Zitto amefeli Leadership Qualities

Zitto amefeli Leadership Qualities

woga wenu woga wa kijinga aibu kubwa hamtaki kuambiwa ukweli udini ukabila ukanda umewajaaa,mtakosa kura kwa uzembe wenu,cdm bila zitto hakina mvuto.zitto,kitila wangemsaidia sana mbowe ambaye hana uwezo hata wa kujenga hoja ni mwanasiasa wa kurudia rudia maneno.

Ficha upumbavu kama Zitto ana uwezo mchukueni huko kwenu Ccm halafu usipende kucopy ID za watu.
cc Boko halal
 
Last edited by a moderator:
kuuumia for what?? tunarudisha nyuma mapambano ya kuiondoa CCM\
unless uje useme zitto anaipaisha CCM...just sad for chadema na mstakabali wake

afadhali yeye hawajamuua

Pole kwa Yaliyompata Zitto, inaweza isiwe ndugu yako, lakini unaweza kuwa mfuasi wake

lakini vitu vya kujiuliza hapa:

kwani wewe ni Chadema?, ulikuwa unaamini Chadema inaweza kuitoa CCM madarakani?, na ulikuwa unaamini Zitto ndio mwenye Nguvu ya kuitoa CCM Madarakani?, Kwa hiyo unaamini kwa sababu Zitto katoka basi Chadema haiwezi kamwe kuitoa CCM Madarakani?

sidhani kama ulikuwa unafata hasa siasa za Chadema, nadhani ulikuwa unafata siasa za Zitto ndani ya Chadema, na mko wengi sana
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Kichuguu, nakubakiana na wewe isipokuwa tu hapo mwisho. Zitto asingefukuzwa immediately madhara yake yangekuwa makubwa zaidi. Hakutakiwa kupewa muda. Akina Brutus walifanya makosa kumpa muda mtu kuzungumza kwenye mazishi ya Julius Caesar. Kilichotokea kila mtu anakufahamu.
 
Last edited by a moderator:
Huyu mheshimiwa kufukuzwa uanachama katika CDM sio kwamba ndo mwisho wa safari yake katika siasa cha kufanya akae atulie na kufanya uamuzi sahihi ni nini cha kufanya ili kuendeleza kujenga nchi yetu kwa sababu huyu jamaa ni msaada mkubwa sana katika nchi yetu make aliweza kuibua mambo mengi sana ambayo ni maovu yaliyofanywa na baadhi ya viongozi.

mwisho,, harakati sio chadema tu broo zitto cha msingi angalia mbele tu usigeuke nyuma kiangalia upumbavu wao huo

Ungemwambia tu akamalizie maisha ya Siasa huko CCM

Zito naamini angedumu kuwa mnyenyekevu kama enzi izo, siku moja angekuwa mgombea uraisi kupitia CDM ila kwa sasa sidhani kama ana maisha marefu ya siasa, ACT imekufa kabla hata haijatoka, Huko CCM sijui atarud kwa gear ipi
 
Zitto si wengine tulishamstukia zaidi ya miaka 7 iliyopita kuwa hafai.

Regardless of his intent, in those seven years he has done more for Tanzania than most Tanzanians, including many contributing on JF.

A list of his achievements far outweighs his shortcomings, and if we had 100 Zitto's in our Parliament, we would have a very good country, managed transparently and looking after its people.
 
Regardless of his intent, in those seven years he has done more for Tanzania than most Tanzanians, including many contributing on JF.

Yeah, he has done more to confuse folks.

A list of his achievements far outweighs his shortcomings, and if we had 100 Zitto's in our Parliament, we would have a very good country, managed transparently and looking after its people.

List them.
 
tuingalie kutumia kurunzi ya leadership qualities and skills. Baada ya kwenda mahakamani na kuweka pingamizi, zito alikuwa amejepiatia muda wa zaidi ya mwaka mmoja kujionesha kama kiongozi mzuri kwa kufanya mambo mawili tu:

(a) kuunganisha tena wanachama wa chama chake ambao walikuwa wamekorofishana kutoka na ule "mkakati;" halafu,

(b) baada ya kukamilisha hilo la (a) hapo juu angekwenda mahakani kufuta kesi na kusema sisi sote na wamoja na tuna lengo moja, malumbano hayafai kwa hiyo hakuna kesi baina yetu.

Ila inaonekana zitto alikuwa ama ana-buy time ili aendelee kuwa mbunge, au alikuwa na confidence kubwa sana kuwa atashinda kesi ambayo sote tunafahamu kuwa ameshindwa.

