Zitto Kabwe achunguzwa kuvuna PAP

Zitto Kabwe achunguzwa kuvuna PAP

visa vya chdm kwa zito haavitaisha labda wachaga waishe dunian,wizi wa mbowe na slaa mmekaa kimya wachaga bana

Ukabira naona umekukalia kooni, dunia ya leo unaongelea ukabira? Pole sana
 
Na wale wote wanufaika wa Stanbic wachunguzwe lakini pia wakiwa nje. Tuache Double Standard

Bila kutajiwa majina ya wale wote waliopewa pesa na Singasinga pale Stanbic, wakati mkataba wa serikali na PAP ulisema pesa hizo zingepelekwa UBL Bank of Tanzania, suala lote la Escrow litakuwa halijapatiwa tiba ya kweli. Licha ya uongo wa wazi uliosemwa na Kikwete eti pesa zile hazikutolewa kwenye lumbesa na mifuko ya rambo, ukweli ni kuwa pesa hizo zililipwa kinyume cha mkataba na sheria ya nchi na hivyo Gavana Ndulu lazima awajibike kama alivyo Kikwete aliyeamuru pesa hizo zitolewe kwenye akaunti ya Escrow.
 
Uko sawa mkuu, sasa hao akina Lisu, sugu na Lema umewatendea haki kuwa ingiza ktk com zako hapo juu? Siyo kuwaonea kweli? Ebu tuwe wakweli

Hawa walisema watamtoa Muhongo kwa nguvu wakijua hakuwa kapata hata sent ya PAP/VIP kisa tu "uwajibikaji", sasa nyani mzee huyu hapa wamemgwaya, au ni mwenzao? inamaana cdm hawapaswi kuwajibika? kamon acheni ujuha. atoke.
 
Ninachofahamu fika ni kuwa wahalifu waliungana kumkomoa Muhongo. Wapo waliomchukia Muhongo kutokana na kuwazibia ulaji (Mkono et al), wapo waliomchukia Muhongo kwa kuwazuia wasihodhi utajiri wa mali asilia ambayo ni kwa manufaa ya wote (Mengi et al), wapo waliotaka kumkomoa Muhongo kwa kuwaeleza ukweli wao juu ya uwezo na uelewa wao mdogo kuhusu sekta ya madini na gas (Zito, Olesendeka et al.), na pia wapo waliofanya kazi ya kumwondoa Muhongo katika nafasi yake ili biashara zao ziweze kuendelea vizuri (Zito, Olesendeka et al.), wapo waliofanya kazi ya kumwondoa Muhongo kwaajili ya faida za kisiasa (wengi wa wabunge wa upinzani), wapo waliofanya kwa nia ya kumkomoa Kikwete (baadhi ya wabunge wa CCM), na wapo waliofanya jitihada ya kumwondoa Muhongo ili wapate nafasi za uwaziri (Filikunjombe et al.), mwisho kabisa tupo tulioshabikia bila kuwa na msingi wowote ule.

Ukiona una nchi ambayo waovu wanaweza kuungana kutimiza malengo yao na wakafanikiwa kuwa na viongozi wanaowataka, kuwaondoa viongozi wasiowataka; na umma ukachezeshwa mchakamchaka kuunga mkono matakwa binafsi ya waovu, Taifa la namna hiyo lipo kwenye hatari ya kushindwa kabisa kulinda maslahi ya walio wengi, na watu wengi hawawezi kuwa tumaini la uhakika kuwa siku moja maslahi yao yatakuwa mbele kuliko ya watu wachache.

Hela yoyote ambayo inatolewa kwa Mwenyekiti wa PAC au mjumbe kutoka Mashirika ya umma, inatafsiriwa kuwa ni rushwa mpaka pale kutakapotolewa maelezo ya kina kwa nini hiyo pesa ilitolewa, na je Zito ali-declaire kuwa amepokea hela kutoka kwenye taasisi ambayo anaisimamia? La sivyo, bila shaka yoyote Zito na taasisi iliyotoa, wote wana hatia.
 
Hawa walisema watamtoa Muhongo kwa nguvu wakijua hakuwa kapata hata sent ya PAP/VIP kisa tu "uwajibikaji", sasa nyani mzee huyu hapa wamemgwaya, au ni mwenzao? inamaana cdm hawapaswi kuwajibika? kamon acheni ujuha. atoke.

Ok, hujaridhika kuwa Sugu, lisu na lema wameitendea haki nafasi zao kama wabunge kwa jamii? Nini wajibu wa mbunge? Au kwako wewe mbunge bora ni yupi?
 
Ni lazima achunguzwe kwani amepokea fedha kutoka kwa Mkono aliyejipatia zaidi ya shilingi bilioni 64 rudia bilioni 64 kutoka Tanesco kama wakili wake. Alipokuwa Musoma wakati wa likizo ya Krismasi alisema hataacha kuiandama serikali pale tu atakaporudishiwa "duka lake" (Tanesco). Amemtumia Kafulila na Zitto kuendesha kampeni ya Escrow kwa matumaini kuwa atarudishiwa duka lake.
Kumchunguza Zitto si tu kwa kashifa hii bali pia kwa kujipatia fedha kutoka mashirika mbalimbali ya umma ni muhimu. Kijana huyu ni janga la kitaifa.
 
