chama makini ni kile kinachowachukulia watu hatua bila kujali wadhifa, rangi au tabaka, na CHADEMA imekua makini katika kutekeleza hayo ispokua tu inapofika kwa Zitto. Je ni kweli kuwa hufahamu ni jinsi gani Zitto amekua akifanya mambo yake kinyume kabisa na misingi ya chama. Sasa kama chama kikianza kuwa na matabaka hasa katika kuchukua maamuzi hatutakua tofauti na CCM waliowafunga kima Farijala Hussein na kuwaacha KAGODA, au wanaposhinwa kuwashughulikia magamba aka mapacha watatu. Huoni kuwa misingi ya chama hapo itaanza kuwa ya kiupendeleo? hasa pale viongozi wa chini wanapowajibiswa kwa adhabu kali kali ikiwemo kufukuzwa uanachama, lakini huyu bwana haguswi? yeye ni nani?
kwa misingi hii ntarudisha kadi
Baadhi yenu mnaijua CDM hivi karibuni, moja wa wabunge wa kwanza ni kutoka mkoa wa Kigoma, Mheshimiwa Dr Warid Kabour kupitia CDM. wakati hua NCCR na CUF vinatesa sana, wakati huo Watanzania hawaaamini upinzani, lakini wananchi wa Kigoma waliamini upinzani na kukipa kura, mwenyekiti wakati huo akiwa mwasisi wa chama mzee mtei. CDM ikifanya kosa kumfukuza zito uchaguzi ujao 2015 CCM haina mpinzani. kumbuka watu wa Kigoma walimwamini zito akiwa mdogo sana na kumtuma kuwakilisha jimbo. Zito, Dr Slaa na Mheshimiwa Mbowe wamekifikisha chama hapo kilipo.
Mchango wa zito ni mkubwa kukifanya CDM kiwe chama chenye wafuasi wengi na kionekane chama pekee chenye kuweza kuwatoa watanzania kwenye lindi la umasikini. kumbuka hoja za ZITO kama buzwagi na misimamo yake bungeni vimesababisha CDM iaminike zaidi kwa wananchi. iwapo Zito atafukuzwa ataondoka na wafuasi wengi sana hasa wale wanaoona kama CDM ni chama cha kikanda, kumbuka Zito ana siri nyingi za CDM pia.
Kama Zito amekosea chama kikae nae na kimrekebishe ili chama kisonge mbele, ili chama kiwe makini ni lazima kikubali mawazo mbadala kwaani kila mtu ana mtazamo na fikra tofauti. CDM kikianza kufukuzana basi utakuwa mwanzo wa kujichimbia kaburi. Kumbukeni kuwa zito ni muisilam kutoka kanda tofauti na kanda ya kaskazini hivyo kuwepo kwake inasaidia kuondoa hoja ya kuwa CDM ni chama cha udini,chama cha ukabila na nk.
CDM ni chama cha demokrasia kama jina lake lilivyo, hivyo demokrasia ni pamoja na kuvumiliana kwa kukubali mawazo ya watu tofauti, hii ndiyo demokrasia ya kweli. Ni kweli yawezekana zito anataka kugombea urais lakini wamwache demokrasia itafanya kazi yake, wengi tunajua kuwa ukiwaweka zito na Dr Slaa mbele ya wananchama Dr Slaa atapita. Nafikiri zito anajua kuwa lengo lake siyo 2015, najua ni zaidi ya hapo hasa miaka ijayo.
Pia wananchi wa mkoa wa Kigoma ni wapinzani wa kweli dhidi ya CCM kumbuka katika uchaguzi wa 2010 kama si njama za CCM mkoa wote wa Kigoma ungekuwa CDM NA NCCR mageuzi. Kwa sasa NCCR mageuzi hawakiamini hasa baada ya James Mbatia kuteuliwa na Kikwete kuwa mbunge hivyo kwa sasa NCCR kinaonekana kama tawi la CCM. Hongera Mheshimiwa Mbowe kwa kutumia busara.