Ujumbe umeeleweka lakini napingana na mtoa hoja sidhani kama issue ya kuwa kiongozi au mwenyekiti wa taasisi lazima uwe tajiri kwa hili sikubaliani naye hata kidogo. Inawezekana anamfaham Zitto kama alivyosema na sikatai kwa kuwa simfahamu zaidi ya kumuona bungeni au akijadiliwa hoja na tabia zake kama hivi jamvini. Unaweza ukawa sahihi katika hoja yako lakini si ki vile kama ulivyosema kuwa alitolewa Kigoma kwa hiyo atachekwa kwangu mimi hayo bwana Kamundu umeenda mbali zaidi ya kinachotakiwa kujadiliwa katika hii mada yako. Labda niulize nini malengo ya mada yako kumbomoa au kumjenga bwana Zitto? Kama vijana inabidi tuelimishane na kuelewa tunachotakiwa kukifanya. Ni kweli katika hatua za mwanzo kama hizi hatuwezi kuwa sahihi kwa kila kitu ndiyo maana tunahitaji mawazo chanya ya wazee na si kwamba hatuwezi fanya kitu kwa kuwa hatuna utajiri sikubaliani na wewe katika hili. Simtetei Zitto kwani amekosea kama mwanachama na kiongozi wa juu katika chama lakini si mtazamo wa chama kama CHADEMA kuwa lazima uwe tajir ndiyo uwe kiongozi au mwenyekiti, la hasha!!!!