Ku-buy time ili aendelee kuwa mbunge siyo sifa nzuri ya uongozi kwani unakuwa ni kiongozi anayeangalia maslahi yake tu.

Vile vile kuwa na overconfidence kuwa utashinda halafu ukashindwa pia siyo sifa nzuri ya uongozi kwa utakuwa ni kiongozi atakayepeleka watu wake pabaya.

Vilevile nadhani chadema wamekurupuka sana kumtolea uamuzi kwani iwapo kweli katiba ya chadema inasema kuwa ukipeleka kesi mahakamani ukashindwa basi unavuliwa uanachama, ni afadhali wao wangekaa kimya tu ili wamuache zitto mwenyewe ndiye apime msingi ya katiba ya chama chake, tendo lake la kwenda mahakani na matokeo ya uamuzi wa mahakama.

Huna haja ya kusukuma mzoga uzidi kuzama majini kama unajua kuwa tayari hauna uhai.

binafsi naona tundu lissu amekurupuka sana.pia naona kama tundu lissu anataka awe peke yake anochowaza yeye ndio sahihi. Kukiwa na mtu mwenye uwezo kama yeye mbaye anaweza akampa challenge lazima ampige majungu mpk ang'olewe.
 
Yeah, he has done more to confuse folks.

SIo Kosa lake, washabiki wa siasa za Kitanzania wamezoea watu wa ndio mzee, watu wanaosimama wanachokiamini huishiwa kurushiwa mawe. I would rather have a politician who speaks their mind even if they are wrong, than those that hide behind the party lines, in fear of retribution.

List them.

I don't run from challenges.


  • Hoja binafsi kumwajibisha waziri mkuu, aliweza kutengeneza bipartisanship ambayo haijawahi kutokea kwenye siasa za TZ, kwa kuwafanya baadhi ya Viongozi wa CCM kukacha patry lines na kusimamia walichoamini, hii ni hatua kubwa kwa demokrasia
  • Buzwagi, akishirikiana na Slaa na wenzake, alisimamia kwa uwazi kabisa mapungufu yaliyojitokeza, yaliyosababisha tume ya mwakyembe kuundwa na kusababisha kuachia ngazi kwa viongozi wengi,akiwemo waziri mkuu-Lowasa
  • Kamati ya PAC, amekuwa akikampeni kuhusu uwazi wa mikataba na accountability ya mashirika ya umma. Kazi zake za PAC zimeshababisha watanzania wengi kujua uwepo wa CAG, nguvu ya CAG pamoja na viongozi husika kuanza kuogopa na kuheshimu ofisi ya CAG. Kabla ya hapo PAC ilikuwa kama pambo tu kwa miaka nenda rudi.
  • Sheria ya Madini, alisimamia yeye na wenzake kuhakikisha kunafanyika reform kwenye sheria hii, ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa sera ya nchi ya gesi. Kukubali kwake kufanya kazi na Viongozi wa CCM for greater good of Tanzania is what makes me appreciate his intent. Kuliko Viongozi wenzake wa CHADEMA ambao wao kutwa kucha ni kulalamika, wakati hakuna hoja binafsi hata moja yenye mashiko waliyopeleka mbelle ya bunge na kuzisimamia.
  • Kelele zake kuhusu fedha za Uswisi, ingawa zili-stumble kwa kushindwa kuproduce majina, zimesaidia kuweka mwanga kwa wananchi kuwa kuna viongozi wao wanaficha fedha nje ya nchi, leo hii hata CCM, wameanza kuambiana ukweli kuhusu hili, na tumeona PCCB kiunafki ikilichunguza hili.
  • Mengine mengi ni madogo madogo, kama kupigani haki za wasanii,kusimamia hoja ya uwepo wa uwazi wa mikataba na kupinga rushwa.

Mengi aliyoyafanya huyu bwana, yalitakiwa yafanywe na wabunge wote wa upinzani, na hasa yalitakiwa yasimamiwe na CHADEMA pamoja na wabunge wenzie wa upinzani.

Cha ajabu hawa wabunge wa upinzani kutwa kucha ni mikutano ya kukusanya wafuasi,kudai ukombozi, kuandamana na kuonesha ukamanda wao. Worse, kuna wengine wamekuwa kama CCM, ukiwauliza walichokifanya wanakuambia wamechimba visima na kugawa madawati, yani kuna wabunge wa upinzani ni vichwa maji kuliko vichwa maji wa CCM, na ingawa wengine ni vijana, wana mawazo ya kizamani kuliko Kingunge.
 
