Zitto amkaribisha Kafulila CHADEMA

mkuu uko very correct, ata kama kafulila ataomba na kurudi cdm na ata kugombea kwa tiketi ya cdm, fine lkn lazima wajue (zito pia kafulila) ajenda zao ziko bayana na watanzania tunawafahamu na mipango yao iko bayana kabisa, zito kabwe ajirekebishe mwenendo wake ambao hatukubaliani nao, aswa yeye km kiongozi wa cdm vinginevyo post ya unaibu katibu mkuu wa chama haiache,

kujiingiza tu ktk mambo ya nccr ata kuwajulisha polisi kilichokuwa kikijiri ktk kikao cha nccr by any means hakikuwa sahihi ana masilahi yapi uko NCCR, asa kwa kiongozi wa cdm mwenye post ya unaibu katibu mkuu wa chama cdm.

bwana zito be serious tunaiunga mkono chadema kwa kuwa tunaamini ukombozi wetu uko uko, sasa wewe na NCCR kulikoni?? viongozi wa chadema muwe serious o/w mjue uko mbele ya safari hatutataka

Mkuu, Zitto hana adabu hata mimi naelewa. Lakini tumtendee haki. Wapi umethibitisha Zitto kaita Polisi kwenye mkutano wa NCCR? Acheni kutumika kijinga bila kujijua. Yeye mwenyewe amesema hawezi kuwa na interest kwenye chama kisicho na mwelekeo na kilichopoteza dira kama NCCR Manunuzi. Tusiutumie unafiki wa Zitto kukuza mambo
 
Mbowe mbona unakuwa mnafiki, kwani Chadema walivyowafukuza madiwani Arusha hawakutumia busara!

Au Arusha gharama sio kubwa!
 
wadau ehh,kufukuzwa kwa kafurila it means na ubunge nao out,sasaa,tujiulize,chaguzi mpya ndogo zitaitishwa hadi lini kwani fedha za walipa kodi zinatumika ovyo wakati wananchi wana matatizo kibao,kuna haja hii sheria ya uchaguzi ifanyiwe maboresho ikizungumzia pia na suala kama hili
 
Mbowe mbona unakuwa mnafiki, kwani Chadema walivyowafukuza madiwani Arusha hawakutumia busara!

Au Arusha gharama sio kubwa!

Jaribu kushirikisha ubongo kujua kilichojiri Arusha ndio uje u-post hapa!!
Madiwani waliitwa,
wakakalishwa chini,
wakaombwa,
wakabembelezwa,
Wakaonywa,
na kusisitizwa wabadili msimamo lakini wapi!!
Kafulila ni kama pigo la Knock Out! Ngumi moja hiyohiyo ndiyo iliyompeleka chini, hakuna kujitetea, kujiuliza, kujifikiria wala kuonywa!!
Usifananishe mkuu!!
 
Ukweli ni kwamba wale madiwani walilazimisha ili wafukuzwe nilipata kusikia mazungumzo yao mkoani Dodoma kwenye hoteli waliyofikia kabla ya kuingia kwenye kikao cha kujieleza hawakuomba hata wasamehewe na kuna mmoja wao aliteka akili za wenzake. Ndiyo maana CDM hawamfukuzi Shibuda kwani hajalazimisha afukuzwe nadhani hata Kafulila hajalazimishwa afukuzwe. Tujenge utamanduni tu wa kuomba msamaha tunapoteleza hasa kwa kushauriwa vibaya au kulewa sifa za kijinga.
Mbowe mbona unakuwa mnafiki, kwani Chadema walivyowafukuza madiwani Arusha hawakutumia busara!

Au Arusha gharama sio kubwa!
 
Jaribu kushirikisha ubongo kujua kilichojiri Arusha ndio uje u-post hapa!!
Madiwani waliitwa,
wakakalishwa chini,
wakaombwa,
wakabembelezwa,
Wakaonywa,
na kusisitizwa wabadili msimamo lakini wapi!!
Kafulila ni kama pigo la Knock Out! Ngumi moja hiyohiyo ndiyo iliyompeleka chini, hakuna kujitetea, kujiuliza, kujifikiria wala kuonywa!!
Usifananishe mkuu!!
fair comment! Umeangalia ukweli zaidi ya emotions za kichama. Hongera!
 
