Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
zitto ni mzigo yeye anafanya mambo as if alipokuwa spika wa bunge la UDSM..no way aende tu ...hafai hata kidogo kuwa CHADEMA na kumuacha ni hatari auende akajiunge na TLP au CCM

Zito hakuwahi kuwa spika na wala asingeupata huo uspika, walipompa uenyekiti fass basi walishamjua, but the boy is good katika fitina za siasa na hasa ndi siasa yenyewe,anatafauta idntity yake mwenyewe tofauti na chama, na kama sisiemi wakilitumia hilo watakuwa wamecheza karata dume, hizo ndio siasa bwana, hazina kanuni wala uaminifu hiyo ndio kanuni zake
 
Hawezi kwani CDM haimtambui kama rais, pili katiba haijaruhusu serikali ya mseto na inaitwa serikali ya CHAMA TAWALA hapo Brooo hiyo ni ngumu na ni ndoto.
 
JK aliposema atashirikisha wapinzani kwenye serikari yake alikuwa ana maanisha CUF au? Je akifanya uteuzi wa kichokozi kwa kumteuwa ZITTO ambae amekuwa PRO-JK kwa sababu zinazoeleweka itakuwaje?

Hayo maneno aliyasoma kwenye hotuba yake au alisema nje ya yale aliyokuwa anasoma? Nadhani alihitaji makofi ya wabunge wa upinzani waliokuwa mle ndani, na wewe unafikiri wabunge wa CCM watalipokea hilo? Raisi amewekwa na chama anatekeleza yaliyokwishaamuliwa ndani ya vikao vya chama husani Kamati kuu, Case Study Thabo Mbeki AS
 
Ndugu Wana JF,

Kuna uwezekano mkubwa baadhi ya wabunge wa chadema wenye muelekeo wa kuitambua serikari ya JK na kutaka kushirikiana na CCM na huenda wakatajwa kuwa kwenye Baraza la mawaziri la JK, Lengo likiwa kuleta msuguano na mitafaruku ndani ya chama chetu cha chadema.

Kwani misimamo mingi ya bwana ZITTO KABWE imekuwa ikiwapa talking point wapinzani wakubwa wa chadema hususani CCM, na nadhani JK anaweza kuwateuwa baadhi ya wabunge wa chadema hususani ZITTO KABWE kama wachambuzi wengi wa masuala ya kisiasa wanavyo speculate, Je ikiwa baadhi ya wabunge wa chadema watateuliwa chadema wamejipanga vipi kukabiliana na suala hilo lenye nia ya kutaka kuongeza msuguano na kukidhohofisha chama? watakubali uteuzi au watawazuia wabunge hao kushiriki kwenye serikari ya ccm, na je uamuzi wowote wa chama utakuwa na repucation gani kisiasa?

Ni mtazamo wangu huru, wadau tujadili hili.












hawezi kuwateua..
kama wameharibu huku hata kwao ataharibu... tabiaya mtu haibadiliki kirahisi kama mtu ni mnafiki ataendelea kuwa mnafiki tu....
at the end atakosa sehemu ya kushikia...
wamuulize Agusstino Lyatonga Mrema alikoishia...
Mtu watanzania tuliyemheshimu kwa kutokuwa na msimamo ndo amedharaulika kuliko wanasiasa wengine wote...
naamini Chama Chetu kinaweza kuendelea bila Zitto bwana.
 
kuna vitu ccm wanaweza kufanya na vingine hawawezi. Kama wananshindwa kuwapa wabunge wao wenye uwezo wa kupambana na ufisadi nafasi nyeti kama mambo ya ndani nk watafikiria kuwaingiza wapinzani serikalini?

kwa bahati mbaya nilikuwa sijasoma mahojiano ya zitto na vyombo vya habari, baada ya kuyapitia kidogo nimegundua huyu dogo hana akili kabisa. Anadai kuwa rais jakaya kikwete kawafanyia makubwa watu wa kigoma. Kwa maneno mengine anataka kusema kuwa laiti kama ccm wakiwa na mbunge hapo wanakigoma wanaweza kupata makubwa zaidi. Yaani yeye kama zitto na chadema haina mchango wowote huko kigoma ila rais kikwete.