Ana options mbili tu (ZZK) za survival yake kisiasa kwa mtazamo wangu na kwa kurejea historia ya wanaCHADEMA wa dizaini yake waliondoka kwa mbwembwe na matumaini ya maisha bora zaidi kisiasa nje ya CDM kwa maana ya aidha;

Mosi ajisalimishe CCM na afuate nyayo za kina mzee Steven Masatu Wassira kwa kukopa mbinu walizozitumia hadi leo wameweza kudumu ndani ya CCM kiasi cha kuwa na nguvu kuliko hata baadhi ya wana CCM waliozaliwa humo namna ya kuenenenda na kukubalika, au;

Akubali kuwa alikosea, awaombe wenzake msamaha ndani ya chama viongozi kwa wanachama waendelee kuimarisha na kukijenga chama kufikia malengo yake japo kuna ugumu flani hasa kwa kuzingatia mambo anayotuhumiwa nayo. Nilivyowasoma wanamageuzi ndani ya CDM, ni kuwa wengi wana misimamo ya kufa mtu hasa ktk baadhi ya mambo. Ni wazi kabisa, kuna makosa ambayo mtu/mwanachama wa kariba na hadhi ya ZZK akiyafanya na ukayatambua unasameheka tu, lakini hili la KUTUMIWA NA WATAWALA CHINI YA CCM HII YA LEO KUHUJUMU CHAMA, KUHUJUMU HARAKATI ZA UKOMBOZI WA II WA MTANGANYIKA, halisameheki asilani!!

Kinyume chake ni kwamba, mara baada ya uchaguzi wa mwaka huu na kuanzia sasa baada ya tukio hili, tujiandae kusahau kabisa kuwa tulikuwa na mwanasiasa machachari, very influencial kwa vijana Zitto Kabwe!!

Hili hata si ajabu, kwa sababu tulishawahi kuwa na watu/wanasiasa wa namna hii kabla, wakafanya makosa kama alivyofanya huyu bwana mzee kwa kutokuwa smart na werevu kama hua katika harakati zake na malengo yake ya kisiasa, wakapotea.....hawako katika ramani ya kisiasa kama kina Masumbuko Lamwai, Kaborou, Thomas Ngawaiya, Tambwe Hiza wa CUF aliyehamiaga CCM akapewa wadhifa wa kuongoza kitengo cha propaganda CCM Lumumba lakini siku hizi nasikia kafungua kijiwe cha kahawa huko Kigamboni........ na wengine wengi!

Lakini kuniambia kuwa ZZK akienda ACT atawika na kubaki na nguvu za kisiasa na ushawishi wake uleule, ni kujidanganya mchana kweupe, halipo hilo!!
 
SIo Kosa lake, washabiki wa siasa za Kitanzania wamezoea watu wa ndio mzee, watu wanaosimama wanachokiamini huishiwa kurushiwa mawe. I would rather have a politician who speaks their mind even if they are wrong, than those that hide behind the party lines, in fear of retribution.

Zitto hajielewi na haeleweki. Ndo maana nikasema sisi wengine tulishaliona hilo zaidi ya miaka 7 iliyopita. Zamani nilikuwa namuunga mkono lakini akaja kunipoteza. Sasa naona CHADEMA nao wameshindwa kumvumilia na wameamua kumtimua.

Sasa subiri uone huko kwingine atakakoenda (kama ataamua kubaki kwenye siasa). Nako natabiri atawasumbua na watamtimua unless aanzishe chama chake mwenyewe (kama ACT siyo chake). Na hata akianzisha chama chake mwenyewe sidhani kama atakuwa na wafuasi wengi.

I don't run from challenges.

Awesome. Now let's go line by line.


  • Hoja binafsi kumwajibisha waziri mkuu, aliweza kutengeneza bipartisanship ambayo haijawahi kutokea kwenye siasa za TZ, kwa kuwafanya baadhi ya Viongozi wa CCM kukacha patry lines na kusimamia walichoamini, hii ni hatua kubwa kwa demokrasia

Na matokeo ya hiyo hoja yalikuwa ni yepi? Hakuna mwingine aliyekuwa na hoja kama hiyo?

  • Buzwagi, akishirikiana na Slaa na wenzake, alisimamia kwa uwazi kabisa mapungufu yaliyojitokeza, yaliyosababisha tume ya mwakyembe kuundwa na kusababisha kuachia ngazi kwa viongozi wengi,akiwemo waziri mkuu-Lowasa
Oh kumbe alishirikiana na wana-CHADEMA wenzie? Mi nilidhani labda alifanya hivyo single-handedly!