Dili la Zitto kwa Kafulila limefutika ghafla na kitendo cha yeye kuandika fb kama tulivyoona still Zitto kwangu simuamini hata kidogo na akijua kua alivyoikejeli cdm na viongozi wake kirahisi rahisi tu anamkaribisha,hapa la msingi kwangu huyu Kijana Kafulia its better afanye makubaliano maalumu na cdm ndio asamehewa huku akiwa chini ya akina Prof Baregu wakimuelekeza njia nzuri za kuendesha politics tofauti na papara alizokua anazifanya
 
Bila juhudi zake za kufichua maovu ya serikali kule bungeni na kujitoa muhanga kwa kukubali kupewa kifungo cha kutokuhudhuria vikao vya bunge kufuatia msimamo wake juu ya Karamagi kusaini mkataba nje ya nchi hatua iliyopelekea CHADEMA kuanzisha Operation Sangara iliyowafanya kupata supporters wengi, CHADEMA ingekuwa hapo ilipo? Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Hao mnaowafikiria sio Virus kama Mbowe mlishawahi kumuuliza kitu gani kilitokea mpaka CHADEMA 'ikakabidhi' kiti cha Ubunge KIBAHA kwa CCM? Umeshawahi kuhoji huyo mheshimiwa Mbowe alishiriki vipi?
 
Kama CHADEMA wana msimamo wa kukataa watu wanaowakejeli na kwenda tofauti na wanachokiamini, WANASUBIRI NINI KUMFUKUZA SHIBUDA?
 
WE NEED HAVOC IN OUR POLITICS TO BRING RESPECT AND INTERNAL CONTROL

ukiwa na wale wa ndio mzee, tunaishia kuwa kama CCM, amabpo kuna billions of talents but they end up kuwa mabubu simply because ya ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI NA WENYE PESA....

Kafulila questioned the chairman's ability to run the party and he was right, but because of Tanzania politics, he got booted; democracy yetu inanuka hadi kwenye vyama vyenyewe

Leo hii tunaona Mbatia yuko right, lakini humu JF tulikua juu sana kumuita mbatia kibaraka wa CCM. coming back to other parties... tunaona precedent ipi from NCCR?? si sawa tu na kafu sasa nao wanataka kutimuana?? a few weeks ago CCM nao nusura watimuane?? what about wale madiwani wa arusha??

OUR POLITICS NI ZILE ZENYE MTAZAMO WA GEORGE BUSH "EITHER YOU ARE WITH US, OR YOU ARE OUR ENEMY"

Mbaya sana kufukuza mtu eti kwa sababu ya kutofautiana na Mh mwenyekiti, na si kwa utendaji mbaya, je wabunge wake wote wakitofautiana naye atawatimua wote? kwa mitndo huu vyama vya upinzani havitafika popote, nawasifu CCM wanavyomaliza tofatui zao bila kufukuzana, wako makini sana kwa hilo, huwa hawakurupuki, kwa hili la kafulila hapa Mbatia amekurupuka, wangeweza kuelewana na kupeana hatua zingine za kinidhamu na si kumfukuza mbunge dishonorably!
 
Sijui ataenda wapi, Kafulila bado tukumbuke ni mwanadamu tu na ni kijana. lakini naamini wengi tunamkubali kuwa ni mpiganaji mzuri anayejua kupanga mashambulizi yake. Na pia tunakubaliana kuwa anahitaji msaada kwenye maeneo baadhi. Wakubwa wamsaidie Kafulila, yeye bado ni zao linaloweza kuwa msaada mkubwa siku za usoni kwa Tanzania yetu.

Alisaliti cdm anaweza akawa tena sumu mbaya labda masharti na vigezo vizingatiwe.
 
