Kituko
JF-Expert Member
- Jan 12, 2009
- 9,555
- 9,368
Vilevile nadhani CHADEMA wamekurupuka sana kumtolea uamuzi kwani iwapo kweli katiba ya CHAEMA inasema kuwa ukipeleka kesi mahakamani ukashindwa basi unavuliwa uanachama, ni afadhali wao wangekaa kimya tu ili wamuache Zito mwenyewe ndiye apime msingi ya katiba ya chama chake, tendo lake la kwenda mahakani na matokeo ya uamuzi wa mahakama. Huna haja ya kusukuma mzoga uzidi kuzama majini kama unajua kuwa tayari hauna uhai.
Kaka Kichuguu, Hapo CHADEMA hawajakurupuka, ila wamemuwahi Zitto, kwa vyovyote vile ilikuwa ni vigumu kwa Zitto kuendelea kuwa ndani ya Chadema, Zitto haelewani na almost top layer yote ya chama (Slaa, Lissu na hata Mbowe kwa sasa) sasa atafanyaje siasa zake humo,
timing ya Zitto ilikuwa ni yeye kuwapiga chini Chadema na kweli angefanikiwa kwenye hilo yeye ndio angeonekana kaiacha Chadema na kisiasa angalau angepata Kanguvu fulani ka kusimamia,
1. Chadema wamewahi kumfukuza Zitto ili angalau wamzoofishe kisiasa kokote aendako na kwa Wananchi kwa ujumla,
2. Chadema wanaionyesha Jamii kuwa Zitto ni Mwanasiasa Mzuri lakini sio Mwaminifu,
3. Chadema wanaionyesha jamii kuwa wao wanauwezo wa Kufanya maamuzi magumu
4. Chadema wanaionyesha Jamii kuwa hakuna mtu ambaye yuko juu ya Chama,
5. Chadema wanaionyesha jamii kuwa hakuna mtu mwenye mamlaka ya kufunja katiba bila kushughulikiwa