Zitto nilikuamini sana kipindi cha nyumalakini kwa sasa sikusomi kaka, Unajipinga mwenyewe kauli zako,
Kwa haswa swala la UKaWA, kwanza Mwenyekiti wako alitangaza mwana ACT yeyote atakae shabikia UKAWa atachukuliwa hatu, Ukaja wewe ukatangaza kuutaka umoja huo na kuandika Barua ya Kujiunga na ukatoa shutuma kwa Chadema kuwa hawakutaki, ila ukasema wakikubali hata leo unajiunga na kutamka wazi hakuna mtu asiye utaka umoja,
Leo unakuja na tamko jingine, ACT haita jiunga na UKAWA eti vyama vingine havina Sera nzuri kama ACT, kwanza kina azimio la Tabora, Je mwanzo ulipo andika barua haukuliona hilo? na je wangekukubalia ungejitoa? Zitto kwanini usiwe unafikiria kabla ya kutenda?
Swali jingine kwa Zitto, Je kama wewe ni Mkuu wa chama, kuna uchaguzi wowote ulifanyika kukuchagua? na kama hakuna utaratibu huo, wewe ni kiongozi wa Chama mpaka kufa kwako? na kama ni hivyo, nikikuita wewe ni mroho wa madaraka nitakuwa nafanya makosa?
Zitto hiki Chama kweli ni cha Watanzania? na akama cha Watanzania, kwanini ulitangaza kushinda majimbo yote ya kigoma na sii Mbeya? na ukijua wewe ni mwanakigoma? unamaanisha hiki chama ni cha watu wa kigoma? kwahiyo uanataka kutuambia kila atakae kuwa na uwezo wa kuanzisha chama akipeleke kwao? huoni kuwa kila kabila litakuwa na Chama chake? na hauoni ukabila na ukwetu utaanzia hapo?
Sawa kaka unajenga chama chako ila jaribu kujielewa na kuelewa kile unafanya
yangu ni hayo tu