king kan
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 1,642
- 2,079
Suala la ardhi limeangamizwa na rushwa.Namshauri waziri amuombe Rais aweke agenda ya ardhi katika kikao kijacho cha baraza la mawaziri,ili azimio liandaliwe mahsusi kuhamisha mamlaka kutoka serikali za mitaa na kurejeshwa serikali kuu.Na maamuzi yote ya ugawaji wa ardhi yasimame mara moja ili iandaliwe policy itakayo elekeza nguvu zake kwenye equity,transparency ,integrity na accountability.Hapa tuna tatizo la ardhi kwa wafugaji na wakulima,ardhi kwa ajili ya makazi,ardhi kwa ajili ya uwekezaji mkubwa ,wa kati na mdogo pamoja na ardhi kwa ajili ya uhifadhi wa mazingira na Mali ya asili.Tumesomesha watanzania wengi sana hapo Chuo cha ardhi na wengine wapo vyuoni hadi hivi Sasa.Ina maana wote hao hakuna kitu kichwani hadi tufikie hapa tulipo Sasa?Ushauri wangu tena,serikali iandae kongamano kubwa pale ardhi university,tupate mawazo ya watanzania wengi,yafanyike kazi mara moja katika kuandaa policy yenye muelekeo niliotaja hapo mwana..Nawasilisha.
Tatizo kubwa halipo kwenye output kutoka Ardhi University. Ushauri wa kitaalamu mara nyingi hauzingatiwi, mfano Shivji alitoa mapendekezo mazuri sana lakini tume yake ilipuuzwa na serikali, Prof. Tibaijuka (akiwa chairperson akishirikiana na Prof. F Kaijage) mwenyewe akiwa UDSM waliandika paper nzuri kwenye Land Tenure Study Group (1995) lakini serikali haikutilia maanani ushauri wao. Mara nyingi matatizo ya Ardhi yamesababishwa na kukosekana kwa uwajibikaji au rushwa.