Ni lazima achunguzwe kwani amepokea fedha kutoka kwa Mkono aliyejipatia zaidi ya shilingi bilioni 64 rudia bilioni 64 kutoka Tanesco kama wakili wake. Alipokuwa Musoma wakati wa likizo ya Krismasi alisema hataacha kuiandama serikali pale tu atakaporudishiwa "duka lake" (Tanesco). Amemtumia Kafulila na Zitto kuendesha kampeni ya Escrow kwa matumaini kuwa atarudishiwa duka lake.
Kumchunguza Zitto si tu kwa kashifa hii bali pia kwa kujipatia fedha kutoka mashirika mbalimbali ya umma ni muhimu. Kijana huyu ni janga la kitaifa.
Kwa kweli mla rushwa siyo mtu wa kuhurumiamia hata kidogo.
 
Serikali hii utafikiri kichwa cha mwendawazimu.
Hawa PCCB wanaojianya wanachunguza wanashindwaje kuchunguza na kubaini wakina nani walichuka ela Mabilioni ya pesa kwenye Lumbesa pale Stanbic bak.?Ni uchizi husio na kifani. Unaacha kuchunguza watu waliokwapua a lot of billions through Stanbic unaanza kukimbizana na hawa watu waliochukua sijui vimilioni kumi sijui tano.Hii ni akili au matope.

Kwa hiyo kwa ushauri wako rushwa ni ile tu ya mabilioni, chini ya hapo tukenue meno.....hii busara yako pia ni tope.
 
asipoachia ngazi tutaenda kumtoa kwa nguzu bungeni, tumeshaanza kuhamasishana na kufikia jmosi haja ng'oka tutaanza kupanda mabasi kuelekea dodoma tayari kwa kazi ya kumng'oa asijifanye kotapini. tundu lissu lema na sugu kama mtamshindwa basi tegemeeni mshikemshike wiki ijayo, hakianani dodoma haitakalika.

Naunga mkono hoja.
 
Serikali hii utafikiri kichwa cha mwendawazimu.
Hawa PCCB wanaojianya wanachunguza wanashindwaje kuchunguza na kubaini wakina nani walichuka ela Mabilioni ya pesa kwenye Lumbesa pale Stanbic bak.?Ni uchizi husio na kifani. Unaacha kuchunguza watu waliokwapua a lot of billions through Stanbic unaanza kukimbizana na hawa watu waliochukua sijui vimilioni kumi sijui tano.Hii ni akili au matope.

Acha uchiz Mwizi ni mwizi tu
 
mbona muhongo hajachukua hata senti tano katimliwa iweje yeye aliyekomba milioni kumi aachwe? tutaandamana kwenda dodoma labda awe analala bungeni

Point sisi tumeshaanza kujipanga hapa Dodoma, tunasubiri hilo amshaamsha
 
asipoachia ngazi tutaenda kumtoa kwa nguzu bungeni, tumeshaanza kuhamasishana na kufikia jmosi haja ng'oka tutaanza kupanda mabasi kuelekea dodoma tayari kwa kazi ya kumng'oa asijifanye kotapini. tundu lissu lema na sugu kama mtamshindwa basi tegemeeni mshikemshike wiki ijayo, hakianani dodoma haitakalika.

Wala huhitaji kuingia hiyo gharama, ni kuongea tu na Mbowe hiyo kazi atampa Lema....yule msela wa Arachuga anarusha tofali balaa....Zito atatolewa na machela.
 
Hii hoja mbona ilikuwepo hum kitambo, na zitto akwishasema kuwa wachunguze na IKITHIBITIKA ATAWAJIBIKA?? Nnachokiona ni cdm na wafuasi wa mlengo wa kushoto, ndyo wanaompiga zitto..

Kumbuka hzo ni propaganda za kisiasa na kwa zitto kafisha za hvyo zipo nyingi sana na hakikika amezikwepa zote....
 
mbona muhongo hajachukua hata senti tano katimliwa iweje yeye aliyekomba milioni kumi aachwe? tutaandamana kwenda dodoma labda awe analala bungeni

Na wewe nunda kweli umerudi tena jukwaa hili? Nilishakufahamisha jukwaa linalokuhusu jf. Sasa kama mna roho fungulieni majina ya mgao kwa waliolipwa stanbic umwone unaemtetea alichotewa kiasi gani. Wewe na genge lenu bado mnaamini akili za watanzaniq ni zile zile za miaka ya uhuru. Si muda mrefu nacho kisima cha Lumumba kitakauka.
 
Kwani Muhongo mliyemshinikiza ajiuzulu amefanya ufisadi gani?

Mbaya zaidi wameshinikiza na kupotosha uma, akawakoroga na kina Kigwangala nao wakamdhalilisha Prof bila sababu yoyote...so sad.
 
Wakati wa mjadala wa sakata la ESCROW bungeni hili swala liliibuliwa na Nchambi pamoja na Lusinde, wakadai wana nyaraka. Lakini wakati Zitto akijibu hoja nakumbuka aliweka commitment yake swala lipelekwe kamati ya maadili ya bunge na yeye yupo tayari kuwajibika ikiwamo kujiuzuru ubunge wake ikiwa itathibitika ni kweli.

Kwangu nilijua kwa kuwa jambo lile liliibukia bungeni tena baina ya wabunge kutuhumiana nikajua commitment ya Zitto ni suluhu mujarabu ili ukweli ufahamike. Sasa kama wale ndugu Nchambi na Lusinde waliibua hili na kudai wana nyaraka kwa nini wasingekubaliana na Zitto na kuweka commitment zao kama mwenzao? Na kwa nini Spika alilikalia kimya pasipo ufafanuzi wowote? maana hizi zilikuwa ni tuhuma dhidi ya mwenyekiti ambaye kamati yake imeshiriki uchunguzi uliokuwa unajadiliwa.

Mkuu, wahusika wote hao ni CCM? inawezekana akina Lusinde walihongwa na hivyo hawakupeleka nyaraka au walipeleka lakini spika akahongwa ili azikalie kimya.
 
Back
Top Bottom