Ukinionesha tusi moja nitaomba samahani, vinginevyo lugha za kupamba wakati mapungufu na uhamna/emptiness ni mkubwa. Kama planning authorities ni Halmshauri je wewe wizara unafanya nini??? mimi ninaongelea kuweka sera na sheria za nchi zinazompatia kila mtanzania nafasi ya kupata fursa ya kuwa na kiwanja na hivyo makazi bora. Nchi ni yetu ardhi ni yetu kwa nini iwe aghali kwa mtanzania??? almost 95% hawawezi kununua ardhi/kiwanja-kama 80% wako vijijini hiyo 15% wako mjini na ni wapangaji wa kudumu. Labda 5% tu ndo nyinyi wenye majengo makubwa kama mahekalu. Waliojenga wengi mafisadi na wezi wa mali za umma, ukweli ni hawajakamatwa tu, wengine ni wale waliopata urithi kutoka kwa wazazi wao miaka mingi iliyopita. HOJA ZANGU Halmaushari zimekosa sera kutoka wizarani ya kutekeleza, wanajirusha kadri wanavyoweza, unakopa kupima viwanja kila mwaka tunalipa kodi zinaenda wapi??? mtu unalipa kodi zaidi ya milioni moja kila mwezi PAYE lakni hakuna huduma??? kila huduma unalipia MAJI, HOSPITALI, UMEME unadaiwa mita, nguzo ikibidi nyaya, ARDHI bei juu, MAHAKAMA, ELIMU, BARABARA road license, ZIMAMOTO etc hii ni mifano tu, kweli aibu. Ujanja ujanja mwingi mnatuingiza kwemye gharama kubwa, kule vijijini kiwanja wanapima heka moja miguu sabini kwa sabini, mbona viwanja winakuwepo, hapa kupima kwa GPS kweli TZS 8000/- kwa mita square moja???? kwa lipi hapo waziri??? kama technolojia ni gharama na hairahisishi kazi (maana hata hivyo viwanja havipatikani) basi haitufai, wanaikumbatia maana ni chanzo cha rushwa wanazozihitaji. Kosa lako ni kushindwa kuona hayo, NCHI YETU TUNAHITAJI VIWANJA VIPATIKANE SIO KWA KUOMBAOMBA NI HAKI YETU. Makudu yanapima viwanja vijijini na maisha yanakwenda. Teknolojia aghali kiasi wanaohitaji kuitumia hawana uwezo wa kuimudu haihitaji uwe profesa wa kweli kujua etknolojia hiyo haina tija kwa wananchi.