Zitto Kabwe ameeleza kuwa ni kweli walipiga kura na kukubaliana watoke wakati Rais akizungumza, lakini wao walipinga na ndiyo maana aliamua bora asiingie ndani ya Bunge, mesema kuwa yeye kama Zitto na wenzake aliona ni bora kutoingia kuliko kuingia na kutoka wakati Rais ambaye ndiye alama ya Bunge na Amiri jeshi mkuu akiongeaa.
Kwa vile kutoka ulikuwa msimamo wa chama, basi yeye na wenzake wamekosea na hilo ni swala la Chama kwani wanaweza kuadhibiwa na chama kwa vile kura za kukubaliana kutoka ilishinda.
Zitto alisema kuwa wanasubiria hatma yake katika chama na kusema kuwa hiyo ndiyo gharama ya Demokrasia. Ila amekanusha kuwa jambo hilo lisifikiliwe ni mgawanyiko bali mtazamo tofauti wa mawazo.
Source: TBC 1 News Bulletin
Kuna wakati nilikuwa nashirikiana na vijana fulani wa Kigoma katika kutatua tatizo lao, sasa mambo yalikuwa kama haya tunakubaliana hivi wao wanakwenda kinyume na makubaliano. Mtu mmoja akanishauri ya kwamba watu wa Kigoma wana kawaida ya kuwa kigeugeu hivyo niachane na shauri lao, sijui kuna ukweli juu ya hili? Maana tabia wakati mwingine zinaweza kutegemeana na asili yetu (mother land).
Nadhani Zitto aanchojaribu ni kuwafundisha nyie mashabiki wa CHADEMA kwamba msiwe watumwa wa mawazo, mitazamo na miongozo ya wachache. Kwa nini awe mtumwa wa mawazo ya Mbowe na Dr Slaa wakati yeye msomi na mwenye exposure ya siasa ya kimataifa.. Nyie lazima mkubwali kile kitendo kilikua cha kitoto na kilidhihirisha kutokua nna malengo ya muda mrefu ya chama.
inauma eee?? Toka mwanzo nilishasema. Kigoma wanatoaga vifaa. Kgm hatuchagui chama bali mtu. Ndio maana kgm ina karibu vyama vyote kasoro cafu.zito ni kichwa. Very brilliant. Ni mtanzania. Ni mzalendo. Hekima na busara na utaifa kwanza. Sio kususa tu. Yatawatokea puani wale wanaoshabiokia bila kufikiri. Sasa habari hii inawauma. Wanajuta aliyeileta jamvini. Lakini si ndio ukweli?? Kwani zito sio kiongozi wa upinzani bungeni? Kwa nini achicheme yaliyo moyoni mwake???
i fully support him 100%.
besides chadema bila dr. Mfuko wa cement 5000/= inaweeekana!
Hilo jina unalotumia haliendani na wewe kabisa,
Hebu elewa hivi
Watu hawamlaumu Zitto kupingana na wenzie, hiyo ni demokrasia na ndio maana Chadema waliitisha kura
WATU WANAMLAUMU ZITTO KUKIMBILIA KWENYE VYOMBO VYA HABARI NA KUROPOKA SIRI ZA CHAMA, KWANI ZITTO ALIKUWA PEKEYAKE ALIYEPINGA?, MBONA WENGINE HAWAKWENDA KWENYE VYOMBO VYA HABARI? YEYE NI NANI? NI MSEMAJI WA CHAMA?
Hilo jina unalotumia haliendani na wewe kabisa,
Hebu elewa hivi
Watu hawamlaumu Zitto kupingana na wenzie, hiyo ni demokrasia na ndio maana Chadema waliitisha kura
WATU WANAMLAUMU ZITTO KUKIMBILIA KWENYE VYOMBO VYA HABARI NA KUROPOKA SIRI ZA CHAMA, KWANI ZITTO ALIKUWA PEKEYAKE ALIYEPINGA?, MBONA WENGINE HAWAKWENDA KWENYE VYOMBO VYA HABARI? YEYE NI NANI? NI MSEMAJI WA CHAMA?
Kwani hili halikuwa wazi? Wangapi walisikika wakipiga kampeni kwa visingizio vya elimu ya kiraia?Pia nimemsikia Zitto akihojiwa na Tbc akikubaliana na hotuba ya Kikwete ya kuwa kwenye uchaguzi kulikuwa na udini.
Du!Zitto ni very smart ndani ya Chadema. Huyu jamaa ndiye aliyetakiwa agombee Urais kupitia Chadema.
Sio Zitto tu hata Dr Slaa alikiri hilo kwenye clip. Haka kamchezo walikoanza CHADEMA bila kujipanga kanawaharibia saana na huenda kakaharibu zaidi.Ina maana Zitto anamtambua JMK kama rais "halali" wa JMT?
naomba kuelimishwa hapa.
Du!
Ustaadhi, Inaonekana unajua kuliko wanachadema wenyewe!