Sasa kama ni hivyo yeye chadema bado anafanya nini? Si bora angungana naye ccm ili kuendeleza gurudumu la kigoma kupata maendeleo makubwa zaidi.

Tatizo la zitto ni hajakubali kusamehe yaliyopita, hususan kile kinyanganyiro cha uenyekiti wa chadema. Hivyo huwa ana seize every opportunity ya defame mbowe ili aonekane hana lolote. Na katika kufanya hivyo analazimika kujidefend kijinga na kitoto kama anavyofanya, lakini tayari damage inakuwa imeshaingia kwenye chama.

Na hiyo ndiyo challenge ambayo chadema inabidi waikubali na kujipanga kuihandle kwa uangalifu mkubwa sana, kama ccm walivyo handle issue ya sitta. Tusiwalaumu wazee na viongozi wa chadema kw akuwa hata wazee na viongozi wa ccm kuna kipindi walitaka kukosea kuhandle issue ya sitta na ilitaka kubackfire vibaya kwano hadi walipounda kamati ya usuluhishi ya mzee mwinyi.

Wazee na viongozi wa chadema should first and foremast wakubali kuwa katika kinyanganyiro cha uenyekiti na uchaguzi mkuu, viti maalum, na kambi ya upinzani kume zusha nyufa, hivyo zinatakiwa kuzibwa. Kabala ya kikao kijacho cha bunge. Kukubali hivyo sio kujidhoofisha badala yake ni kujiimarisha kw akuwa chadema ni chama kinachokua kw akasi sana of recent na majukumu yake yamepanuka sana.

Baada ya kukiri hivyo wasuluhishane ili kuwaonyesha watanzania kuwa chadma inaweza kusolve internal disputes amicably. Hivyo ndio kitaweza kuaminiwa zaidi. Kwa kuwa mbowe kama mwenyekiti yuko at the centre of stage ya migogoro midogo midogo hivyo asiwe part ya kutafuta suluhisho, awe sehemu ya watu wanaofanyiw usuluhishi.

Moja ya mapendekezo amabyo naweza kutoa kama njia ya usukuhishi ni kupiga marufuku kwa viongozi na wabunge wa chadema kudiscuss chadema's sensitive information kwenye social forums kama facebook, jamii forum n.k. Hiii itasadia kuleta harmony kwenye chama na being an opposition camap tutaaminika zaidi. Na atakaye kiuka achukuliwe hatua baada ya usuluhishi.

Kikubwa tukumbuke kuwa kutofautiana misimamo na migogogoro ni kitu cha kawaida katika vyama vya siasa, ama kuvujisha siri za chama pia hutokea mara kwa mara. Athari inayoikumba chadema ni ile dhana ya usomi wakati viongozi wa ccm wakivujisha siri zao mpaka zidakwe na wandishi wa habari inachukua muda,

youthfulness ya chadema inayowaelekeza viongozi wake wengi kutumia social foums wakiamua kuvujisha siri za vikao vya chadema hutapakaa kama bush fire.

 
Serikali anayounda JK ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ni ya chama kilichoshinda (CCM) na hakuna mabadiliko ya katiba yaliyofanyika kuunda serikali ya umoja!
 
JK aliposema atashirikisha wapinzani kwenye serikari yake alikuwa ana maanisha CUF au? Je akifanya uteuzi wa kichokozi kwa kumteuwa ZITTO ambae amekuwa PRO-JK kwa sababu zinazoeleweka itakuwaje?
Vipi ndugu yangu! Hujui kuwa jk huwa anaongea kitu ambacho hata yeye mwenyewe hakijui? Na hawezi hata kukitolea ufafanuzi muda mfupi baada ya kukizungumza? Na anapenda sana kupigiwa makofi hata kama alichokisema hakivutii!