  • Kamati ya PAC, amekuwa akikampeni kuhusu uwazi wa mikataba na accountability ya mashirika ya umma. Kazi zake za PAC zimeshababisha watanzania wengi kujua uwepo wa CAG, nguvu ya CAG pamoja na viongozi husika kuanza kuogopa na kuheshimu ofisi ya CAG. Kabla ya hapo PAC ilikuwa kama pambo tu kwa miaka nenda rudi.
Hakuna wabunge wengine waliowahi kufanya hivyo?

  • Sheria ya Madini, alisimamia yeye na wenzake kuhakikisha kunafanyika reform kwenye sheria hii, ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa sera ya nchi ya gesi. Kukubali kwake kufanya kazi na Viongozi wa CCM for greater good of Tanzania is what makes me appreciate his intent. Kuliko Viongozi wenzake wa CHADEMA ambao wao kutwa kucha ni kulalamika, wakati hakuna hoja binafsi hata moja yenye mashiko waliyopeleka mbelle ya bunge na kuzisimamia.

Hizo reforms unasema alizisimamia yeye na 'wenzake'. Hao 'wenzake' ni akina nani? Again nilidhani labda alifanya hivyo singe-handedly kumbe napo alikuwa na 'wenzake' who shall remain nameless....

  • Kelele zake kuhusu fedha za Uswisi, ingawa zili-stumble kwa kushindwa kuproduce majina, zimesaidia kuweka mwanga kwa wananchi kuwa kuna viongozi wao wanaficha fedha nje ya nchi, leo hii hata CCM, wameanza kuambiana ukweli kuhusu hili, na tumeona PCCB kiunafki ikilichunguza hili.

Naam, umezipa jina kuntu kabisa kuwa ni 'kelele zake' maana bila kutaja majina mahsusi na kiasi cha pesa walichonacho huko Uswisi ni makelele tu na mimi siwezi kumpa credit kwa kelele tu.



  • Mengine mengi ni madogo madogo, kama kupigani haki za wasanii,kusimamia hoja ya uwepo wa uwazi wa mikataba na kupinga rushwa.

Haki za wasanii hata Sugu huzipigania. Kuhusu uwepo wa uwazi wa mikataba nayo wapo wengi tu ambao hujenga hoja kama hiyo. Kupinga rushwa hata CCM wapo wanaopinga rushwa. Sioni kilicho special kwa Zitto hapo.

Mengi aliyoyafanya huyu bwana, yalitakiwa yafanywe na wabunge wote wa upinzani, na hasa yalitakiwa yasimamiwe na CHADEMA pamoja na wabunge wenzie wa upinzani.

Una uhakika wabunge wote wa upinzani hakuna waliyoyafanya hayo unayodai Zitto kayafanya?


Cha ajabu hawa wabunge wa upinzani kutwa kucha ni mikutano ya kukusanya wafuasi,kudai ukombozi, kuandamana na kuonesha ukamanda wao. Worse, kuna wengine wamekuwa kama CCM, ukiwauliza walichokifanya wanakuambia wamechimba visima na kugawa madawati, yani kuna wabunge wa upinzani ni vichwa maji kuliko vichwa maji wa CCM, na ingawa wengine ni vijana, wana mawazo ya kizamani kuliko Kingunge.

Hata Zitto hana tofauti na hao unaowaponda. Pia, naye ana kashfa za tuhuma dhidi yake vilevile.

Nadhani sasa kajua kuwa hata yeye ni expendable.
 
Tatizo kuna watu hawajui wanampoteza sana Zitto kwa sifa sometimes za kijinga kabisa. Tutarudi hapa hapa kuhoji mnayo msifia .......
 

binafsi naona tundu lissu amekurupuka sana.pia naona kama tundu lissu anataka awe peke yake anochowaza yeye ndio sahihi. Kukiwa na mtu mwenye uwezo kama yeye mbaye anaweza akampa challenge lazima ampige majungu mpk ang'olewe.

Sikubaliani na wewe na ni kwa sababu moja; Hujui nafasi ya Tundu ndani chama ya kiungozi na pia katika kesi hii ilifunguliwa na Zitto ambaye in return haki wamepewa CHADEMA km chama dhidi yake!!