Kama mm naona chadema wakutane atakapotaka kurudi wamjadil pia asimame tena ktk nafasi yake agombee atapita cuz ana sera nzuri sema alisalit2
 
Tuhangaike zaidi na haka kasheria batili sana ka kuvuliwa uongozi wa kuchaguliwa unapofukuzwa uanachama wa chama kilichokupatia tiketi ya kugombea. Kafulila hakuchaguliwa na wana-NCCR tu. Kachaguliwa na WATANZANIA wa jimbo hilo.

Kikundi kidogo tu cha viongozi wa NCCR wanakaa hapa Dar wanafanya maamuzi ya kijinga kama haya bila kujali wapiga kura wake. Gharama za uchaguzi mdogo zitawaangukia WATANZANIA wote.

Ubakaji huu wa democrasia mchana kweupe namna hii haufai kwa kweli. Kafulila anayo mapungufu yake kama mtu mwingine yeyote. Adhabu hii ndio iliyomstahili kweli kwa mujibu wa KATIBA yao?
 
I think Kafulila needs councelling! We must learn how to put our brains in gear before we release our mouth opens for the tongues to swerve as they feel!

Kafulila anaweza akashinda akikata rufaa lakini sas badda ya hapo inabidi awaheshimu na wenzake pia. No matter how strong and smatter you are, more than one head always arrives to a better conclusion and hence do not disobey others simply b/se you feel you have a mass behind you!
 
Wakti Kafulila anatoka CDM na kutimkia NCCR-Mageuzi aliropoka na kubwabwaja maneno ya ovyo dhidi ya viongozi wa CDM. Mimi nilisema kuwa KAFULILA sasa KAFULIA! Leo tena akiwa NCCR amerudia maneno yake ya kipuuzi ya kudharau uongozi wa Juu wa Chama chake. Hii ni hulka na tabia ya KAFULI. Kafulia ni mropokaji,mkorofi na asiye na adabu kwa viongozi wake. Kwa kifupi hana ADABU.

Inasikitisha kuona kuwa Zitto Kabwe huwa anapenda sana kum-support huyu Kafulia. Sijui ni kwanini Zitto anapenda kujihusisha sana na matatizo au vurugu za Kafulia. Nakumbuka vizuri sana kuwa hata wakti Kafulia anahama CDM, Zito alimtetea Kafulia na kuahidi kumsaidia kwenye kampeni za Ubunge akiwa hukohuko NCCR! Huu uhusiano wa hawa jamaa kidogo unatia shaka!

Zitto na Kafulia wana character zinazo-match kiasi cha kuelewana na kukubaliana katika maswala fulani fulani hata KAMA YATA KIGHARIMU chama husika kwa wakti huo. Hii ni hatari sana kwa chama chochote chenye kuwa na hawa jamaa hasa wakiwa pamoja. Hawa WAKO TAYARI KUPINDUA SERIKALI YA CHAMA KWA GHARAMA YOYOTE. Kumbukeni juhudi za Zitto kutaka kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa-CHADEMA akitaka kushindana na Mbowe! Tamaa ya madaraka na sifa za harakaharaka. Zitto ana high ambitious kwenye siasa na hii itakuja kumgharimu siku moja.

Kwa maana hiyo basi kama Zitto kamkaribisha Kafulila(same tribe) ina maana hawa jamaa watakuwa na agenda yao ya siri, Lazima hawa 2 watakuwa na malengo ya 2015,na sitashangaa kumsikia Zitto akitangaza kugombea Urais 2015 kupitia CDM na huku mgombea msaidizi akiwa ni KAFULIA!

Nawaomba uongozi wa Juu wa CDM usifanye haraka ya kumpokea Kafulia na hata kama atapokelewa awe mwanachama wa kawaida tu asipewe nafasi ya kugombea ngazi yeyote mpaka hapo atakapothibitisha kuwa AMEJIREKEBISHA na awe chini ya uangalizi wa chama kwa mwaka 1 au zaidi.Kwanza atoe sababu za kilichomwondoa CDM wakti huo na sababu zilizomwondoa NCCR kwa sasa na akubali kuitwa kuwa yeye ni MALAYA wa kisiasa. CDM wamweleze pointblank kuwa akileta nyodo zake tu WANAMVUA GAMBA!