Si sera ya ccm kuwa na serikali ya mseto. Na hata makubaliano ya ccm na cuf, ni kwa zenji tu,ambako kura ya maoni ilipigwa!
 
je hakuna repucation zozote kama chama kikimwaga zitto, kwani kumekuwa na propaganda za udini chadema na hizo propaganda zinatumiwa makusudi na ccm ili kumweka zitto kama icon ndani ya chadema hivyo basi kama chadema kita mwaga zitto , ccm hawawezi take advantage kukimaliza chama chetu kisiasa?

kutofautiana misimamo na migogoro ni kitu cha kawaida hata katika ndoa ya watu wawili. Sembuse chama chenye wananchama maelfu hata mamilioni. Hoja ya msingi ni kuwa chadema lazima ijijengee uwezo wa conflict resolution haraka sana. najua chadema tayari wana uzoefu wa kutatua migogoro, wanatakiwa kuwekeza nguvu zaidi katika monitoring and evaluation of terms za usuluhishi.

Kwa kuwa uongozi utakuw ana majukumu makubwa ya kukijenga chama na kuhudumia kambi ya upinzani bungeni, wazee wa chadema wachukue leading role of that process.
kikubwa wengi tunachangia kwa jazba sana na kuhukumu moja kwa moja kabla ya kuwapa watu nafasi kusikilizwa. Let people be heard.
 
Acheni kuchonganisha CHADEMA badala ya kuwashauri
 
Je hakuna repucation zozote kama chama kikimwaga ZITTO, kwani kumekuwa na propaganda za udini CHADEMA na hizo propaganda zinatumiwa makusudi na CCM ili kumweka ZITTO kama icon ndani ya chadema hivyo basi kama Chadema kita mwaga ZITTO , CCM hawawezi take advantage kukimaliza chama chetu kisiasa?

Watanzania wanaelewa nani wanafanya propaganda za kidini na tukisema tuchague kwa udini ni nani atashinda mimi nashangaa kwa nini waislamu wanawadharau wakristu wakati tumeongozwa na viongozi waislamu na wapita sehemu ambazo kuna wakristu wengi, lakini sehemu ambazo waislamu ni wengi sijawahi kuona anapita mkristu na safari hii tumeona. Chadema ina wakristu wengi kama ambavyo CUF wote ni waislamu sasa tunamlaumu nani wakati hakuna mkristu aliyekatazwa kujiunga na CUF wala muislamu aliyekatazwa kujiunga na chadema.

Ila swali langu ni kuwa kwa nini viongozi wote wa juu serikali hii ya awamu ya nne ni waislamu? mfano JK na Makamu wake, Shein na Makamu wake wawili etc. sasa kwa chadema mwenyekiti na katibu kuwa wakristu na makamu mwenyeki na naibu katibu mkuu waislamu kwa nini inatuhumiwa kwa udini, ile hali CCM mwenyekiti,Katibu mkuu makamu mwenyekiti zanzibar wote ni waislamu hakuna anayepiga kelele.

CCM na CUF msiongee kabisa issue ya udini maana inawahusu sana, maana ndo mmeunda serikali yenye harufu ya udini tangu 2005 mpaka sasa.

Issue hapa ni maisha bora, Huduma bora, Elimu bora, mambo ya udini tumeletewa na wakoloni na wazungu na waarabu hawahangaikii hata kido ila sisi huku ndo tunasubua, na ndo chanzo cha umasikini wetu.
 
Zanzibar wamebadilisha katiba yao ili kuruhusu serikali ya mseto, katiba ya Jamhuri ya Muungano bado ni ileile, kama akidhubutu kufanya hivyo itakuwa opportunity kwa upinzani maana raisi atakuwa anakiuka katiba!

Hatuongozwi na illusion, katiba ndo inayotuongoza mbali na kwamba inahitaji kufanyiwa marekebisho, sishangai kama JK ana ndoto hizo, kwa ccm ni kawaida!

Na kama Zito anataka kujichafua kisiasa aisaliti CHADEMA! watanzania wa sasa si wale wa mwaka 47!
 
Acheni bangi nyie, Shibuda is a nutcase, how could he possibly be a Minister, atakuwa waziri wa kitu gani?!! lol. No such thing!
 