Na kingine, hebu suppose wewe ndiye ungekuwa ktk nafasi ya TL na ukafuatwa na waandishi wa habari ukaulizwa swali hili, "Mmeshinda kesi dhidi ya nwanachama wenu ZZK dhidi ya kukizuia chama kuchukua hatua za kumfukuza uanachama, ni nini maoni yako kama mwanasheria mkuu wa chama na hatima yake sasa baada ya maamuzi haya ya mahakama?"......Tell me, ungejibuje au ungekuwa na maoni gani bro??

BTW, chama kilishatoa maamuzi dhidi ya ZZK isipokuwa yalikuwa paused na shauri lililokuwa mahakamani tu, shauri limetolewa uamuzi then una - play CD....

That is what Tundu Lissu did!!
 
Zitto hajielewi na haeleweki. Ndo maana nikasema sisi wengine tulishaliona hilo zaidi ya miaka 7 iliyopita. Zamani nilikuwa namuunga mkono lakini akaja kunipoteza. Sasa naona CHADEMA nao wameshindwa kumvumilia na wameamua kumtimua.

Sasa subiri uone huko kwingine atakakoenda (kama ataamua kubaki kwenye siasa). Nako natabiri atawasumbua na watamtimua unless aanzishe chama chake mwenyewe (kama ACT siyo chake). Na hata akianzisha chama chake mwenyewe sidhani kama atakuwa na wafuasi wengi.

Mimi sio mganga wa kienyeji, hizo hadithi za utabiri nitakuachia wewe na hao wa sampuli hiyo. I stick to verifiable facts.

Awesome. Now let's go line by line.
Na matokeo ya hiyo hoja yalikuwa ni yepi? Hakuna mwingine aliyekuwa na hoja kama hiyo?

Matokeo Waziri mkuu alibaki, lakini ilijenga precedent ambayo ni muhimu kwa siasa za Tanzania, kuwa Waziri mkuu can be removed, if deemed incompetent. Sitegemei wewe kuelewa umuhimu wa precedent, kama umeamua kuona hilo ni jambo dogo, Sikumbuki on top of my head, but i can confidently say, hakuna aliyepeleka hoja kam hiyo toka upinzani Tanzania kwa miaka 20 kadhaa ya upinzani. So, yes, for an MP, this is an achievement.

Oh kumbe alishirikiana na wana-CHADEMA wenzie? Mi nilidhani labda alifanya hivyo single-handedly!
Hakuna wabunge wengine waliowahi kufanya hivyo?
Uliuliza Mafanikio ya Zitto, sasa mbona unaanza kusogeza goli?hakuna binadamu anayefanya kazi peke yake, hata mcheza tennis akishinda anashukuru timu yake na sponsors.it's the gentleman thing to do. Wabunge wa CHADEMA waliowahi kuleta hoja za Kitaifa zilizozizima mwaka mzima na viongozi wakuu wa serikali kuwajibika hawajai kiganja kimoja cha mkono, kama unakataa hilo umeamua tu kukataa. Kama unawajua wataje hapa, kinyume na hapo hizo zitakuwa chuki binafsi kwa mafanikio yaliyo wazi.

Hizo reforms unasema alizisimamia yeye na 'wenzake'. Hao 'wenzake' ni akina nani? Again nilidhani labda alifanya hivyo singe-handedly kumbe napo alikuwa na 'wenzake' who shall remain nameless....
Kila kiongozi wa taasisi ana haki ya kimsingi ku-take credit ya mafanikio ya taasisi anayoiongoza, yeye kama mwenye kiti wa PAC, ni haki yake ya kimsingi kuhusishwa na mafanikio ya kamati anayoiongozam unajua kuna kamati ngapi bungeni? unaweza taja kamati 5 tu zenye level ya public impact and awareness kuzidi PAC? humu ndani kila mtu yuko tayari kumrushia JK lawama, wakati anaongoza nchi yenye viongozi maelfu kwa maelfu,kwa nini?kwa sababu siku zote the buck stops at the top. Usijifanye hujui hili, you are better than that. Stop playing dumb please.

Naam, umezipa jina kuntu kabisa kuwa ni 'kelele zake' maana bila kutaja majina mahsusi na kiasi cha pesa walichonacho huko Uswisi ni makelele tu na mimi siwezi kumpa credit kwa kelele tu.
Sometimes, kelele is better than keeping quite, i respect a politician who says what they believe than one that hide behind neutral and party lines. Hizi Kelele kuna taasisi zimeundwa kwa ajili ya kupiga hizi kelele, Twaweza comes ti mind. Kelele ni jambo muhimu sana kwenye demokrasia na utawala bora. Sasa hivi kila kiongozi anayetaka kuweka fedha Uswisi atajifikiria mara mbili, kwangu hii ni hatua na mafanikio ya mpiga kelele.angekaa kimya kusingekuwa na uwazi uliopo sasa ambao hadi head of PCCB yuko obliged kuchunguza hizi fedha na kuzitolea ufafanuzi kwa PAC pamoja na mihimili mengine ya serikali.

Haki za wasanii hata Sugu huzipigania. Kuhusu uwepo wa uwazi wa mikataba nayo wapo wengi tu ambao hujenga hoja kama hiyo. Kupinga rushwa hata CCM wapo wanaopinga rushwa. Sioni kilicho special kwa Zitto hapo.

Shida yako unataka mafanikio ya ZITTO yawe null and void the moment wahusika wengine wakiwa na mafanikio yanayofanana, guess what, the world does not work like that. Federer being a a grandslam champion does not make nadal any less of a champion, it makes them both champions, This is not a zero sum game where only one can and must exists.This is too petty from you.

Una uhakika wabunge wote wa upinzani hakuna waliyoyafanya hayo unayodai Zitto kayafanya?

Wako wachache sana, na hawajai viganja vya mkono nikiwahesabu, kama unadhani nadanganya au siko sahihi si vibaya ukayataja majina yao hapa kila mtu aweke maoni yake, unaogopa nini kuwataja?

Hata Zitto hana tofauti na hao unaowaponda. Pia, naye ana kashfa za tuhuma dhidi yake vilevile.

Hakuna sehemu nimesema ZITTO hana mabaya yake, nimesema mapungufu yake yanazidiwa na mazuri, kutokana na ubora wa mambo mazuri aliyoyafanya kama mbunge wa upinzani na mwanasiasa wa Tanzania.

Nadhani sasa kajua kuwa hata yeye ni expendable.
Politically, this is not a win for CHADEMA, they are not better without him and they know it. We have seen what happened the year after they sidelined him, the best they could do was align themselves with UKAWA, and the best political event of the year came from two politicans they dismissed from CHADEMA, Zitto and Kafulila.

I don't see how ZITTO is being expendable here..,
 
Tuingalie kutumia kurunzi ya leadership qualities and skills. Baada ya kwenda mahakamani na kuweka pingamizi, Zito alikuwa amejepiatia muda wa zaidi ya mwaka mmoja kujionesha kama kiongozi mzuri kwa kufanya mambo mawili tu:

(a) Kuunganisha tena wanachama wa chama chake ambao walikuwa wamekorofishana kutoka na ule "Mkakati;" halafu,

(b) Baada ya kukamilisha hilo la (a) hapo juu angekwenda mahakani kufuta kesi na kusema sisi sote na wamoja na tuna lengo moja, malumbano hayafai kwa hiyo hakuna kesi baina yetu.

Ila inaonekana Zitto alikuwa ama ana-buy time ili aendelee kuwa mbunge, au alikuwa na confidence kubwa sana kuwa atashinda kesi ambayo sote tunafahamu kuwa ameshindwa.

Ku-buy time ili aendelee kuwa mbunge siyo sifa nzuri ya uongozi kwani unakuwa ni kiongozi anayeangalia maslahi yake tu.

Vile vile kuwa na overconfidence kuwa utashinda halafu ukashindwa pia siyo sifa nzuri ya uongozi kwa utakuwa ni kiongozi atakayepeleka watu wake pabaya.

Vilevile nadhani CHADEMA wamekurupuka sana kumtolea uamuzi kwani iwapo kweli katiba ya CHADEMA inasema kuwa ukipeleka kesi mahakamani ukashindwa basi unavuliwa uanachama, ni afadhali wao wangekaa kimya tu ili wamuache Zitto mwenyewe ndiye apime msingi ya katiba ya chama chake, tendo lake la kwenda mahakani na matokeo ya uamuzi wa mahakama.

Huna haja ya kusukuma mzoga uzidi kuzama majini kama unajua kuwa tayari hauna uhai.

Angefanya vipi hayo yote unayopendekeza wakati Idara ya Usalama (TISS) na makada wakubwa wa ccm wanampumulia mgongoni wakitaka atimize masharti waliyopeana ya kukimaliza CHADEMA before 2013??!!!
 
Kuna jambo moja unajisahau. kuwA makini au kua star ndani ya chama hakumaanishi ukivunja katiba usiwAjibishwe.kama unampenda zito zaidi ya chadema kanywe nae kahawa
 
Sometimes, kelele is better than keeping quite, i respect a politician who says what they believe than one that hide behind neutral and party lines. Hizi Kelele kuna taasisi zimeundwa kwa ajili ya kupiga hizi kelele, Twaweza comes ti mind. Kelele ni jambo muhimu sana kwenye demokrasia na utawala bora. Sasa hivi kila kiongozi anayetaka kuweka fedha Uswisi atajifikiria mara mbili, kwangu hii ni hatua na mafanikio ya mpiga kelele.angekaa kimya kusingekuwa na uwazi uliopo sasa ambao hadi head of PCCB yuko obliged kuchunguza hizi fedha na kuzitolea ufafanuzi kwa PAC pamoja na mihimili mengine ya serikali.

Chifu, hili la fedha za Uswisi si ni Zitto huyo huyo alipoulizwa na AG Werema (kwenye kamati) kuhusu majina akasema hana, ama?! Sasa hapo anastahili sifa ya nini wakati alikuwa akidanganya raia??

Sasa kiongozi atajifikiria mara mbili vipi wakati jamaa yako hata jina moja hakuwa nalo. Na pia kwani hukusikia tena juzi juzi hapa benki moja ya Uswisi ilitoa taarifa za fedha za waafrika (wakiwemo watanzania) zilizomo kwenye benki hiyo?

Kuna msemo kuwa kelele za chura hazimzuii tembo kunywa maji, nafikiri unaupata.


Politically, this is not a win for CHADEMA, they are not better without him and they know it. We have seen what happened the year after they sidelined him, the best they could do was align themselves with UKAWA, and the best political event of the year came from two politicans they dismissed from CHADEMA, Zitto and Kafulila.

Ebu toa evidence kuonyesha "they are not better without him..." Na onyesha "what happened the year they sidelined him"

Pamoja na hao kuwasidelined kama unavyodai, matokeo ya serikali za mitaa yanakuumbua chifu. Kwani UKAWA imefanya vizuri kuliko ilivyowahi kutokea katika siasa za vyama vingi. Sasa kwa kutumia mfano huu (ambao ndiyo muhimu katika siasa), unapata guts za kusema "they are not better without him"??? How better do you them to be?!??
 
kuuumia for what?? tunarudisha nyuma mapambano ya kuiondoa CCM\
unless uje useme zitto anaipaisha CCM...just sad for chadema na mstakabali wake

afadhali yeye hawajamuua

Chifu, hiyo ni tuhuma nzito sana. Unataka kusema CHADEMA kilishawahi kuua mtu? Kilishitakiwa kwa mauaji hayo?
 
lengo la zitto kwenda mahakamani ilikuwa kulinda vyeo vyake vya kibunge . yaani ubunge wenyewe na uongozi wa PAC baaasi .
 
Mimi sio mganga wa kienyeji, hizo hadithi za utabiri nitakuachia wewe na hao wa sampuli hiyo. I stick to verifiable facts.

No problem at all.

Matokeo Waziri mkuu alibaki, lakini ilijenga precedent ambayo ni muhimu kwa siasa za Tanzania, kuwa Waziri mkuu can be removed, if deemed incompetent.

Hold up, wait a minute. So the Premier stayed on but yet a precedent was set that a prime minister can be removed if deemed incompetent? You are contradicting yourself now. How can a precedent of removing a prime minister be set if the prime minister stayed?

Sitegemei wewe kuelewa umuhimu wa precedent,

Ni wazi hujui hata maana ya precedent!!!!!!!!!!!

kama umeamua kuona hilo ni jambo dogo,

Jambo kuwa kubwa kwako si lazima liwe kubwa kwangu. Unajua maana ya precedent wewe?

Sikumbuki on top of my head,

'off the top of my head' - source

but i can confidently say, hakuna aliyepeleka hoja kam hiyo toka upinzani Tanzania kwa miaka 20 kadhaa ya upinzani. So, yes, for an MP, this is an achievement.

You are a bundle of contradictions! One minute you say you don't remember off the top of your head and the next minute you say you "can confidently say" no one else from the opposition had a similar argument? You are a trip!

Uliuliza Mafanikio ya Zitto, sasa mbona unaanza kusogeza goli?

Nimelisogeza wapi?

hakuna binadamu anayefanya kazi peke yake, hata mcheza tennis akishinda anashukuru timu yake na sponsors.

Twaib, hapo tu pamoja.

it's the gentleman thing to do.

It's the gentleman thing to do? Hapo unatafsiri 'uungwana' au....? Kwamba kufanya hivyo ni jambo la kiungwana?

