Fundi Madirisha
Senior Member
- Jun 30, 2020
- 184
- 987
Kwa jicho la kawaida sana nakiona hiki hakina maisha marefu. Kina mtaji mkubwa wa wanachama kule Zanzibar lakini kwa siasa anazofanya kiongozi wake mkuu, sioni kabisa maisha marefu ya chama hiki. Anataka kutumia usanii katika kukiendesha chama hawezi kufika mbali.
Huwezi kuwa mstaarabu kwa mtu ambaye si mstaarabu. CCM hawataki ustaarabu wa kuendesha nchi hii, hawapo tayari kabisa kuona mabadiliko ya kimfumo yafanyike. Sasa ACT-Wazalendo kwa Hadaa za Zitto Kabwe wameingia kwenye mtego wa CCM kufanyia marekebisho NEC ambayo kimsingi hata viongozi wa kamati hiyo ni wanaccm. Hivi kuna asiyemjua Prof Mkandara Itikadi yake? Kuna asiyemjua Halafu Rashidi wa ADC ambaye Chama chake ni sawa na UDP ya Cheyo?
Sababu kuu ya ACT-Wazalendo ya kudai marekebisho ya tume huru ya uchaguzi na siyo Katiba mpya eti wanataka tume huru ili wachaguliwe waende bungeni wakiwa wengi wakadai katiba, huu ni unafki wa hali ya juu sana. Yaani ACT hawaoni umuhimu wa kuandika katiba wao wanahangaika maslahi ya kisiasa badala ya mfumo? Hawaoni Shida wanazopata wananchi kupitia mifumo iliyopo ya kiutawala ila wao ni uchaguzi tu?
Kwa sasa watu wanalia majeshi la Polisi kwa sababu ya mfumo, watu wanalia na mahakama zetu kwa sababu ya mfumo, tunalia na Ufisadi kwa sababu ya mfumo, leo hii wenzetu wanaona mfumo unaweza kubadilishwa na NEC?
CCM hawataki ustaarabu lakini wanataka wenzao wawe wastaarabu, demokrasia ina gharama zake. Kama watu waliwahi kupoteza maisha, kama kuna watu waliwahi kupigwa risasi, kama kuna watu waliwahi kutekwa na kupotezwa , yote haya ni kwa sababu ya CCM kungan'ang'ania madaraka. Kwahiyo ni lazima kuwe na msimamo wa CCM kuondoka madarakani kwa nguvu ya umma wapende wasipende. Mtu anapokataa ustaarabu basi lazima nawe usiwe mstaarabu. Hii ni nchi yetu sote hakuna mwenye hati miliki nayo.
Zitto Kabwe hajawahi kushika madaraka makubwa kama aliyonayo ya sasa kama kiongozi mkuu wa chama chake, nafasi yake kwenye kutafuta suluhu serikali ya Mapinduzi Zanzibar anajiona ni nafasi kubwa na ananyenyekewa sana, kumbe hajui kuwa wenzake wanatazama mbali zaidi. Hicho chama kingefika mbali angekuwepo Maalim Seif, Zitto Kabwe si mwanasiasa wa kuaminika ,siyo wa kuachiwa taasisi pekee yake aendeshe. Sina imani kama Maalim Seif angekuwepo angekubali kudai marekebisho ya uchaguzi badala ya katiba mpya, au labda kwakuwa Katiba ya Zanzibar ina ahueni kidogo. Maskini Zitto amesahau kuwa Katiba ni muhimu zaidi kuliko tume.
Tunazungumza humu lakini ni suala la muda tuu. Tunajua suala liingine la ACT-WAZALENDO ni njaa wanataka wapate wabunge waende wakaongeze ruzuku ili waendeshe chama chao, ACT-WAZALENDO hawana shida kabisa na kushika dola.
Huwezi kuwa mstaarabu kwa mtu ambaye si mstaarabu. CCM hawataki ustaarabu wa kuendesha nchi hii, hawapo tayari kabisa kuona mabadiliko ya kimfumo yafanyike. Sasa ACT-Wazalendo kwa Hadaa za Zitto Kabwe wameingia kwenye mtego wa CCM kufanyia marekebisho NEC ambayo kimsingi hata viongozi wa kamati hiyo ni wanaccm. Hivi kuna asiyemjua Prof Mkandara Itikadi yake? Kuna asiyemjua Halafu Rashidi wa ADC ambaye Chama chake ni sawa na UDP ya Cheyo?
Sababu kuu ya ACT-Wazalendo ya kudai marekebisho ya tume huru ya uchaguzi na siyo Katiba mpya eti wanataka tume huru ili wachaguliwe waende bungeni wakiwa wengi wakadai katiba, huu ni unafki wa hali ya juu sana. Yaani ACT hawaoni umuhimu wa kuandika katiba wao wanahangaika maslahi ya kisiasa badala ya mfumo? Hawaoni Shida wanazopata wananchi kupitia mifumo iliyopo ya kiutawala ila wao ni uchaguzi tu?
Kwa sasa watu wanalia majeshi la Polisi kwa sababu ya mfumo, watu wanalia na mahakama zetu kwa sababu ya mfumo, tunalia na Ufisadi kwa sababu ya mfumo, leo hii wenzetu wanaona mfumo unaweza kubadilishwa na NEC?
CCM hawataki ustaarabu lakini wanataka wenzao wawe wastaarabu, demokrasia ina gharama zake. Kama watu waliwahi kupoteza maisha, kama kuna watu waliwahi kupigwa risasi, kama kuna watu waliwahi kutekwa na kupotezwa , yote haya ni kwa sababu ya CCM kungan'ang'ania madaraka. Kwahiyo ni lazima kuwe na msimamo wa CCM kuondoka madarakani kwa nguvu ya umma wapende wasipende. Mtu anapokataa ustaarabu basi lazima nawe usiwe mstaarabu. Hii ni nchi yetu sote hakuna mwenye hati miliki nayo.
Zitto Kabwe hajawahi kushika madaraka makubwa kama aliyonayo ya sasa kama kiongozi mkuu wa chama chake, nafasi yake kwenye kutafuta suluhu serikali ya Mapinduzi Zanzibar anajiona ni nafasi kubwa na ananyenyekewa sana, kumbe hajui kuwa wenzake wanatazama mbali zaidi. Hicho chama kingefika mbali angekuwepo Maalim Seif, Zitto Kabwe si mwanasiasa wa kuaminika ,siyo wa kuachiwa taasisi pekee yake aendeshe. Sina imani kama Maalim Seif angekuwepo angekubali kudai marekebisho ya uchaguzi badala ya katiba mpya, au labda kwakuwa Katiba ya Zanzibar ina ahueni kidogo. Maskini Zitto amesahau kuwa Katiba ni muhimu zaidi kuliko tume.
Tunazungumza humu lakini ni suala la muda tuu. Tunajua suala liingine la ACT-WAZALENDO ni njaa wanataka wapate wabunge waende wakaongeze ruzuku ili waendeshe chama chao, ACT-WAZALENDO hawana shida kabisa na kushika dola.