Jatropha, NAKUBALIANA NAWE MKUU. UTATUZI WA MIGOGORO WAZEE WA CHADEMA WAFANYA HIYO KAZI HARAKA BEFORE NEXT BUNGE; KUWEKEA MASHARTI MAALUMU VIONGOZI KUJENGA UMOJA MIONGONI MWA JAMII BADALA YA KUONGEZA MIPASUKU UNNECCESSARILY
 
Hofu ya Zitto ni kufunikwa na Mnyika ambaye ndiye mpinzani wa kweli na ni msomi mahiri kuliko Zitto.
Nadhani huyu bwana mdogo anahitaji kupepewa
 
Dah!!! ile tthead ya saa sita mchana ni kweli imetolewa????? C'mooon JF there is some fishy bness going on administrator ungeiacha banaa!
 
Wakati Bashe na Nape walipokuwa wakiongeea uvundo wa CCM walikuwa mashujaa/wazalendo...Zitto akiongelea uozo wa Chadema anakuwa msaliti...Kweli CHADEMA imeingiliwa. Kwa siasa za chuki na ubaguzi kama hizi ni wazi kile chama tuliofikiri kuwa kinaweza kuwa mbadala makini wa CCM ndio kinaelekea kuwa a truly CCMs photocopy......
 
Hofu ya Zitto ni kufunikwa na Mnyika ambaye ndiye mpinzani wa kweli na ni msomi mahiri kuliko Zitto.
Nadhani huyu bwana mdogo anahitaji kupepewa

Kujaribu kumfanya Mnyika kuwa mshindani ama adui wa Zitto hakumsaidii Mnyika na wala CHADEMA. Hawa pamoja na Halima Mdee wanapaswa kuwa mbali na hizi siasa za makapi ya CCM (SLAA na MBOWE) ili muda utakapowadia wao kuondoka basi ile nuru ya chama mbadala makini iweze kushamiri.......Kumbuka, hata Mnyika naye ana mapungufu yake na hivyo kumuingiza katika hii vita dhidi ya Zitto kunaweza kumfanya mhanga asiye na hatia.....Ni wazo la busara tu
 
Kujaribu kumfanya Mnyika kuwa mshindani ama adui wa Zitto hakumsaidii Mnyika na wala CHADEMA. Hawa pamoja na Halima Mdee wanapaswa kuwa mbali na hizi siasa za makapi ya CCM (SLAA na MBOWE) ili muda utakapowadia wao kuondoka basi ile nuru ya chama mbadala makini iweze kushamiri.......Kumbuka, hata Mnyika naye ana mapungufu yake na hivyo kumuingiza katika hii vita dhidi ya Zitto kunaweza kumfanya mhanga asiye na hatia.....Ni wazo la busara tu

Ukitulia huwa unaongea mapoint sana ukikutana na vibabu vya CCM aaaaah :llama:
 
Mbona siyo siri tena? Hata mfuasi wa CCM hapa ukumbini Selemani kishasema kuna mipango ya ku-infiltrate Chadema.

Kaka na wewe unaamini hii propaganda ya infiltration?

Chadema wana mapungufu mengi tena Mbowe ndio liability kuu na sasa hiki kihoro cha kukosa Urais cha Slaa. Hii ya infiltration imekuwa ikitumika tangia enzi za Kabourou ili kuhalalisha siasa zao za kumtenga. Hata Mzee Makani naye walidai hivyohivyo kama ilivyokuwa kwa Shahibu, Chacha Wangwe na hata Kafulila. Its a cheap prpaganda ambayo rafiki yako Mbowe na watu wake wamezoea kuitumia kukandamiza mitazamo tofauti ndani ya chama haswa kwa wale wanaodare kuthreaten nafasi ya Mbowe na watu wake na kuhoji yasiyotakiwa kuhojiwa.

Hivi ujiulizi ni kwanini wakati wa neema kama huu kuna watu wenye nafasi zao Chadema wanahama chama kila kukicha. Hata yule Mwenyekiti wa Mbeya ambaye ukweli ni Mbowe aliyehusika na sakata lake katika uchaguzi wa 2008 kama watu hawajamtuliza ni wazi ataondoka sasa hivi. Uzuri ni kuwa hawaendi CCM kama ambavyo wanapropaganda wa CHADEMA wanavyombea ili kualalisha ujinga wao.....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom