Zitto Kabwe: ACT- Wazalendo, hatutajiunga na UKAWA

Zitto Kabwe: ACT- Wazalendo, hatutajiunga na UKAWA

Amani iwe kwenu wana ukumbi:

Mkuu wa chama cha ACT wazalendo Zitto Kabwe amesema hawana mpango wa kujiunga na ukawa kwa kuwa chama chake kina sera tofauti.

Ameyasema hayo leo ndani ya kikao chao cha ndani na kusisitiza kuwa azimio lao la Tabora linamtaka kila mtu kutangaza mali na madeni yake ndo ajiunge naye.

Chanzo ITV taarifa ya habari ya saa 2 usiku.
 
Hakiongea na wanachama wenzake wa ACT-Wazalendo,kiongozi mkuu wa huyo Bw.ZZK amedai kwamba ACT haiwezi kujiunga na UKAWA kutokana na tofauti za kifalsafa baina ya ACT na UKAWA,pia akinukuu azimio la Tabora ambalo linamtaka mwanachama wa ACT kutamka Mali,Madeni na Maslahi binafsi kitu ambacho amedai UKAWA akipo.

Swali: Hivi ni nani alianza kumkataa mwezake asijiunge naye?ni ACT au UKAWA?
Au ndiyo kale kamsemo ka wahenga kanachosema "SIZITAKI MBICHI HIZI" kanajidhihirisha kwenye kauli hiyo ya ZZK?

Source: ITV Habari!
 
Zitto kabwe kiongozi mkuu wa act ,hatuko tayari kuungana na ukawa,hayo yamesemwa na kiongozi mkuu wa act zito kabwe leo akiwa anaongea na wanachama wa act jijini dar es salam.
Mm kama mwana chama wa act kiongozi wangu ananichanganya sana miezi miwili iliyopita kiongozi wangu wa act alinukuliwa na redio dw ya ujerumani akisema act wako tayari kujiunga na ukawa,kulikoni tena leo kiongozi wangu amebalika?
 
kila kitu kinamwisho wake...na huu ndo mwisho wa dogo/kaka yetu zitto...tumpe pole.
 
Zitto mpaka anaboa na hilo azimio lake la Tabora. Kila mahali yeye analitaja tu. Kwani mtu akishataja mali na madeni yake automatically anakuwa kabatizwa na kuachana na ufisadi wake!?

Yani huyu jamaa kaishiwa sera kabisa nafsi yake inamsuta. Ninachokifahamu mimi ni kwamba Ukawa hawawezi kumkaribisha Zitto kutokana na uhaini alio ufanya Chadema.
 
Wakuu JF,

Amani iwe Nanyi.
Ninajaribu kuoanisha kauli za Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo Ndugu Zitto Kabwe za Juzi na Leo.

Juzi alikaririwa kwenye Mitandao ya Kijamii akibashiri Mapinduzi Makubwa katika Siasa za Upinzani Tanzania,alienda Mbali zaidi na Ku refer Kilichotokea Kenya,2002 Pale Chama cha KANU kili0ong'olewa na Muungano wa Vyama vya Upinzani chini ya Mwai Kibaki.

Leo baada tu ya Mkutano wa UKAWA kuahirishwa the same Zitto anakuja kutoa tamko kuwa ACT itasimama kama yenyewe na haitajiunga na UKAWA.

Maswali

1. Kauli ya juzi kuwa tutashuhudia Mabadiliko Makubwa kwenye Siasa za Upinzani Kesho Jumatatu 27/7/2015 na kufananisha na Kenya 2002 ilikuwa na Maana gani hasa ?

2. Ni nani hasa aliyeihitaji ACT UKAWA Mpaka leo Kiongozi wao aseme hawana Mpango wa kwenda UKAWA.

2. Ni lini ameanza kuwa Msemaji wa Vyama vya Upinzani ?

3. He,tukisema kuwa ni Opportunist aliyekuwa ana expect leo Lowasa Kutangaza kuhamia upinzani/UKAWA na yeye kualikwa UKAWA tutakuwa tumekosea ?,Kuwa ameona Opportunity imeota Mbawa ?
 
Yani huyu jamaa kaishiwa sera kabisa nafsi yake inamsuta. Ninachokifahamu mimi ni kwamba Ukawa hawawezi kumkaribisha Zitto kutokana na uhaini alio ufanya Chadema.

Anakaribia kuwa chizi. Wabunge 50 aliotegemea wamepima upepo wakaona hamna namna ya wao kujiunga nae. Kaambulia wanne tu, ambao hata hivyo hawatishi.
 
Amechoka kweli asee ameshindwa hata kunyoa ndevu? Midevu kibao imemjaa pyee
 
Ww unashindana na wanasiasa kina Zitto watakupasua kichwa nakushauri nenda kafanye shughuli za maendeleo
 
Mala chama changu kipo tayari kushirikiana na ukawa mala siwezi kuungana na ukawa,,sasa tumueleweje huyu mtu?? Kwa heri zitto
 
Anakaribia kuwa chizi. Wabunge 50 aliotegemea wamepima upepo wakaona hamna namna ya wao kujiunga nae. Kaambulia wanne tu, ambao hata hivyo hawatishi.

Chama chake kinasubiri wabunge reject ambao si washambuliaji, Chadema wanasajili viungo wakabaji na washambuliaji wa bei mbaya!
 
Back
Top Bottom