Wabunge wa CHADEMA waliowahi kuleta hoja za Kitaifa zilizozizima mwaka mzima

Utaje huo mwaka na taja hizo hoja zililetwa lini mpaka lini ili nione kama kweli zilizizima (is that even a word?) mwaka mzima.

na viongozi wakuu wa serikali kuwajibika hawajai kiganja kimoja cha mkono,

Viongozi gani wakuu wa serikali waliwajibika kutokana na hoja za Zitto?

kama unakataa hilo umeamua tu kukataa.

Hapana, si hivyo hata kidogo. Hapa ni mwendo wa ithibati tu.

Kama unawajua wataje hapa, kinyume na hapo hizo zitakuwa chuki binafsi kwa mafanikio yaliyo wazi.

Usinigeuzie kibao mimi.

Kila kiongozi wa taasisi ana haki ya kimsingi ku-take credit ya mafanikio ya taasisi anayoiongoza, yeye kama mwenye kiti wa PAC, ni haki yake ya kimsingi kuhusishwa na mafanikio ya kamati anayoiongozam unajua kuna kamati ngapi bungeni? unaweza taja kamati 5 tu zenye level ya public impact and awareness kuzidi PAC? humu ndani kila mtu yuko tayari kumrushia JK lawama, wakati anaongoza nchi yenye viongozi maelfu kwa maelfu,kwa nini?kwa sababu siku zote the buck stops at the top. Usijifanye hujui hili, you are better than that. Stop playing dumb please.

Hahaaaa okay, but I'm not playing dumb. Don't get defensive when you can't answer a question. And it's okay to say 'I don't know' when you don't know.

Sometimes, kelele is better than keeping quite,

Like when is making noise better than keeping quiet?

i respect a politician who says what they believe than one that hide behind neutral and party lines.

But how do you know for fact that what they say is actually what they believe and not just talk to aimed at scoring popularity points?

Hizi Kelele kuna taasisi zimeundwa kwa ajili ya kupiga hizi kelele, Twaweza comes ti mind. Kelele ni jambo muhimu sana kwenye demokrasia na utawala bora.

Sawa, hilo nakubali.

Sasa hivi kila kiongozi anayetaka kuweka fedha Uswisi atajifikiria mara mbili,

Hapo awali kuna kiongozi gani aliyeweka fedha zake Uswisi?

kwangu hii ni hatua na mafanikio ya mpiga kelele.angekaa kimya kusingekuwa na uwazi uliopo sasa ambao hadi head of PCCB yuko obliged kuchunguza hizi fedha na kuzitolea ufafanuzi kwa PAC pamoja na mihimili mengine ya serikali.

Hapo unajidhihirisha tu jinsi viwango vyako vilivyo chini. Unakuwa impressed na vitu vidogo vidogo mno. Huna tofauti na wale wanaoita wenzao 'vichwa' kwa kuongea mambo ya kawaida kabisa.

Shida yako unataka mafanikio ya ZITTO yawe null and void the moment wahusika wengine wakiwa na mafanikio yanayofanana, guess what, the world does not work like that.

Not sure exactly what you are talking about there.

Federer being a a grandslam champion does not make nadal any less of a champion, it makes them both champions, This is not a zero sum game where only one can and must exists.This is too petty from you.

Okay....

Wako wachache sana, na hawajai viganja vya mkono nikiwahesabu, kama unadhani nadanganya au siko sahihi si vibaya ukayataja majina yao hapa kila mtu aweke maoni yake, unaogopa nini kuwataja?

Wewe ndo unadai wako wachache sana na kwamba hawajai kwenye viganja vya mikono ukiwahesabu. Kwa kusema hivyo natumai utakuwa unawajua maana unaweza hata kuwahesabu.

Nitajie basi hao wachache wasioweza kujaa viganjani?

Hakuna sehemu nimesema ZITTO hana mabaya yake, nimesema mapungufu yake yanazidiwa na mazuri, kutokana na ubora wa mambo mazuri aliyoyafanya kama mbunge wa upinzani na mwanasiasa wa Tanzania.

Nami sikusema umesema Zitto hana mabaya. Unajihami bure tu.

Politically, this is not a win for CHADEMA,

The jury is still out on that so we shall see.

they are not better without him and they know it.

I think they are 10 times better now. And dare I say it was good riddance to bad rubbish.

We have seen what happened the year after they sidelined him, the best they could do was align themselves with UKAWA, and the best political event of the year came from two politicans they dismissed from CHADEMA, Zitto and Kafulila.

Best political event of the year? What was that?

I don't see how ZITTO is being expendable here..,

CHADEMA can go on without him. He is expendable.
 
Back
Top Bottom