Huo ndo ushauri wangu kwa uongozi wa CDM na wana CDM wote nchini.
 
Hebu watanzania tufike mahala tufanye kufikiri kama ni janga linalokaribia kuangamiza utaifa wetu,matokeo yake ni kuzorota kwa uchumi,siasa na utamaduni.
Kuna watu wanamubeza Kafulila pasipo kufikiria juu ya mapana ya Demokrasia ya kweli na inayoonekana katika mihimili yake mikuu.
Kwa nini hatujiulizi kwamba kwa katiba iliyopo ina ufalme wa kichama kuamua kumfukuza uanachama mbunge wake kwa tofauti za mawazo kinyume na uhuru wa mtu kutoa mawazo yake na kuyaheshimu hata kama huyapendi.
Ina wanyima wananchi Fursa ya kumfukuza mbunge wao kwa kushindwa kutimiza majukumu yake ya kibunge ila ina kipa mamlaka makubwa chama kumfukuza mbunge au kumtetea pale ambapo hakidhi matakwa ya wananchi.
Mamuzi ya chama hayapingwi na wananchi.
Chama ndicho Alfa na Omega.
Wananchi ambao katiba ya JAmhuri ya Muungano,ibara ya 9,inatamka wazi kwamba wananchi ndiyo Alfa na Omega kwa masuala yoyote yanayohusu Taifa.
Lakini contradiction yake Chama kinamfukuza mbunge hata kama wananchi wanamwitaji kuliko hitaji la chama!!!!!!!!!
watu tunashangilia kufukuzwa kwa kafulila katika mazingira ya demokrasia ya wakubwa!!!!!!!!!!!siyo ya wananchi!!!!!!!!
Kumbe Demokrasia kwa Tanzania ya kumchagua mwakilishi wao ni wakati wa uchaguzi tuu,wakimchagua hawana nguvu ya kumkataa kwa muda ule mpaka kipindi cha miaka mitano kiishe,Ila Chama kina demokrasia wakati wote wa kumuidhinisha na wa kumfukuza!!!!!!!!!!!
Vyama vina nguvu kuliko maelfu ya wananchi walio poteza masaa,wakikauka kwenye jua kumpigania mbunge wao!!!!!!!
Mbunge akigombana na wananchi wake hawana ubavu wa kumtoa!!!!! Ila akigombana na kiongozi wa kikundi cha chama ananyang'anywa ubunge wake mara moja!!!!!!!!!!.pasipo kuwasikiliza wananchi wake.Hii ndiyo tafsiri ya demokrasia kwa mnao shangilia badala ya kutafakariii?
Suala jingine ni kwamba Chama chochote cha siasa ni mali ya Ummah,ndiyo maana nguvu yake ni wananchi,lakini kikubwa zaidi haviendeshwi kwa pesa zake tuu bali kodi zetu sisi wananchi,vinahudumia wananchi wake kwa kuwasemea na kuwatetea,vina milango wazi kwa watanzania siyo warwanda au popote,Kafulila ni Mtanzania,anao uhuru wa kuhoji,anao uhuru wa kuchagua chama cha kujiunga nachama chochote kikatiba.
Naskitika watu wanaoshangiria uhalamia huu wa demokrasia hewa,kweli nimeamini suala lolote la kijinga,kipuuzi na kipumbavu,makao makuu yake ni Tanzania na siyo pengine,Kila jamii inastahili ya uongozi wake,kweli Mtanzania nimeamini hawezi kuongozwa na Jamii ya kenya na ya Kenya haiwezi kuongozwa na Mtanzania.
Ingekuwa ni jamii nyingine hapa duniani ingehoji nguvu ya Chama kuzidi ya wananchi waliomchagua!!!!!!!!!!
Ni wananchi wawe na mamlaka ya mwisho?au Vyama viwe na mamlaka ya mwisho kwa mstakabali wa taifa hili?Kafulila karibu Chadema,mapambano ni safari yenye mabonde ya furaha na milima ya uvuli wa mateso na umaiti.
 
Back
Top Bottom