tofauti.
Ameyasema hayo leo ndani ya kikao chao cha ndani na kusisitiza kuwa azimio lao la Tabora linamtaka kila mtu kutangaza mali na madeni yake ndo ajiunge naye.
Chanzo ITV taarifa ya habari ya saa 2 usiku.
mbona ACT waliandika barua kwenda kwa vyama vinavyounda ukawa wakitaka kujiunga lakini walikataliwa, leo eti huyu kinyonga anasema hawataki kujiunga ukawa. AIBU ZAO BAADA YA KUPIGWA STOP.
KAMA KUNA MTU ANAMWAMINI ZITTO KABWE HUYO LAZIMA AATAKUWA NA MATATIZO YA AKILI