Zitto Kabwe: ACT- Wazalendo, hatutajiunga na UKAWA

Zitto Kabwe: ACT- Wazalendo, hatutajiunga na UKAWA

Anachohitaji Zitto hivi sasa ni kutafakari kikamilifumwelekeo wake kisiasa - kama bado anaamini ana mustakabali (future) katika fanihiyo baada ya mwanga (spotlight) wa enzi za Buzwagi kuanza kufifia. Hizi dhanaza rejareja anazohangaika nazo leo hii hazina maana wala umuhimu kwake yeye nataifa kwa ujumla. Hakuna falsafa wala itikadi mpya anayoileta zaidi yakuonekana kama mtu anayehaha kushindana au kupambana na wale anaowaona maaduizake binafsi katika ulimwengu wa siasa (defensive mindset).

Prof. Shivji amewasilisha maswali ya msingi. Azimio la Arusha haliendani kabisana mfumo wa kiuchumi na kijamii tulio nao wakati huu.
Hata hayomaadili anayodai yako katika Azimio la Tabora si ainisho kamili la maadilikatika mfumo tulio nalo sasa. Yeye kashikilia kipengele cha "viongozikutangaza mali". Hiyo sio falsafa wala itikadi; ni sehemu ya utaratibutu (procedure) wa udhibiti na ufuatiliaji wa mienendo ya viongozi katikakigezo cha wizi wa mali za umma na ufisadi.

Hata katika mifumo inayoongozwa na falsafa/itikadi za kibepari wanazo taratibuza kuhakikisha kwamba wenye dhamana ya dola hawatumii nafasi zao kuhujumuuchumi wa taifa kwa wizi na rushwa. Hakuna falsafa/itikadi inayoshabikia wiziwa mali za umma. Tatizo la wizi/ufisadi hapa kwetu si la kifalsafa walakiitikadi. Ni tatizo la kukosa uongozi wa kweli (tumefilisika kiuongozi). Kwamfumo tulio nao, hata viongozi wa Serikali na vyama wakitangaza mali zao leohii bado wataendelea kutuibia bila hatua kuchukuliwa.

 
Mara zote mimi huamini katika umoja na si katika utengano, pia naamini katika dhamira kuwa kila mmoja wetu ana umuhimu wake.

Inawezekana sana katika maslahi ya kisiasa kuwepo misigano lakini ikiwa adui ni mmoja tofauti hupaswa ziwekwe pembeni ili dhumuni lifikiwe.

Kushutumiana na kuapizana ama kudharauliana huondosha kuaminiana na upendo.

Hayo yanapotimia baadhi yetu husema "huyu si mwenzetu hatuwezi kwenda nae" inasahaulika kwamba huyohuyo anaweza kuwa na msaada japo mdogo katika safari.

Ningelipenda kusema neno hili "SIASA ZA VISIRANI NA VISASI ZIMEPITWA NA WAKATI"

BAADA YA KUSEMA HAYO NINGELIPENDA KUMUOMBA MH. ZK AFUTE KAULI ZAKE, NA PIA WAHESHIMIWA VIONGOZI WA UKAWA WAKUBALI KUKAA MEZA MOJA NA ACT WAZALENDO AU YEYOTE AWAE AJIUNGE UKAWA ILI KUFIKIA LENGO HUSIKA.

Kinyume na hilo usemi "wagawe uwatawale" utapata nguvu na mwisho wa siku tutatoleana macho na kulaumiana.

Katika safari hii kila mmoja wetu anahitajika. hii ni sawa na vita kila aina ya silaha inahitajika, kila tutakachokidharau yawezekana ndicho kingelikuwa msaada. Sote tunategemeana iwe iwavyo.

Maneno haya hayapendezi machoni pa wengi wetu, ila ndio ukweli nisiopaswa kuuficha.

wakatabahu,

M.
 
Hongera. .mawazo yako ni sahihi kabisa. Lakini Ikumbukwe kuwa April mwaka huu ACT iliandika barua kwa Umoja huo kuomba kujiunga lakini haikujibiwa. Badala yake chama kimoja wapo kikavaa koti ya Umoja huo kukataa ACT. Hatujui Waliogopa miiko ya uongozi au walijua ingekuwa ngumu wazalendo kukubali kula matapishi. Mimi kama mwanachama ninaungana na kiongozi mkuu kauli aliyoitoa ilikuwa ya kijasri . Hatuwezi kuungana sasa kwa sababu misingi ya vyama vyote vya ukawa imenajisiwaa. Huwezi kusema leo ni fisadi kesho akawa kamanda. Bila kuomba msamaha kwa wananchi kwa kuwadanganya. Hivyo basi ni imani yangu chama changu hakitaingiwa na tamaa ya dola kiasi cha kuinajisi miiko ya uongozi na Azimio la Tabora. Twende wenyewe tukalihubiri Azimio la Tabora. Watanzania wasipotuelewa leo watatuelewa kesho. ...
 
Kiongoz wa act zitto kabwe amesema hayo ktk mahojiano radio DW.
Ameongeza kuwa waliandika barua tar 26 aprl ya kuomba utaratib wa kujiunga ukawa lkn hawajajibiw..... Hivyo wakaamua kujisimamia wenyewe....
Ni vyema kama vyama vya siasa vinaendana malengo kuungana.... Lkn sisi tuna malengo ya kumkomboa mtanzania.
 
Huyo anatapatapa tu baada ya kunyimwa nafasi UKAWA. Sisi hatutaki wasaliti na matapeli UKAWA. Huyo naye alikuwa anajaribu kupiga deal Lowassa ahamie ACT akachemka kwa kuwa chama chace ni kichanga. Kwenda ACT ambayo mpk sasa haina hata wagombea nchi nzima ni risky business. Lowassa aliwashitukia. So, Zitto Kabwe asianze kutapeli watu. Upo ushahidi wa dhahiri kuhusu yeye kupiga jaramba ili Lowassa ahamie ACT lkn alishindwa.

Afterall, lengo kuu la chama chochote cha siasa ni kushika dola. Huwezi ukaleta mabadiliko yoyote ya kimfumo bila kushika dola. Tatizo lao wao walikuwa wanashindana na zaidi na CHADEma badala ya kushindana na CCM ambacho ndicho chama tawala. Sasa nguvu ya CHADEMA+UKAWA+Lowassa imewamaliza kisiasa. Sasa wanaweweseka
 
Back
Top Bottom